Wito: Hoja za Kisheria za TLS, Prof. Shivji na wengine wote kupinga IGA, zisijibiwe Kisiasa kwa maneno matupu!, zijibiwe Kisheria kwa Vifungu!

Wito: Hoja za Kisheria za TLS, Prof. Shivji na wengine wote kupinga IGA, zisijibiwe Kisiasa kwa maneno matupu!, zijibiwe Kisheria kwa Vifungu!

Huyu ndio wewe pachal mayala ila sio lile lidudu lingine lenye ujumbe wa uchawa, hapa ndio wewe sasa akili safi sio huko kwingine unakojipeleka. Simamia hapa tu.

Hawa ngedere wa kizanzibar ni majambazi
 
Wanabodi,
Mjadala wa IGA ya DPW kupewa Bandari yetu ya Dar es Salaam, unazidi kushika kasi.

Jana asubuhi nilipandisha bandiko hili Bunge, Serikali na Mahakama, Sio Mungu, Sio Malaika, Zinaweza Kukosea!. Zinapokosea, Zina Wajibu Kurekebisha na Kutenda Haki, Vinginevyo Karma Will Do kuhusu hiyo IGA.

Jana hiyo hiyo ikatokea coincidentally Jukwaa la Wahariri likawaita wahusika wakuu kwenye mkutano na Wahariri, na kujibu maswali ya Wahariri.

Kwanza niwapongeze TEF kwa initiative hiyo, mkutano huo uliotangazwa live na media zetu mainstream na social media, umelisaidia sana taifa katika uelimishaji umma kuhusu jambo hili.

Tangu sakata hili lianze, serikali yetu haijawahi kuwa proactive hata mara moja kwa kujitokeza kuelimisha umma, siku zote, ni inakuwa reactive kujitokeza kujibu hoja.

Miongoni mwa wajibu hoja huo mkutano wa jana ni Wanasheria, kiongozi wa Jopo la Wanasheria, Hamza Johari na Mwanasheria wa Wizara.

Bandiko hili ni wito kwa serikali yetu tukufu na Sikivu, IGA imepingwa kwenye fronts kuu mbili, hoja za Kisiasa, na hoja za Kisheria.

Kwenye hoja za kisiasa ni watu mbalimbali wameibuka ama kuunga mkono ama kuipinga kwa hoja za kisiasa, hoja hizi zikijibiwa kisiasa ni sawa.

Lakini kuna hoja very solid za kisheria zilizotolewa na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, TLS, na hoja nyingine nyingi za kisheria zilizoibuliwa na wanasheria mbalimbali, akiwemo Prof. Shivji, Rugemeleza Nshala, Mwambukusi na mawakili wengine wengi.

Hoja hizi za kisheria zimetolewa kwa maandishi zikiandamana na vifungu vya kisheria. Jana nimesikia zikijibiwa kwa kauli nyepesi nyepesi za kisiasa za maneno matupu bila vifungu vya kisheria to back up majibu hayo.

Natoa wito kwa serikali yetu Sikivu, hoja zote za kisheria kuuipinga IGA zilizotolewa kwa maandishi zikiwemo hoja za TLS, Prof. Shivji na Wengine wote Kupinga IGA, zisijibiwe kisiasa kwa kauli tuu nyepesi nyepesi za maneno maneno matupu!, hoja hizi nzito za kisheria, zijibiwe kisheria kwa maandishi zikiambatana na vifungu!.

Kufuatia IGA hii, katika kuiunga mkono, kumejitokeza wanasheria chawa wanaofanya uchawa wa kisheria kuitetea hii IGA.

Na mimi kwa vile ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, nami nilitoa hoja zangu kuhusu hii IGA Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! ambazo baadhi mpaka sasa bado hazijajibiwa popote!.
Kwa vile IGA ni utangulizi wa HGA, naomba kuendelea kuwapa matumaini Watanzania kuwa kwa kelele hizi, HGA, itakuwa nzuri.

Serikali Ijibu Hoja.
Paskali
Naunga mkono hoja ✔️ ingawa hawawez jibu article by article kisheria.
 
Hili jambo halikupangika vyema. Ndio maana hawawezi kuwa na majibu hayo ya kisheria.

Tuanza na makosa tu ktk hiyo nyaraka;
1. Ile power of attorney ya mh. Rais, inavyosomeka ni kwamba inampa Waziri Mbarawa kusaini kwa niaba ya Tz na Dubei. Sasa hilo wanajibuje? Kwamba ilikosewa?
2. Hiyo IGA, wahusika wote wa upande wa Dubei, hawaeleweki, majina, vyeo, kuna saini tu. Ni kina nani?
3. IGA ni kati nchi na nchi, Sisi Rais kaonekana kwenye nyaraka, Waziri, kaonekana, na kuna sehemu PS wa wizara kaonekana, wao yupo mkurugenzi wa bandari (DP WORLD), hii ni kampuni tu. Wa Dubei wako wapi?! Unajibuje hilo ..
4. Power of Attorney upande ule alopewe huyo Mkurugenzi wa bandari Dubei, kapewa na nani?! Ukiisoma unaona juu tu, stamp ya Government of Dubei. Ni nani katika serikali ya Dubai, kampa hiyo nguvu,? Cheo na majina na signature, havipo? Mbona sisi Mh Samia kaonekana. Unajibu hili?
5. Zile hoja za huyu mwekezaji kupewa Land Rights na sheria za ufidiaji kinyume na sheria zetu za Ardhi, unazijibuje?!
6. Alisema Prof. Shivji, wao DP World wamepewa haki zote za mkataba, sisi Tanzania tumechukua wajibu wote wa mkataba. Yeye haonekani ktk kipengele chochote akiwa na wajibu. Ni nini hiki?!
7. Wanasema wakienda usuluhishi huko S. Afrika , sheria inayotumika ni "Laws of England". Hii inakinzana na sheria zetu zote. Unajibuje hilo?!
8. Mchakato wa tender ulitangazwa kwa tangazo lipi? Waweke wazi,

Mambo ni mengi sana.

Hili jambo ni zito.
Hili jambo si zito kihivyo, bali kunamaslahi ya wafaidika wa mfumo wa uendeshaji wa Bandari uliopo, hawataki mabadiliko.
Lakini Serikali inalazimika kuleta mabadiliko ili kuongeza pato la Taifa. from 7 Trilion mpaka 24 Trilion kwa mwaka
si haba.

Upoteaji wa Makontena Upo sasa TZ DSM lakin akija TP World hautakuwepo tena, Hiyo ndiyo shida iliyopo.
Sijui na wewe Pascal Ni Mnufaika ? au mpiga debe tuu?
Mimi namuunga Mkono Mama na Wasaidizi wake , naona wanaenda vizuri ili kuleta mapinduzi ya Uchumi wa kisasa wenye Ajira za kutosha na pato kwa taifa na Mtu mmoja mmoja.
Mimi Nataraja kununua Hisa za DP World zitakapo nadishwa ,le ya kwetu 35%
 
Hili jambo halikupangika vyema. Ndio maana hawawezi kuwa na majibu hayo ya kisheria.

Tuanza na makosa tu ktk hiyo nyaraka;
1. Ile power of attorney ya mh. Rais, inavyosomeka ni kwamba inampa Waziri Mbarawa kusaini kwa niaba ya Tz na Dubei. Sasa hilo wanajibuje? Kwamba ilikosewa?
2. Hiyo IGA, wahusika wote wa upande wa Dubei, hawaeleweki, majina, vyeo, kuna saini tu. Ni kina nani?
3. IGA ni kati nchi na nchi, Sisi Rais kaonekana kwenye nyaraka, Waziri, kaonekana, na kuna sehemu PS wa wizara kaonekana, wao yupo mkurugenzi wa bandari (DP WORLD), hii ni kampuni tu. Wa Dubei wako wapi?! Unajibuje hilo ..
4. Power of Attorney upande ule alopewe huyo Mkurugenzi wa bandari Dubei, kapewa na nani?! Ukiisoma unaona juu tu, stamp ya Government of Dubei. Ni nani katika serikali ya Dubai, kampa hiyo nguvu,? Cheo na majina na signature, havipo? Mbona sisi Mh Samia kaonekana. Unajibu hili?
5. Zile hoja za huyu mwekezaji kupewa Land Rights na sheria za ufidiaji kinyume na sheria zetu za Ardhi, unazijibuje?!
6. Alisema Prof. Shivji, wao DP World wamepewa haki zote za mkataba, sisi Tanzania tumechukua wajibu wote wa mkataba. Yeye haonekani ktk kipengele chochote akiwa na wajibu. Ni nini hiki?!
7. Wanasema wakienda usuluhishi huko S. Afrika , sheria inayotumika ni "Laws of England". Hii inakinzana na sheria zetu zote. Unajibuje hilo?!
8. Mchakato wa tender ulitangazwa kwa tangazo lipi? Waweke wazi,

Mambo ni mengi sana.

Hili jambo ni zito.
Jana niliwaonea huruma wale wataalam wa mbarawa wanavyojichanganya huku na kule ,kwa kifupi mkanganyiko ndo umeongezeka zaidi badala ya kupungua
 
Kama kilichowekwa hadharani kina kasoro cha sirini je?
Mungu ni fundi ndio maana uso unavutia Ila sehemu za Siri hazivutii mkuu! Elewa hapo Tu.
Nafikiria pia ule mkataba wa LNG aliosaini makamba si utakuwa ni kituko cha mwaka kama huu ndo upo hivi
 
Kama Ticts walikuwa Bandarini kwa almost 20 years na bado bandari haikuperform basi tatizo sio uwekezaji bali ni sisi wenyewe. 💉🔨
Ajabu unaiacha kampuni ina operate 20 years halafu unakuja sema haiku perform. Performance haikuwa criteria ya kuruhusu kuendelea na kazi?
 
Hakuna hoja iliyotolewa ambayo haijajibiwa hadi sasa.

Kinachotokea sasa sio kwamba Serikali haijajibu ila watu wameamua kuamini pande wanayoona waiamini hata kama wamepewa maelezo sahihi. Na hii ni Siasa.

Serikali imeshatoa maelekezo na sasa haipaswi kutumia muda kujieleza tena. Inatakiwa iendelee na taratibu za kukamilisha makubaliano na mikataba mingine maana wakati ni ukuta.
Weka majibu ya hizo hoja hapa.
 
Jana niliwaonea huruma wale wataalam wa mbarawa wanavyojichanganya huku na kule ,kwa kifupi mkanganyiko ndo umeongezeka zaidi badala ya kupungua
Wangekuwa watu wa kufikiri vyema, wangejipa muda, waandae hoja zote na kuandika majibu, yani wajipe muda, ila daah. Mara teknolojia kubwa, mitambo, mara ajira hazitakoma. Mara hakuna mkataba wa utekelezaji, mara kuna 35% anamiliki Mtanzania, yani ni mix mataputapu.
 
Exactly!

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Kama Ticts walikuwa Bandarini kwa almost 20 years na bado bandari haikuperform basi tatizo sio uwekezaji bali ni sisi wenyewe. [emoji382][emoji375]
Uwekezaji chini ya huyu mama halafu unategemea mafanikio ni uongo .wwkazaji kama unatabia ya kutofuatilia ni kazi bure. Mfano tics walikuwa wanalipa kama 10bil hivi magufuli alipo kuja hela ikapanda mpaka 20b hivi
 
Wangekuwa watu wa kufikiri vyema, wangejipa muda, waandae hoja zote na kuandika majibu, yani wajipe muda, ila daah. Mara teknolojia kubwa, mitambo, mara ajira hazitakoma. Mara hakuna mkataba wa utekelezaji, mara kuna 35% anamiliki Mtanzania, yani ni mix mataputapu.
Pawa of instruments aliyopewa mbarawa jamaa ameruka ruka ww alipofika kumalizia akaparuka ,jamaa wakamwambia amesoma nunusu ,jamaa akagoma kumalizia pale ilipoandikwa ,wakamuomba akagoma kabisa
 
Wanabodi,
Mjadala wa IGA ya DPW kupewa Bandari yetu ya Dar es Salaam, unazidi kushika kasi.

Jana asubuhi nilipandisha bandiko hili Bunge, Serikali na Mahakama, Sio Mungu, Sio Malaika, Zinaweza Kukosea!. Zinapokosea, Zina Wajibu Kurekebisha na Kutenda Haki, Vinginevyo Karma Will Do kuhusu hiyo IGA.

Jana hiyo hiyo ikatokea coincidentally Jukwaa la Wahariri likawaita wahusika wakuu kwenye mkutano na Wahariri, na kujibu maswali ya Wahariri.

Kwanza niwapongeze TEF kwa initiative hiyo, mkutano huo uliotangazwa live na media zetu mainstream na social media, umelisaidia sana taifa katika uelimishaji umma kuhusu jambo hili.

Tangu sakata hili lianze, serikali yetu haijawahi kuwa proactive hata mara moja kwa kujitokeza kuelimisha umma, siku zote, ni inakuwa reactive kujitokeza kujibu hoja.

Miongoni mwa wajibu hoja huo mkutano wa jana ni Wanasheria, kiongozi wa Jopo la Wanasheria, Hamza Johari na Mwanasheria wa Wizara.

Bandiko hili ni wito kwa serikali yetu tukufu na Sikivu, IGA imepingwa kwenye fronts kuu mbili, hoja za Kisiasa, na hoja za Kisheria.

Kwenye hoja za kisiasa ni watu mbalimbali wameibuka ama kuunga mkono ama kuipinga kwa hoja za kisiasa, hoja hizi zikijibiwa kisiasa ni sawa.

Lakini kuna hoja very solid za kisheria zilizotolewa na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, TLS, na hoja nyingine nyingi za kisheria zilizoibuliwa na wanasheria mbalimbali, akiwemo Prof. Shivji, Rugemeleza Nshala, Mwambukusi na mawakili wengine wengi.

Hoja hizi za kisheria zimetolewa kwa maandishi zikiandamana na vifungu vya kisheria. Jana nimesikia zikijibiwa kwa kauli nyepesi nyepesi za kisiasa za maneno matupu bila vifungu vya kisheria to back up majibu hayo.

Natoa wito kwa serikali yetu Sikivu, hoja zote za kisheria kuuipinga IGA zilizotolewa kwa maandishi zikiwemo hoja za TLS, Prof. Shivji na Wengine wote Kupinga IGA, zisijibiwe kisiasa kwa kauli tuu nyepesi nyepesi za maneno maneno matupu!, hoja hizi nzito za kisheria, zijibiwe kisheria kwa maandishi zikiambatana na vifungu!.

Kufuatia IGA hii, katika kuiunga mkono, kumejitokeza wanasheria chawa wanaofanya uchawa wa kisheria kuitetea hii IGA.

Na mimi kwa vile ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, nami nilitoa hoja zangu kuhusu hii IGA Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! ambazo baadhi mpaka sasa bado hazijajibiwa popote!.
Kwa vile IGA ni utangulizi wa HGA, naomba kuendelea kuwapa matumaini Watanzania kuwa kwa kelele hizi, HGA, itakuwa nzuri.

Serikali Ijibu Hoja.
Paskali
Naunga mko hoja kwa asilimia 101 na naunga mkono uwekezaji wa miaka 1000. Ilimradi HGA itakuwa nzuri.
 
Wanabodi,
Mjadala wa IGA ya DPW kupewa Bandari yetu ya Dar es Salaam, unazidi kushika kasi.

Jana asubuhi nilipandisha bandiko hili Bunge, Serikali na Mahakama, Sio Mungu, Sio Malaika, Zinaweza Kukosea!. Zinapokosea, Zina Wajibu Kurekebisha na Kutenda Haki, Vinginevyo Karma Will Do kuhusu hiyo IGA.

Jana hiyo hiyo ikatokea coincidentally Jukwaa la Wahariri likawaita wahusika wakuu kwenye mkutano na Wahariri, na kujibu maswali ya Wahariri.

Kwanza niwapongeze TEF kwa initiative hiyo, mkutano huo uliotangazwa live na media zetu mainstream na social media, umelisaidia sana taifa katika uelimishaji umma kuhusu jambo hili.

Tangu sakata hili lianze, serikali yetu haijawahi kuwa proactive hata mara moja kwa kujitokeza kuelimisha umma, siku zote, ni inakuwa reactive kujitokeza kujibu hoja.

Miongoni mwa wajibu hoja huo mkutano wa jana ni Wanasheria, kiongozi wa Jopo la Wanasheria, Hamza Johari na Mwanasheria wa Wizara.

Bandiko hili ni wito kwa serikali yetu tukufu na Sikivu, IGA imepingwa kwenye fronts kuu mbili, hoja za Kisiasa, na hoja za Kisheria.

Kwenye hoja za kisiasa ni watu mbalimbali wameibuka ama kuunga mkono ama kuipinga kwa hoja za kisiasa, hoja hizi zikijibiwa kisiasa ni sawa.

Lakini kuna hoja very solid za kisheria zilizotolewa na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, TLS, na hoja nyingine nyingi za kisheria zilizoibuliwa na wanasheria mbalimbali, akiwemo Prof. Shivji, Rugemeleza Nshala, Mwambukusi na mawakili wengine wengi.

Hoja hizi za kisheria zimetolewa kwa maandishi zikiandamana na vifungu vya kisheria. Jana nimesikia zikijibiwa kwa kauli nyepesi nyepesi za kisiasa za maneno matupu bila vifungu vya kisheria to back up majibu hayo.

Natoa wito kwa serikali yetu Sikivu, hoja zote za kisheria kuuipinga IGA zilizotolewa kwa maandishi zikiwemo hoja za TLS, Prof. Shivji na Wengine wote Kupinga IGA, zisijibiwe kisiasa kwa kauli tuu nyepesi nyepesi za maneno maneno matupu!, hoja hizi nzito za kisheria, zijibiwe kisheria kwa maandishi zikiambatana na vifungu!.

Kufuatia IGA hii, katika kuiunga mkono, kumejitokeza wanasheria chawa wanaofanya uchawa wa kisheria kuitetea hii IGA.

Na mimi kwa vile ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea, nami nilitoa hoja zangu kuhusu hii IGA Japo Bunge Limeridhia, DPW Kuendesha Bandari Zetu, ni Makubaliano Tu, Tukithibisha Kuna Matatizo, Tunarekebisha Mkataba wa HGA, Kazi Nzuri Iendelee! ambazo baadhi mpaka sasa bado hazijajibiwa popote!.
Kwa vile IGA ni utangulizi wa HGA, naomba kuendelea kuwapa matumaini Watanzania kuwa kwa kelele hizi, HGA, itakuwa nzuri.

Serikali Ijibu Hoja.
Paskali
Leo umeeleweka, Tulia kule Mbeya kwao akiwa Mtaalam wa sheria na mkuu wa Mhimili wa wanainch wa Bunge, alipigha siasa kuhusu huu MKATABA BADALA YA KUJIBU VIFUNGU KISHERIA, Paskali kuna wakati unakua wazi,leo nakupa hongera sana. Serikali ijibu hoja sio blabla!!
 
Hili jambo halikupangika vyema. Ndio maana hawawezi kuwa na majibu hayo ya kisheria.

Tuanza na makosa tu ktk hiyo nyaraka;
1. Ile power of attorney ya mh. Rais, inavyosomeka ni kwamba inampa Waziri Mbarawa kusaini kwa niaba ya Tz na Dubei. Sasa hilo wanajibuje? Kwamba ilikosewa?
2. Hiyo IGA, wahusika wote wa upande wa Dubei, hawaeleweki, majina, vyeo, kuna saini tu. Ni kina nani?
3. IGA ni kati nchi na nchi, Sisi Rais kaonekana kwenye nyaraka, Waziri, kaonekana, na kuna sehemu PS wa wizara kaonekana, wao yupo mkurugenzi wa bandari (DP WORLD), hii ni kampuni tu. Wa Dubei wako wapi?! Unajibuje hilo ..
4. Power of Attorney upande ule alopewe huyo Mkurugenzi wa bandari Dubei, kapewa na nani?! Ukiisoma unaona juu tu, stamp ya Government of Dubei. Ni nani katika serikali ya Dubai, kampa hiyo nguvu,? Cheo na majina na signature, havipo? Mbona sisi Mh Samia kaonekana. Unajibu hili?
5. Zile hoja za huyu mwekezaji kupewa Land Rights na sheria za ufidiaji kinyume na sheria zetu za Ardhi, unazijibuje?!
6. Alisema Prof. Shivji, wao DP World wamepewa haki zote za mkataba, sisi Tanzania tumechukua wajibu wote wa mkataba. Yeye haonekani ktk kipengele chochote akiwa na wajibu. Ni nini hiki?!
7. Wanasema wakienda usuluhishi huko S. Afrika , sheria inayotumika ni "Laws of England". Hii inakinzana na sheria zetu zote. Unajibuje hilo?!
8. Mchakato wa tender ulitangazwa kwa tangazo lipi? Waweke wazi,

Mambo ni mengi sana.

Hili jambo ni zito.
Wao hawajamuuka wakidhani Watanzania ni mbumbu, wewe umewanyoosha haswaa!!
 
Muda wa maswali na majibu umeisha
Mkataba ni mbovu period
Majibu yote yapo hadharini sasa ufafanuzi wa nini?
Bandari waiache hata kama inaingiza hasara so what ?
 
Pawa of instruments aliyopewa mbarawa jamaa ameruka ruka ww alipofika kumalizia akaparuka ,jamaa wakamwambia amesoma nunusu ,jamaa akagoma kumalizia pale ilipoandikwa ,wakamuomba akagoma kabisa
Hahaha, wapi kwenye kikao chake cha jana na wahariri au?
 
Sasa Shivji unamjibu nini?
Mtu kaongea openly kuwa serikali inafanya kusudi bandari ifeli ili ibinafsishwe...mtu kama huyu unamjibu nini?
Mtu kabaki Karne ya 20 ya kutaka serikali ifanye kilakitu..utamjibu nini??
Shivji siyo msahafu, epuka kuabudu binadamu mwenzako
 
Yaan Shivji anasema kipengele Fulani kinasema hv,,, kwa hiyo baadae kitaleta madhara haya. Hatimaye mtu anakuja badala ya kujibu hoja yake mtu anaishia kusema hata wahuni huzeeka. Mambo ya kishenzi sana, wajibu hoja plz
 
Back
Top Bottom