Wito Kwa Serikali na DPP: Kesi Ya Ugaidi Dhidi Ya Freeman Mbowe Na Wenzake Irushwe LIVE Kupitia Channel Maalum Ya Online TV

Wito Kwa Serikali na DPP: Kesi Ya Ugaidi Dhidi Ya Freeman Mbowe Na Wenzake Irushwe LIVE Kupitia Channel Maalum Ya Online TV

Hii issue ya kesi ya Freeman Mbowe tushaandika thread ya kuomba irushwe LIVE katika channel maalum, hata kabla kesi haijaanza.

Ila serikali ikaweka nta kwenye masikio yao, sasa hata raia wanazuiwa kuingia mahakamani kusikiliza na kama wakati mwingine kama jana walinyang'anywa sim zao.
 
Hii issue ya kesi ya Freeman Mbowe tushaandika thread ya kuomba irushwe LIVE katika channel maalum, hata kabla kesi haijaanza.


Huyu mwamba:

IMG_20210829_163746_049.jpg


si wakelele moja.

Hata Hamza angalikuwa kasema nao tu, kama wangekuwa wa kusikia.
 
Amesikika Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Magdalena Ntandu akielekeza utaratibu mpya kuhusiana na kufuatilia kesi inayomkabili Mh. Mbowe.

Kasema eneo la mahakama ni dogo kuwatosha wote ambao wangependa kuhudhuria. Suluhu ya hapa ilikuwa kutafuta namna wezeshi kwa wote ambao wangependa kuhudhuria na kufuatilia kesi hii.

Umuhimu wa kuonekana haki ikitendeka katika shauri lolote hakuwezi kudunishwa.

Kama mkoloni aliyaacha majengo ya mahakama wazi bila madirisha milango ya kufungwa, kwanini serikali ya rais mwanamke mtarajiwa wa 2025 leo ifungie wasikilizaji wa kesi ya mtuhumiwa wake nje na kwa matumizi ya nguvu?

Katazo la mtu kuwa na simu au hata kuwasiliana kwa maandishi au memo mahakamani ni kinyume sheria. Kwanini serikali ijipe jukumu la kuvunja sheria ndani au katika viunga vya mahakama kwa namna yoyote?

Kuna mawazo kuwa kuna mhimili mmoja unaendelea kuiingilia mingine na kushurutisha yake. Jambo hili si la afya hata kidogo. Mambo kama haya ndiyo yanayoleta udharura kwenye madai ya katiba mpya.

Ili kuonyesha haki inatendeka pia katika kesi hii, dhana ya mahakama kuwa ni sehemu ya wazi na iheshimiwe.

Kuliacha shauri hii kuendeshwa kwa uwazi likiwemo kurushwa kwenye Runinga ikibidi, kungejibu changamoto ya nafasi na pia kupunguza mkusanyiko usiokuwa wa lazima mahakamani hapo.

Ikumbukwe kuwa serikali ya haki ni mwakilishi wa wananchi wake. Ni jambo la aibu sana kama serikali ina nia yoyote ovu dhidi ya raia wake awaye yote.

Ni muhimu sana jitihada zote zikafanyika kuonyesha kwa vitendo kuwa haki inatendeka.

Itambulike kuwa hatutakaa kimya kwa uonevu dhidi yetu kama raia.
Kwani wewe na machadema wenzako mkitoa pesa kwa TV zirushe kuna tatizo? Unataka nani akulipie gharama Ili Wewe uone?
 
Amesikika Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Magdalena Ntandu akielekeza utaratibu mpya kuhusiana na kufuatilia kesi inayomkabili Mh. Mbowe.

Kasema eneo la mahakama ni dogo kuwatosha wote ambao wangependa kuhudhuria. Suluhu ya hapa ilikuwa kutafuta namna wezeshi kwa wote ambao wangependa kuhudhuria na kufuatilia kesi hii.

Umuhimu wa kuonekana haki ikitendeka katika shauri lolote hakuwezi kudunishwa.

Kama mkoloni aliyaacha majengo ya mahakama wazi bila madirisha milango ya kufungwa, kwanini serikali ya rais mwanamke mtarajiwa wa 2025 leo ifungie wasikilizaji wa kesi ya mtuhumiwa wake nje na kwa matumizi ya nguvu?

Katazo la mtu kuwa na simu au hata kuwasiliana kwa maandishi au memo mahakamani ni kinyume sheria. Kwanini serikali ijipe jukumu la kuvunja sheria ndani au katika viunga vya mahakama kwa namna yoyote?

Kuna mawazo kuwa kuna mhimili mmoja unaendelea kuiingilia mingine na kushurutisha yake. Jambo hili si la afya hata kidogo. Mambo kama haya ndiyo yanayoleta udharura kwenye madai ya katiba mpya.

Ili kuonyesha haki inatendeka pia katika kesi hii, dhana ya mahakama kuwa ni sehemu ya wazi na iheshimiwe.

Kuliacha shauri hii kuendeshwa kwa uwazi likiwemo kurushwa kwenye Runinga ikibidi, kungejibu changamoto ya nafasi na pia kupunguza mkusanyiko usiokuwa wa lazima mahakamani hapo.

Ikumbukwe kuwa serikali ya haki ni mwakilishi wa wananchi wake. Ni jambo la aibu sana kama serikali ina nia yoyote ovu dhidi ya raia wake awaye yote.

Ni muhimu sana jitihada zote zikafanyika kuonyesha kwa vitendo kuwa haki inatendeka.

Itambulike kuwa hatutakaa kimya kwa uonevu dhidi yetu kama raia.
Kweli ndoto hazina limits

Unaweza hata kuota uko mbinguni

Endelea kuota
 
Mtu Katoa pointi uchadema umetokea wapi tatizo njaa zenu zimefanya akili imeamia matakoni,,ndio mama Trump aliwaita shit hole
Wewe ukiyeshiba mbona kutwa kupiga miayo na kurushiwa risasi mpaka mnabaki kulialia mitandaoni kuchangisha watu.
 
Kwani wewe na machadema wenzako mkitoa pesa kwa TV zirushe kuna tatizo? Unataka nani akulipie gharama Ili Wewe uone?

Wapi kumeombwa mtu wa kulipia gharama? Hujui ambao wangependa kurusha hata kwa kuilipa serikali ni wengi tu.

Kumbe humjui anayezuwia hata kurusha SMS tu?

Hiiiiii bagosha!
 
Habari wana Jamii,

Nimekaa na kutafakari kuhusu kesi ya Ugaidi Ya Freeman Mbowe na Wenzake ambayo inakaribia kuanza mwezi ujao. Na ndio nikaamua kuanzisha hii thread maalum ya kuomba kesi hio irushwe "LIVE COVARAGE" kwa kutumia Channel Maalum (Za Bure) kama ilivyofanyika;

I) South Africa - Katika kesi ya Oscar Pistorious (Mkimbiaji Kilema - Mwana Olympic).

II) Kenya - Katika kesi ya kupinga Uchaguzi Mkuu uliopita.


Kwasababu kuu,

1) Ni Kesi yenye umuhimu na mvuto (attention) mkubwa kitaifa na kimataifa.

2) Kuepusha msongamano wa raia kwenda kuisikiliza Mahakamani kwasababu ya maambukizi ya Covid 19.

3) Raia wa Tanzania walio ndani na nje ya nchi wana haki ya kujua, kuona, kusikiliza mashtaka yalio dhidi ya kiongozi wao wa Chama Kikuu Cha Upinzani.

4) Vyombo visivyo vya Serikali (NGO's, Donners e.t.c) vina mvuto wa kujua na kufuatilia dhidi ya kuendeshwa kwa kesi hio kubwa.

5) Ni haki ya kisheria na katiba kwa kila mtu kujua au kufuatilia kesi mahakamani ambayo ana mahusiani nayo, au yenye maslahi nae.

6) Kuna raia wanaishi mbali na Dar Es Salaam na hawana uwezo wa kwenda kushuhudia kesi ya kiongozi wao.

7) Mahakama Ya Kisutu ni ndogo kuweza kutosheleza watu wote watakao kwenda kushuhudia kesi hio.

8) Dunia na Taifa kwa ujumla lijiridhishe kwamba watuhumiwa watatendewa haki.

Kwa unyenyekevu mkubwa ningependa kutoa vito (Tuweke Itikadi Za Vyama Pembeni) kwa;

A) Wana Familia Wenzangu Wa JamiiForums Na Wana Mitandao Ya Kijamii - Kupaza Sauti.

B) Wanasheria na Mawakili Wote - Kupeleka Maombi Mahakamani Ya Kutoa Kibali Cha Kuoneshwa LIVE COVERAGE.

C) Wanasiasa - Kupaza Sauti Serikali/DPP Ikubali Maombi Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.

D) Wana Habari - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.

E) NGO's (Human Rights Watch) - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.

#KesiYaUgaidiLIVE.


Zitto
Pascal Mayalla




Mfano wa Kesi Ya Uchaguzi Kenya.
View attachment 1878832

Mfano Wa Kesi Ya Oscar Pistorious Nchini South Africa.

View attachment 1878833
Naunga mkono hoja. Napendekeza NGO za wapigaji kama LHRC' WATETEZI walipie gharama za kurusha live
 
Back
Top Bottom