Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
Nyie ndo walinzi wa taifa hili. Sio CCM
Nafahamu mnaona kwa namna gani CCM wanalipeleka Taifa hili pabaya.
Nafahamu mnajua namna ya Viongozi wa CCM wanavyolifisadi hili Taifa kwa wizi wa kutisha na matumizi mabaya ya kodi za wananchi huku wakitaka watukuzwe at the expense ya kodi za wananchi.
Najua mnaona wanavyoiba fedha za wananchi kupitia tenda za miradi mbalimbali huku miradi yenyewe ikijengwa chini ya kiwango.
Najua mnaona wanavyoongeza gharama za miradi inayotumia fedha za wananchi ili waibe hela kwa faida zao na kugharamia wizi wa uchaguzi. Mfano overpricing ya viwanja vya michezo vinavyoendelea kujengwa huko Dodoma, Arusha na hapa Dar es Salaam.
Nafahamu mnajua namna taifa hili lilivyofikia kwenye hatari ya kuwa failed state kutokana na kikundi cha watu wachache hasa CCM kujimilisha Taifa hili. Wanateuana watu wasio na uwezo kwa sababu tu ya kujuana na uchawa.
Najua mnafahamu chaguzi za Taifa hili sio chaguzi kama chaguzi ila ni maigizo yanayofanyika ili kuwahadaa wananchi. Viongozi wanaopatikana kupitia chaguzi hizo sio Viongozi waliochaguliwa kweli na wananchi na uthibitisho ni Maneno ya makada na Viongozi wa CCM wenyewe. Rejeeni Hotuba ya Nape kuhusu wanavyoshinda uchaguzi alipokuwa Kagera na ile hotuba ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido walivyoelezea kuikweli namna CCM wanavyonajisi chaguzi za nchi hii kupitia Tume hii ya Uchaguzi ambayo ni vibaraka wa CCM.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Nafahamu mnaona namna uchawa unavyoliangamiza taifa na kodi za wananchi zinavyotumika kutengeneza watu wajinga wanaoitwa machawa kuwarubuni Watanzania.
Najua mnafahamu kuwa haya yote yanafanywa na CCM kwa sababu moja tu. Nchi hii ina Katiba mbovu inayowawezesha kufanikisha markings yote haya bila kufanywa chochote na wala kuhojiwa na yeyote.
Najua mnajua kuwa leo hii mkiamua kusimama na Wananchi, Taifa letu litafanikiwa kupata Katiba Bora ambayo itaweka mifumo imara na kuondoa uwekezano wa nchi yetu kufikia hapa tulipofikia kuelekea kuwa failed state.
Najua mnafahamu kuwa kiukweli CCM si chochote si lolote bila nyie. Na kiburi chao ni kwa sababu tu mmefumbia macho ujinga wao.
Ombi langu kwenu,
Sasa simameni na Wananchi. Msiruhusu CCM waibe uchaguzi, mairuhusu CCM waendeleze udhalimu wao maana udhalimu wao unaenda kuliangamiza hili taifa.
Nyie ndo walinzi wa hili Taifa na CCM wakikaa kando haitawaathili wala kuwapunguzia chochote ila italihakikishia hili Taifa uimara na mafanikio ya uhakika kwa wananchi wake kwa miaka mingi ijayo.
Nawaomba tena. Simameni na Wananchi na kataeni kutumiwa na CCM.
Nafahamu mnaona kwa namna gani CCM wanalipeleka Taifa hili pabaya.
Nafahamu mnajua namna ya Viongozi wa CCM wanavyolifisadi hili Taifa kwa wizi wa kutisha na matumizi mabaya ya kodi za wananchi huku wakitaka watukuzwe at the expense ya kodi za wananchi.
Najua mnaona wanavyoiba fedha za wananchi kupitia tenda za miradi mbalimbali huku miradi yenyewe ikijengwa chini ya kiwango.
Najua mnaona wanavyoongeza gharama za miradi inayotumia fedha za wananchi ili waibe hela kwa faida zao na kugharamia wizi wa uchaguzi. Mfano overpricing ya viwanja vya michezo vinavyoendelea kujengwa huko Dodoma, Arusha na hapa Dar es Salaam.
Nafahamu mnajua namna taifa hili lilivyofikia kwenye hatari ya kuwa failed state kutokana na kikundi cha watu wachache hasa CCM kujimilisha Taifa hili. Wanateuana watu wasio na uwezo kwa sababu tu ya kujuana na uchawa.
Najua mnafahamu chaguzi za Taifa hili sio chaguzi kama chaguzi ila ni maigizo yanayofanyika ili kuwahadaa wananchi. Viongozi wanaopatikana kupitia chaguzi hizo sio Viongozi waliochaguliwa kweli na wananchi na uthibitisho ni Maneno ya makada na Viongozi wa CCM wenyewe. Rejeeni Hotuba ya Nape kuhusu wanavyoshinda uchaguzi alipokuwa Kagera na ile hotuba ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Longido walivyoelezea kuikweli namna CCM wanavyonajisi chaguzi za nchi hii kupitia Tume hii ya Uchaguzi ambayo ni vibaraka wa CCM.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Nafahamu mnaona namna uchawa unavyoliangamiza taifa na kodi za wananchi zinavyotumika kutengeneza watu wajinga wanaoitwa machawa kuwarubuni Watanzania.
Najua mnafahamu kuwa haya yote yanafanywa na CCM kwa sababu moja tu. Nchi hii ina Katiba mbovu inayowawezesha kufanikisha markings yote haya bila kufanywa chochote na wala kuhojiwa na yeyote.
Najua mnajua kuwa leo hii mkiamua kusimama na Wananchi, Taifa letu litafanikiwa kupata Katiba Bora ambayo itaweka mifumo imara na kuondoa uwekezano wa nchi yetu kufikia hapa tulipofikia kuelekea kuwa failed state.
Najua mnafahamu kuwa kiukweli CCM si chochote si lolote bila nyie. Na kiburi chao ni kwa sababu tu mmefumbia macho ujinga wao.
Ombi langu kwenu,
Sasa simameni na Wananchi. Msiruhusu CCM waibe uchaguzi, mairuhusu CCM waendeleze udhalimu wao maana udhalimu wao unaenda kuliangamiza hili taifa.
Nyie ndo walinzi wa hili Taifa na CCM wakikaa kando haitawaathili wala kuwapunguzia chochote ila italihakikishia hili Taifa uimara na mafanikio ya uhakika kwa wananchi wake kwa miaka mingi ijayo.
Nawaomba tena. Simameni na Wananchi na kataeni kutumiwa na CCM.