Wito kwa watanzania wote: Ili CCM na serikali zake wajue hatuwataki, 2025 wote tususie uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi

Wito kwa watanzania wote: Ili CCM na serikali zake wajue hatuwataki, 2025 wote tususie uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi

Haya unayoyaeleza hapa ni kuwa Katiba Mpya, itatekelezwa kwa usahihi kabisa na vyombo vyote vilivyomo serikalini, hali ambayo tunajua siyo kweli chini ya CCM.

Sasa mimi ngoja nikupe pendekezo mbadala wa hayo unayoyahimiza wewe; hasa hilo la kususia uchaguzi.

1. Mimi nahimiza watu wengi sana wanaolitakia mema taifa hili wajitokeze kwa wingi sana wakati wa kupiga kura, na wapige kura za kuikataa CCM.

2. Badala ya kutegemea Katiba Mpya kulinda kura za wananchi zisiibiwe na CCM (kwa kufanya uhalifu), mimi nawahimiza wananchi hawa wakatae uhalifu na kuvurugiwa kura zao (kuzuia uhalifu). Kinachotakiwa sasa hivi, si kuwahimiza wananchi wasusie uchaguzi, bali ni kuweka mikakati sahihi ya kuzuia uhalifu huo. Wananchi waelimishwe, na wapewe njia sahihi za kukataa kura zao kuharibiwa.
Swala linalojitokeza hapa ni nani atakayefanya kazi ya kuwapanga wananchi,... wewe mkuu 'Mathanzua', na wengine wengi tuliochoshwa na hujuma za CCM, ni wajibu wetu kuwa sehemu ya kuzuia uovu unaofanywa na CCM, kwa kuelimishana. Vyama vya siasa na taasisi za kijamii, ni wajibu wao kusaidia katika kuwapanga wananchi watimize wajibu wao

3. Hiyo namba tatu uliyoweka hapo, sioni maana yake hata ndogo katika kuzuia yanayofanywa na CCM.
Hali ni mbovu kiasi kwamba kuna watu wanajiita kwa sifa kubwa kuwa wao ni "CHAWA"? Haya hayajawahi kutokea hata siku moja katika historia ya nchi hii.
Wewe ni wazi ni li CCM.Naomba nirudie,huwezi kufanya jambo hilo hilo kwa njia hiyo halafu utegemee matokeo tofauti,it is stupid.What you have suggested ndiyo tuliyofanya miaka yote,kwa hiyo matokeo yatakuwa Yale Yale.Wizi wa kura na kutoweza kuhoji matokeo mahakamani.Afterall mahakama ni za CCM na huwezi kuhoji matokeo mpaka yatangazwe.Hizo zote ni njia za kujihakishia ushindi.

Ya tatu nimeitaja kwa kuwa wananchi wa 2025 sio wa 2015.Wananchi wa 2025 wanaifahamu vizuri CCM, kwamba ni Chama kiovu hell bent kulinda maslahi ya watu wachache na kuendeleza kuwakandamiza by any means possible.For me enough is enough,CCM must go.
 
Ngumu sana hiyo.
Wala sio ngumu,this is the easiest method,kuwanyima haki ya kututawala kwa kutowapigia kura.Kuna ugumu gani wewe kubaki nyumbani kwako na wanao siku ya uchaguzi.Watanzania lazima tuamke,let us do something for our freedom.Miaka 63 ya Uhuru literally nothing in terms of development,ni usanii,ngonjera na sarakasi tu ,no haikubaliki.
 
Ni miaka 63 sasa CCM ipo madarakani. Kimsingi hakuna maendeleo ya maana waliyotuletea, isipokuwa kuturudisha nyuma kimaendeleo miongo kadhaa.

Kila serikali iliyoingia madarakani ilileta usanii wa kisiasa na kiuchumi na hatimaye kuturudisha nyuma decades.Wanayojisifia kwamba ni maendeleo si lolote kabisa ukilinganisha na rasilimali nyingi tulizo nazo. Tuamke Watanzania.

Comrade Magufuli katika awamu yake moja alijitahitahidi kubadilisha taswira ya Tanzania kwa kutuletea maendeleo kiasi fulani, lakini juhudi zake zilifishwa prematurely, inasikitisha sana.

Kwa jinsi hali ya kisiasa ilivyo nchini mwetu, hatuna jinsi yeyote ambayo kama Watanzania tunaweza kujinasua kwenye mkwamo wa kimaendeleo na kisiasa tulio nao sasa.Katiba haiheshimiwi kabisa na sioni uwezekano wa Bunge au hata wana siasa kutusaidia.

Mwito wangu kama Mtanzania ni huu, kama mpaka 2025 tusipokuwa na Katiba mpya, wala Tume Huru ya Uchaguzi, siku ya uchaguzi wote tubaki nyumbani.Sisi wananchi ndio tunaowapa wanasiasa legitimacy ya kutawala, kama wasipotupa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi tubaki nyumbani,simply tuwanyime legitimacy ya kututawala.It is now or never, tushirikiane wote.
Watu mnaacha kuhangaika na wahusika kufanya miradi ya wananchi kwa 100% zenye faida, badala yake mnahangaika na chama na katiba, chama hata kije Cha namna gani lakini kama ni cha waTanzania hawa hawa hakuna lolote la tofauti mtaona, tena bado mtarejea kuwakumbuka tu hao CCM, katiba mnaongelea katiba , hulka ya mTanzania inabadilishwa na katiba? Kweni hata katiba iliyopo inafuatwa?

Acheni usanii wa kuwahadaa watu ili mpenye kwenye viuchaguzi muende kupiga hela, ninyi ndo wale wale tu tena ndo wabaya kuliko
 
Watu mnaacha kuhangaika na wahusika kufanya miradi ya wananchi kwa 100% zenye faida, badala yake mnahangaika na chama na katiba, chama hata kije Cha namna gani lakini kama ni cha waTanzania hawa hawa hakuna lolote la tofauti mtaona, tena bado mtarejea kuwakumbuka tu hao CCM, katiba mnaongelea katiba , hulka ya mTanzania inabadilishwa na katiba? Kweni hata katiba iliyopo inafuatwa?

Acheni usanii wa kuwahadaa watu ili mpenye kwenye viuchaguzi muende kupiga hela, ninyi ndo wale wale tu tena ndo wabaya kuliko
Obviously wewe ni li-CCM ndio maana unaipenda Status Quo iendelee.Lakini unataka CCM iendelee madarakani mpaka lini na uovu wote huu.We want change kwa kuwa tunataka cake ya Taifa kila mtu apate,sio watu wachache by ndugunization and urafikinization kama ilivyo sasa and that is possible.Na kama it is possible,why don't we aspire for that,which is obviously a better alternative?

Mkuu niseme hivi,ni ujinga kung'ang'ania an inferior alternative kama kuna a better alternative,it is infact dumb.
 
Sisi bado tunaitaka CCM wewe kama hutaki hama nchi
Kwani CCM ndio wenye
hati miliki ya Tanzania?!This is frankly a very dumb and stupid comment,no wonder CCM ipo kama ilivyo.So mnataka kuwatawala Watanzania kwa nguvu,which of course you are doing already.Hapana haikubaliki,you people have to go.

Yaani mmewarudisha nyuma Watanzania kiasi hiki bado mnang'ang'ania tu.Ufisadi Moto, Ndugunization na Urafikinization(Mwitongo)imejaa;Elimu mmeharibu;Afya mmeharibu,watu kila sehemu ni wagonjwa;Kilimo mmeharibu;Uchumi mmeharibu;Mikataba mibovu kila kukiucha(the most recent DP World);Umeme shida;Maji shida,watu wanatumia maji ya madimbwi ya kunyweshea Ng'ombe,miaka sitini na tatu baada ya Uhuru,simply everything is in disarray.Hapana ondokeni inatosha,hatuwataki tena,achieni wengine,you have miserably failed Tanzanians.
 
Ni miaka 63 sasa CCM ipo madarakani. Kimsingi hakuna maendeleo ya maana waliyotuletea, isipokuwa kuturudisha nyuma kimaendeleo miongo kadhaa.

Kila serikali iliyoingia madarakani ilileta usanii wa kisiasa na kiuchumi na hatimaye kuturudisha nyuma decades.Wanayojisifia kwamba ni maendeleo si lolote kabisa ukilinganisha na rasilimali nyingi tulizo nazo. Tuamke Watanzania.

Comrade Magufuli katika awamu yake moja alijitahitahidi kubadilisha taswira ya Tanzania kwa kutuletea maendeleo kiasi fulani, lakini juhudi zake na kiuhalisia na za kwetu pia,zilifishwa prematurely, inasikitisha sana.

Kwa jinsi hali ya kisiasa ilivyo nchini mwetu, hatuna jinsi yeyote ambayo kama Watanzania tunaweza kujinasua kwenye mkwamo wa kimaendeleo na kisiasa tulio nao sasa.Katiba haiheshimiwi kabisa na sioni uwezekano wa Bunge au hata wana siasa kutusaidia.

Mwito wangu kama Mtanzania kwa Watanzania wenzangu ni huu, kama mpaka 2025 tusipokuwa na Katiba mpya, wala Tume Huru ya Uchaguzi, siku ya uchaguzi wote tubaki nyumbani tusiende kupiga kura.Naamini hii ndiyo lugha tu CCM watakayoelewa.Sisi wananchi ndio tunaowapa wanasiasa legitimacy ya kutawala.Sasa kama wasipotupa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi tubaki nyumbani,simply tuwanyime legitimacy ya kututawala.It is now or never, naomba tushirikiane wote.

NB😛lease share this message widely.
CCM Wana vyama mchongo vingi tu, ukisusia vile mchongo vitashiriki na bado uchaguzi utaonekana ni wa vyama vingi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Me huwa siwaelewagi mnaolilia tume huru ya uchaguz et sijui katiba mpya, hivi unahisi hayo yatabadilisha nini ikiwa watu ni wale wale?

Hiyo tume huru ya uchaguzi watashindwa nini kuihonga hela ili watoe matokeo wanayoyataka?

Jirani zetu Kenya hapo uchaguzi wao uliopita ulisimamiwa na tume huru, je wamepata walichotegemea?

Sijui katiba mpya, je yaliyopo kwenye katiba ya sasa yanasimamiwa?

Ishu ni viongozi hawana uchungu na watanzania na ni wabinafsi na issue sio katiba mpya wala tume huru

Sent using Jamii Forums mobile app
Na kina Mandela, Nyerere, Kenyatta, n.k. wangekuwa na mawazo kama yako, tusingejikomboa.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Zipo njia nyingine nyingi za kupinga sera za CCM, ila kususia upigaji kura sio njia sahihi, respectfuly.
 
Me huwa siwaelewagi mnaolilia tume huru ya uchaguz et sijui katiba mpya, hivi unahisi hayo yatabadilisha nini ikiwa watu ni wale wale?

Hiyo tume huru ya uchaguzi watashindwa nini kuihonga hela ili watoe matokeo wanayoyataka?

Jirani zetu Kenya hapo uchaguzi wao uliopita ulisimamiwa na tume huru, je wamepata walichotegemea?

Sijui katiba mpya, je yaliyopo kwenye katiba ya sasa yanasimamiwa?

Ishu ni viongozi hawana uchungu na watanzania na ni wabinafsi na issue sio katiba mpya wala tume huru

Sent using Jamii Forums mobile app
Ina maana sisi hatuwezi kua na jambo letu wenyewe zuri ambalo wengine wataliiga hadi tujikosoe kutipia kenya.kwahiyo kama kenya alikosea na sisi tukosee?.Unasema viongozi hawana uchungu alafu unaona katiba bora sio suluhisho,je hao wenye uchungu watazaliwa lini ili waje waongoze?.Viongozi wanatakiwa waongozwe na matakwa yaliyowekwa na wananchi kupitia sheria na katiba.Sio utashi wao.Tukiishi kwa style hiyo nchi haiwezi kwenda mbele.
 
Mtaishia kugongwa virungu na police muishie kuwa walemavu halafu mje na kauli ya Mungu atatulipia.

Ukishajitambua kwenye maisha pigania maendeleo ya familia yako hayo mengine unayoona hayawezekani yaache yakupite tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Siasa iko kila mahali,hayo maendeleo utayafanyaje kama mambo ya msingi yakufanywa na serikali hayafanywi kwa usahihi.Ata hivyo sio watu wote wana kiu ya mabadiliko kwahiyo inawezekana wewe ni kundi ilo ndo maana unaogopa virungu.
 
Me huwa siwaelewagi mnaolilia tume huru ya uchaguz et sijui katiba mpya, hivi unahisi hayo yatabadilisha nini ikiwa watu ni wale wale?

Hiyo tume huru ya uchaguzi watashindwa nini kuihonga hela ili watoe matokeo wanayoyataka?

Jirani zetu Kenya hapo uchaguzi wao uliopita ulisimamiwa na tume huru, je wamepata walichotegemea?

Sijui katiba mpya, je yaliyopo kwenye katiba ya sasa yanasimamiwa?

Ishu ni viongozi hawana uchungu na watanzania na ni wabinafsi na issue sio katiba mpya wala tume huru

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna kitakachobadiika kama ulivosema watu ni wale wale
 
Watu mnaacha kuhangaika na wahusika kufanya miradi ya wananchi kwa 100% zenye faida, badala yake mnahangaika na chama na katiba, chama hata kije Cha namna gani lakini kama ni cha waTanzania hawa hawa hakuna lolote la tofauti mtaona, tena bado mtarejea kuwakumbuka tu hao CCM, katiba mnaongelea katiba , hulka ya mTanzania inabadilishwa na katiba? Kweni hata katiba iliyopo inafuatwa?

Acheni usanii wa kuwahadaa watu ili mpenye kwenye viuchaguzi muende kupiga hela, ninyi ndo wale wale tu tena ndo wabaya kuliko
Kwa hiyo kwa akili zako unaona ni sawa tuendelee kua na katiba isiyofuatwa miaka nenda rudi.Kama wewe huna akili zakutaka nchi iwe na mambo mazuri waachie wenye hizo akili wafanye.
 
CCM Wana vyama mchongo vingi tu, ukisusia vile mchongo vitashiriki na bado uchaguzi utaonekana ni wa vyama vingi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mkuu hili jambo ni kata fitina.Ni hivii,yeyote atakayeshiriki Uchaguzi 2025 bila kuwepo Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba Mpya, tunajua si mwenzetu.It is as simple as that.
 
Mh ndugu yangu ccm unawajua vizuri? Tukifanya hivyo watafanya sherehe kubwa kwa kupita bila kupingwa

Na watatupongeza wanainchi kwa kuwa wazarendo kwa ccm😅😅😅
 
Hakuna kitakachobadiika kama ulivosema watu ni wale wale
Watu wote tukiwa na mawazo yakusema hakuna kitakachobadilika ata haya maendeleo ya dunia na teknolojia yaliyopo sasa duniani yasingekuwepo.Mabadiliko hayaji tu from no where.Lazima kuwe na watu wanaofikiri tofauti badala ya kuridhika.
 
Mh ndugu yangu ccm unawajua vizuri? Tukifanya hivyo watafanya sherehe kubwa kwa kupita bila kupingwa

Na watatupongeza wanainchi kwa kuwa wazarendo kwa ccm[emoji28][emoji28][emoji28]
Lazima washerehekee kwasababu ela zakuwahonga viongozi wa mitaa na vijiji zitakua chache.
 
Back
Top Bottom