Wivu!!

Wivu, wivu wivu aaah, Gari nzuri kuliko ya Boss wako, inakuwa ishu....... asante Lizzy.
 
Wivu, wivu wivu aaah, Gari nzuri kuliko ya Boss wako, inakuwa ishu....... asante Lizzy.

Hehehe!Elia sasa bosi akikuonea wivu hapo kuna hatari maana anaweza hata kukufukuza kazi akiweza!Au mwalimu kwa mwanafunzi...ni mwendo wa kufelishana tu kwenye shule zetu hizi!
 

Babu heshima kwako
Ulipata divisheni ngapi?
 
Sasa kati ya Lizzy na CPU nani mwenye wivu kumpita mwenzake??
 
Reactions: CPU
Kwenye mapenzi: Wivu kati ya wawili ndani ya mahusiano unaweza kua kirutubisho au chachu ya mapenzi.Ukionyesha kwa kiasi utamfanya mwenzi wako ahisi kwamba unampenda na kumjali...sisemi kwamba ni kitu pekee kinachofanya hivyo bali ni kichocheo kizuri iwapo hakitazidishwa na kusababisha kero.Wivu unapozidi unaonyesha mapungufu yako kanakwamba hujiamini kitu ambacho kinaweza kupelekea mwenzako nae ahisi kwamba HUMUAMINI.

Dear Lizzy, kwa kadiri nilivyoifahamu hii mada, kuna wivu wa aina mbili - wivu mzuri na wivu mbaya. Wivu mzuri ni ule unaokusukuma kufikia hatua aliyofikia mwenzako, mbaya ni ule wa husuda na chuki ambao matokeo yake mwenye wivu huwacha kujiendeleza na kubakia kuumia roho, kupika fitina na kumwaga majungu.

Lakini bado siuelewi huu wivu wa mapenzi/kwa mpenzi wako. Ni nini hasa? Kuuliza uliza "umeenda wapi?", "kwa nini umechelewa kurudi?", ulikuwa unazungumza na nani?", kutaka kujua ameenda wapi na nani", "kupekua mikoba na mifuko ya suruali", "kusoma sms na msgs kwnye simu na internet", "Sitaki uzungumze, uwe na urafiki na fulani" n.k. Ikiwa ni moja, baadhi au yote katika haya hatuoni kuwa ni kero? Ni aina gani ya matendo ya wivu "mzuri" baina ya wapenzi ambayo yatazidisha mapenzi badala ya kuwa kero?
 
Sasa kati ya Lizzy na CPU nani mwenye wivu kumpita mwenzake??

Mi mbona nishamuova teki zamaaaaani.
Imagine hata akisalimiana na mama ake kwa kukumbatiana namfokea
 
MammaMia vyote ulivyotaja hapo ndio kero zenyewe.Mambo yakulindana kama wafungwa sio kabisa.Wivu mzuri ni ule unaokuwezesha kumwambia mwenzako au hata kufikiri tu kwamba siku akikusaliti utaumia na sio kumpekua pekua..wivu unaokufanya ujitahidi kumtendea mema ili asije akawa impressed na mtu mwingine kwa mambo ambayo unapenda atake/afurahie kutoka kwako tu..wivu unaokufanya utamani kua bora kuliko wote kwake.Wivu mzuri ni ule unaokusukuma kufanya mambo yatakayo mfanya asitake kukuacha!
 
Mi mbona nishamuova teki zamaaaaani.
Imagine hata akisalimiana na mama ake kwa kukumbatiana namfokea
Hehehehe...hubby anataka mikono ya wifey imhusu yeye tu na kifua chake kimguse yeye tu.Ndo maana na kupenda..na wivu wako unaniongezea raha!
 
Dah, Wivu sio mzuri!!!
Lakini mi nina wivu sijui!!!
Hebu ngoja nijikague aisee!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…