Wizara ya Afya Tanzania
Official Account
- Oct 1, 2020
- 58
- 127
- Thread starter
-
- #21
Asante kwa kuwasiliana nasi.Kupima Corona shs ngapi kwa sasa?
Nahitaji kujua utaratibu wa kupima DNA uko vipi na gharama zake na huduma inapatikana mikoa youte yani hospitali zote za wilaya ? Maana nina utata juu ya mtoto aliepatikana kwa mwenza wangu
Asante kwa majibu mujarab sasa pale Mabibo ni wapi hasa wanapima na siku na muda wa kazi tafadhaliAsante kwa kuwasiliana nasi.
Kupima Maambukizi ya Ugonjwa wa Homa ya Mapafu (Covid-19) kwa Raia wa Tanzania ni Shilingi 40,000, raia wa kigeni ni USD 50$
Mimi niwapongeze sana wizara ya afya kwa mageuzi makubwa ya sekta ya afya nchini
1.Kumekua na madaktari bingwa wa kutosha pamoja na vitendea kazi vifaa tiba katika hospitali zetu za mikoa na rufaa
2.Kumekua na uboreshwaji mkubwa wa huduma kwa wagonjwa ( Customer care) siku hizi matusi, kupuuzwa na dharau kwa wagonjwa vimepungua sana kama sio kwisha kabisa
3.Kumekua na ongezeko la watendaji, maboresho ya hospitali, kujengwa kwa hospitali mpya na vituo vya afya kwenye kata zetu na vijiji, hata wale waliokua hawajui hospitali siku hizi wanazijua na wanapata huduma
4.Kumekua na uboreshwaji wa bima ya afya ya taifa. Siku hizi watu wa NHIF hatudharauliki kama awali. Nimeshuhudia mke wa ndugu yangu ambae mumewe ni mwalimu na yeye mama wa nyumbani akifanyiwa upasuaji wa moyo kwa kutumia NHIF bila kikwazo na kupona. Hongera sana MNH
5.Niseme pia kumekua na huduma bora zaidi hospitali za serikali na hospitali na mashirika ya kijamii/dini kuliko hospitali binafsi. Kwakuwa nyie ndio wasimamizi mtusaidie wananchi kujua tatizo ni nini. Kuna hospitali ambazo ukifika mjamzito kujifungua wanakushawishi kufanya upasuaji sijui hili limekaaje kiafya
Ushauri
1.Matibabu ni gharama sana na watanzania wengi hawana uwezo wa matibabu. Tunaomba nyie na NHIF muandae mpango mzuri na rahisi wa kila mtanzania kuchangia bima ya afya. Kama ilivyo Ile 50,400 kwa watoto basi angalieni watu wazima na familia wanaweza lipia kiasi gani kwa kila mwaka.
NHIF wakiweza kuweka njia rahisi na nafuu na kutengeneza mfumo ambao wananchi wengi watakua wanachangia itakua rahisi pia wananchi wachache wanaougua kutibiwa, kuliko sasa wanavyochangisha wananchi wachache na pesa nayo inakua chache kuwatibia wananchi wachache wanaougua
2.Kingine basi niwaombe mshirikiane na wizara ya elimu kuweka somo litakaloweza kubeba maadili na desturi za mtanzania na maisha yake. Vijana wetu siku hizi hawana jando na unyago, wazazi wote wawili wamekua watu wa majukumu mengi huku watoto wakiachwa wanajifunza toka kwenye t.v. na wasaidizi wa nyumbani. Ukitengenezwa mtaala mzuri wa kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha nne nina uhakika vijana wetu wanaweza kuwa taifa bora sana baadae. Tutaepuka hata watoto kuendelea kuharibiwa kwa kurubuniwa kwani wengi wanakua hawajui na wanafanyiwa mambo mabaya wakiwa wachanga sana hadi inapojulikana inakua basi tena
3.Wizara ya afya na elimu angalieni hizi boarding za watoto wadogo jamani na mkiweza mzifungie kabisa au pale penye ulazima kibali kitoke kwenu. Hainingii akilini mtoto wa miaka 2, 3, 4, 5, hadi 10 kuwa shule ya bweni. Malezi na matunzo ya awali toka kwa wazazi ni muhimu sana kwa mtoto. Wamama na wababa kwanini tunazaa halafu hatutaki kulea? Kweli baba na mama wanampeleka mtoto mdogo bweni, mtoto ambae hata kujifunika shuka usiku au kupiga mswaki hawezi!! Halafu wanakaa nyumbani, wanakula kwa amani kabisa na kulala?? Kuna visa vingi nimekutana navyo vya kuumiza sana toka kwa hawa watoto
Cc Wizara ya Afya Tanzania
Nimekusoma ndugu mtaalam na mchambuzi mbobevu wa mambo ya kiafya, Wizara wanatakiwa kuhakikisha kunakuwepo na uhakika wa vipimo mhimu katika hospital zao maana ni aibu kubwa unakuta kila kipimo mhimu kutopatikana kwa mda wote kwa sababu ya mashine kuwa mbovu ama kutokuwepo kabisa vipimo hitajika kwa hospital ya ngazi husika ama wafuatilie kwa ukaribu zaidi uendeshaji wa hospital zao ili kupunguza vikwazo kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma kwao,. Jamii kubwa inategemea sana hizi hospital kwa sababu ya kipato duni lakini hugeuka kuwa kero kwao kuliko suluhisho kwa shida zao hivo kutafuta njia mbadala ambazo huwa si rafiki kwa afya zao...Nakazia tena inatia aibu sana kukosekana kwa basic laboratory investigations kwa hospital ngazi ya rufaa mkoa, wizara inafanya kazi kubwa na nzuri usiku na mchana kujaribu kupanua na kuongeza juhudi ya kutoa huduma bora kwa wananchi lakini iwapunguzie mzigo kwa kuongeza vipimo na wataalam wa kada husika ili kuleta ustawi bora wa afya
Hivi Tanzania kuna Corona ?Ndugu wana JamiiForums,
Tunashukuru kwa maoni yenu na Ushauri mnaotupa kila siku. Kupitia thread hii, tutapokea maoni, Ushauri, na malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.
Unaweza kututumia pia Private Message(PM) na utajibiwa kwa haraka sana.
Fuatilia ukurusa rasmi wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazeena Watoto (Idara Kuu Afya) wa Jamii Forums (Wizara ya Afya Tanzania) kupatea habari mbalimbali kuhusu Sekta ya Afya Nchini Tanzania.
Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:
Instagram @wizara_afyatz
Twitter @wizara_afyatz
Facebook “Ministry of Health, Gender, Elderly & Children”
Website www.moh.go.tz
Official Blog www.afyablog.moh.go.tz
Anuani
S.L.P 743 Dodoma
Tanzania
#TunaboreshaSektayaAfyaView attachment 1588107
Asante kwa kaz yenu nzuri. Swali langu ni kuwa, mgonjwa anapoambiwa alete damu(watu wa kuchangia damu) damu anayoongezewa mgonjwa inakuwa ni ile iliyoletwa na watu wa mgonjwa?Ndugu wana JamiiForums,
Tunashukuru kwa maoni yenu na Ushauri mnaotupa kila siku. Kupitia thread hii, tutapokea maoni, Ushauri, na malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.
Unaweza kututumia pia Private Message(PM) na utajibiwa kwa haraka sana.
Fuatilia ukurusa rasmi wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazeena Watoto (Idara Kuu Afya) wa Jamii Forums (Wizara ya Afya Tanzania) kupatea habari mbalimbali kuhusu Sekta ya Afya Nchini Tanzania.
Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:
Instagram @wizara_afyatz
Twitter @wizara_afyatz
Facebook “Ministry of Health, Gender, Elderly & Children”
Website www.moh.go.tz
Official Blog www.afyablog.moh.go.tz
Anuani
S.L.P 743 Dodoma
Tanzania
#TunaboreshaSektayaAfyaView attachment 1588107
Nina wasiwasi na Uzi huu.Mbona wizara ya afya hamjibu comment za wananch humu tofauti na Tanesco watu wanatoa malalamiko mko kimya