Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

1722519671620.png


Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

1722519723201.png


Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

1722519791453.png


Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
 
Sio kupitia wizara ya elimu tu,yaani bora hata ipitie wizara ya elimu,kuna zile zinapitia utumishi!

Halafu pale sasa utumishi wana HR wajinga wajinga,wanajifanya wajuaji huku kichwani hawana lolote.

Wanatoa vigezo kibao tena vya kujirudia,ukiwapigia simu ni kiburi tu hawapokei.

Binafsi,ofisi ya Rais wale HR wote wakiongozwa na wale dadaz hawana akili sawasawa kichwani,wana usumbufu sana kwenye hizo scholarship.
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.
halafu utasikia watz wakarimu sana.
ukarimu wa kinafiki. watz ni wana roho mbaya kama oil chafu. ukarimu wa kinafikifiki ukimzidi lazima akuchukie.
"Wherever you see Black people you see problems. Black itself alone is a problem."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.​
Mbona hao mabinti wote kwenye picha wanafanana na Rita Mlaki
 
Sio kupitia wizara ya elimu tu,yaani bora hata ipitie wizara ya elimu,kuna zile zinapitia utumishi!

Halafu pale sasa utumishi wana HR wajinga wajinga,wanajifanya wajuaji huku kichwani hawana lolote.

Wanatoa vigezo kibao tena vya kujirudia,ukiwapigia simu ni kiburi tu hawapokei.

Binafsi,ofisi ya Rais wale HR wote wakiongozwa na wale dadaz hawana akili sawasawa kichwani,wana usumbufu sana kwenye hizo scholarship.
Kila sehemu kunanuka nepotism za kijinga tu
 
Je unaongelea ubalozi WA Swetizerland ua New Zealand? Maana New Zealand hawana ubalozi hapa?
Nimeuzungumzia New Zealand pamoja na Uswisi kama Case study tu ila balozi nyingi hapa bongo mambo ni ya kihuni. High Commission for the United Republic of Tanzania tunatumia ubalozi wa Afrika ya Kusini tukiwa pamoja na Angola, Botswana, Eswatini, Lesotho, Malawi, Mauritius, Mozambique, Namibia, Zambia, pamoja na Zimbabwe.
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

View attachment 3058653

Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

View attachment 3058654

Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

View attachment 3058655

Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
Kuna dada mmoja alipata scholarship ya kusoma Japan kutoka Zanzibar. Anasema watu wa serikali walikuwa wanapata scholarships lakini hawazitangazi, wakitaka kuwapa ndugu zao, ambao hata hawana vigezo.

Alisema alipofika ubalozi wa Japan aligundua kuwa ubalozi unasubiri sana watu wanaotaka scholarship waje ubalozini, lakini unaona watu hawaji, kwa sababu serikali ilikuwa haitangazi scholarships mpaka siku za mwisho.

Ni ujinga mkubwa sana.
 
Kuna dada mmoja alipata scholarship ya kusoma Japan kutoka Zanzibar. Anasema watu wa serikali walikuwa wanapata scholarships lakini hawazitangazi, wakitaka kuwapa ndugu zao, ambao hata hawana vigezo.

Alisema alipofika ubalozi wa Japan aligundua kuwa ubalozi unasubiri sana watu wanaotaka scholarship waje ubalozini, lakini unaona watu hawaji, kwa sababu serikali ilikuwa haitangazi scholarships mpaka siku za mwisho.

Ni ujinga mkubwa sana.
Nikupe CODE moja! Ukienda ubalozini kuuliza hizi mambo usiongee na Mtanzania kabsa, tengeneza sentensi zako tamu za Kiingereza nenda kazungumze na wahusika sio wale wadada wa mapokezi! Nina rafiki yangu amesoma lugha ya Kirusi na ana cheti cha level B1 😀 Alikwenda Russian Culture House, wabongo wakamkimbia maana alikuwa anafahamu lugha vyema! Sasa hivi yupo zake Saint Petersburg State University mwaka wa pili anapiga Masters. Wabongo ni matatizo kabsa.
 
Sio kupitia wizara ya elimu tu,yaani bora hata ipitie wizara ya elimu,kuna zile zinapitia utumishi!

Halafu pale sasa utumishi wana HR wajinga wajinga,wanajifanya wajuaji huku kichwani hawana lolote.

Wanatoa vigezo kibao tena vya kujirudia,ukiwapigia simu ni kiburi tu hawapokei.

Binafsi,ofisi ya Rais wale HR wote wakiongozwa na wale dadaz hawana akili sawasawa kichwani,wana usumbufu sana kwenye hizo scholarship.
Wale madada wamfika pale sbb yakutoa mapenzi ndo maana wamekunywamadawa yakuongeza mikia
 
Back
Top Bottom