Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Safi sana Mkuu! Nimezungumzia kuwa ukienda kwenye ofisi za mabalozi na ukakutana na wale watu wa mapokezi watakuambia kuwa uende Wizarani huko ndipo kuna maelekezo yote! Sasa nikasema ni vyema mtu akakutana na wahusika wa uongozi sio mapokezi au wabongo! Sidhani kama kuna sehemu nimesema kwamba kufahamu lugha kutasaidia moja kwa moja!
Ukikutana na wahusika, ukikutana na mapokezi, huwezi kuepuka kuanzia wizarani ambako kuna vigezo vimeongezwa na lugha yako haitakusaidia kuvipita hivyo vigezo.

Kwa mfano, wewe si mfanyakazi wa serikali. Warusi hawana kigezo cha wewe kuwa mfanyakazi wa serikali ili kupata scholarship.

Ukienda kuongea na Mrusi Kirusi wakati Wizara imeweka kigezo cha wewe kuwa mfanyakazi wa serikali, kujua kwako Kirusi kutakupitishaje kwenye hicho kigezo cha kuwa mfanyakazi wa serikali?
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

View attachment 3058653

Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

View attachment 3058654

Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

View attachment 3058655

Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
Natamani Watanzania wapate fursa ya kusoma nje. Kuna mambo mengi ya kujifunza. Pamoja na kutoka familia maskini nilipata fursa ya kusoma nje (Uingereza na sehemu fulani Ufaransa) na wakati wa likizo nilikwenda Ireland na likizo nyingine Poland na nilijifunza mambo mengi ambayo yamenisaidia kuwa kama nilivyo leo. Nilisoma kwenye chuo ambacho tulikuwa wanafunzi kutoka mataifa 27 duniani na kila mwaka chuo kili'organise' cultural day - siku ambayo kila taifa/continenti walionyesha utamaduni wao. It was very interesting. Kwa kifupi, kusoma nje ni eye-opener.
 
Ukikutana na wahusika, ukikutana na mapokezi, huwezi kuepuka kuanzia wizarani ambako kuna vigezo vimeongezwa na lugha yako haitakusaidia kuvipita hivyo vigezo.

Kwa mfano, wewe si mfanyakazi wa serikali. Warusi hawana kigezo cha wewe kuwa mfanyakazi wa serikali ili kupata scholarship.

Ukienda kuongea na Mrusi Kirusi wakati Wizara imeweka kigezo cha wewe kuwa mfanyakazi wa serikali, kujua kwako Kirusi kutakupitishaje kwenye hicho kigezo cha kuwa mfanyakazi wa serikali?
Nielewe Mkuu nimetumia Urusi kama case study ila sidhani kama ukienda kukutana na Watu wa ubalozi moja kwa moja ukazungumza nao lugha yao watakuacha! Kumbuka kuwa ukienda nchi ambazo lugha ya vyuo vyao sio kiingereza ni lazma usome lugha yako kwanza ndo uendelee na masomo. Sasa wewe ndo unayechagua nani aende na nani asiende, kuna mmoja ana cheti cha level B1 cha lugha na mwingine hana, utamchagua nani?1​
 
Natamani Watanzania wapate fursa ya kusoma nje. Kuna mambo mengi ya kujifunza. Pamoja na kutoka familia maskini nikipata fursa ya kusoma nje (Uingereza na sehemu fulani Ufaransa) na wakati wa likizo nilikwenda Ireland na likizo nyinge Poland na nilijifunza mambo mengi ambayo yamenisaidia kuwa kama nilivyo leo. Nilisoma kwenye chuo ambacho tulikuwa wanafunzi kutoka mataifa 27 duniani na kila mwaka chuo kili'organise' cultural day - siku ambayo kila taifa/continenti walionyesha utamaduni wao. It was very interesting. Kwa kifupi, kusoma nje ni eye-opener.
Ila sio kila mtu anataka kila mtu aende kuosha macho nje
 
Nielewe Mkuu nimetumia Urusi kama case study ila sidhani kama ukienda kukutana na Watu wa ubalozi moja kwa moja ukazungumza nao lugha yao watakuacha! Kumbuka kuwa ukienda nchi ambazo lugha ya vyuo vyao sio kiingereza ni lazma usome lugha yako kwanza ndo uendelee na masomo. Sasa wewe ndo unayechagua nani aende na nani asiende, kuna mmoja ana cheti cha level B1 cha lugha na mwingine hana, utamchagua nani?1​
Hujaelewa au unapuuza point ya msingi.

Unazungumzia kwamba ukijua Kirusi ubalozi hautakuacha.

Wakati mchakato wa scholarship umehodhiwa na serikali wizarani.

Serikali wizarani imeweka vigezo vya figisu kibao. Mfano kigezo cha mtu kuwa mfanyakazi wa serikali.

Sasa, kwa mfano wewe si mfanyakazi wa serikali, kirusi unakijua. Utapenya vipi hapa wizarani ambapo kuna kigezo cha kuwa mfanyakazi wa serikali, ili uweze kufika ubalozini kujionesha unakijua Kirusi?

Kumbuka, kwa mchakato wa sasa wizarani ndio wanakupitisha uende ubalozini. Mchakato wa schokarship unaanza wizarani, si ubalozini.

Sasa, unaongeleaje kuwa impress watu wa ubalozini kwa Kirusi chako wakati watu wa wizarani hawajui wala kujali kirusi, wana vigezo vyao tofauti kama uwe mfanyakazi wa serikali, ambavyo wewe hujavifikisha?

Huoni kwamba una address kigezo cha ubalozini kabla ya cha wizarani wakati mchakato unaanzia wizarani?
 
Hujaelewa au unapuuza point ya msingi.

Unazungumzia kwamba ukijua Kirusi ubalozi hautakuacha.

Wakati mchakato wa scholarship umehodhiwa na serikali wizarani.

Serikali wizarani imeweka vigezo vya figisu kibao. Mfano kigezo cha mtu kuwa mfanyakazi wa serikali.

Sasa, kwa mfano wewe si mfanyakazi wa serikali, kirusi unakijua. Utapenya vipi hapa wizarani ambapo kuna kigezo cha kuwa mfanyakazi wa serikali, ili uweze kufika ubalozini kujionesha unakijua Kirusi?

Kumbuka, kwa mchakato wa sasa wizarani ndio wanakupitisha uende ubalozini. Mchakato wa schokarship unaanza wizarani, si ubalozini.

Sasa, unaongeleaje kuwa impress watu wa ubalozini kwa Kirusi chako wakati watu wa wizarani hawajui wala kujali kirusi, wana vigezo vyao tofauti kama uwe mfanyakazi wa serikali, ambavyo wewe hujavifikisha?

Huoni kwamba una address kigezo cha ubalozini kabla ya cha wizarani wakati mchakato unaanzia wizarani?
Kwa hoja yako ni kwamba Wizara ndo inawaomba ubalozi kuwa inahitaji kuwapeleka watanzania nje au!?
 
Hujaelewa au unapuuza point ya msingi.

Unazungumzia kwamba ukijua Kirusi ubalozi hautakuacha.

Wakati mchakato wa scholarship umehodhiwa na serikali wizarani.

Serikali wizarani imeweka vigezo vya figisu kibao. Mfano kigezo cha mtu kuwa mfanyakazi wa serikali.

Sasa, kwa mfano wewe si mfanyakazi wa serikali, kirusi unakijua. Utapenya vipi hapa wizarani ambapo kuna kigezo cha kuwa mfanyakazi wa serikali, ili uweze kufika ubalozini kujionesha unakijua Kirusi?

Kumbuka, kwa mchakato wa sasa wizarani ndio wanakupitisha uende ubalozini. Mchakato wa schokarship unaanza wizarani, si ubalozini.

Sasa, unaongeleaje kuwa impress watu wa ubalozini kwa Kirusi chako wakati watu wa wizarani hawajui wala kujali kirusi, wana vigezo vyao tofauti kama uwe mfanyakazi wa serikali, ambavyo wewe hujavifikisha?

Huoni kwamba una address kigezo cha ubalozini kabla ya cha wizarani wakati mchakato unaanzia wizarani?
Hapa kwa nilivyomuelewa ni kwamba hata kama mchakato unaanzia wizarani ila kitendo cha kujua culture yao ya kujua lugha yao ya kirusi basi kuna uwezekano ubalozi husika wakati wa kuselect watu ukapewa kipaombele regardless ujaenda wizarani.
 
Hapa kwa nilivyomuelewa ni kwamba hata kama mchakato unaanzia wizarani ila kitendo cha kujua culture yao ya kujua lugha yao ya kirusi basi kuna uwezekano ubalozi husika wakati wa kuselect watu ukapewa kipaombele regardless ujaenda wizarani.
Ni kweli Mkuu! Nimekuelewa! Na hoja kuu ni kuwa Wizara isaidie tu kufanikisha watu waende sio kuwa wachambuzi tena na madalali.
 
Hapa kwa nilivyomuelewa ni kwamba hata kama mchakato unaanzia wizarani ila kitendo cha kujua culture yao ya kujua lugha yao ya kirusi basi kuna uwezekano ubalozi husika wakati wa kuselect watu ukapewa kipaombele regardless ujaenda wizarani.

Huelewi wapi?

Ubalozi umepewa masharti kwamba usichukue mtu yeyote ambaye hajapitia wizarani. Wizara imekuwa ndiyo point ya kwanza ya kupitia kabla ya kufika ubalozini.

Isn't that so?

Mbona swali moja la msingi hamlijibu?

Wizara ndiyo inachuja nani wa kumpeleka ubalozini.

Ukijua Kirusi bila kutimiza vigezo vya wizarani, kama kuwa mfanyakazi wa serikali, utapenya vipi wizarani ili ufike ubalozini?

Yani mchakato ni lazima uanzie point 1 (wizarani), watu wa wizarani ndio wanaamua nani aende point 2 (ubalozini), unafikaje ubalozini kuomba scholarship ikiwa hujapenya wizarani?

Hujajibu swali hili.
 
Ni kweli Mkuu! Nimekuelewa! Na hoja kuu ni kuwa Wizara isaidie tu kufanikisha watu waende sio kuwa wachambuzi tena na madalali.
Wizara ime monopolize mchakato, ndiyo first contact ya kuchuja watu wanaoweza kupokelewa ubalozini.

Ukienda ubalozini moja kwa moja unaambiwa pitia wizarani.

Isn't that so?
 
Kwa hoja yako ni kwamba Wizara ndo inawaomba ubalozi kuwa inahitaji kuwapeleka watanzania nje au!?
Siyo kwamba wizara ndiyo inawaomba ubalozi kuwa inahitaji kuwapeleka Watanzania nje.

Wizara imeweka utaratibu kuwa scholarships zote, za nchi zote, mchakato wake unaanzia wizarani.

Kwamba mtu hawezi kujiendea mwenyewe ubalozini tu akachukua schokarship juu kwa juu.

Ukienda ubalozini, unaambiwa fuata mchakato wa kuanzia wizarani.

Umeelewa hapo?
 
Ndugu yangu hapa TZ hakuna anayetaka utoboe zaidi ya mama yako, roho za korosho sana zimejaa huko maofisi ya serikali...hizo nafasi zipo sana tu na Wala hazijazwi sababu ya roho ya kutu, mbongo anaona Bora asijaze mtu kuliko kupata wewe mtu Baki na ndivyo ilivyo si tu kwenye suala kama Hilo bali ni katika masuala chungu nzima, tuna mentality za hovyo za kwamba Bora tukose wote tu.

Adui wa mtanzania ni mtanzania mwenzake.
 
Huelewi wapi?

Ubalozi umepewa masharti kwamba usichukue mtu yeyote ambaye hajapitia wizarani. Wizara imekuwa ndiyo point ya kwanza ya kupitia kabla ya kufika ubalozini.

Isn't that so?

Mbona swali moja la msingi hamlijibu?

Wizara ndiyo inachuja nani wa kumpeleka ubalozini.

Ukijua Kirusi bila kutimiza vigezo vya wizarani, kama kuwa mfanyakazi wa serikali, utapenya vipi wizarani ili ufike ubalozini?

Yani mchakato ni lazima uanzie point 1 (wizarani), watu wa wizarani ndio wanaamua nani aende point 2 (ubalozini), unafikaje ubalozini kuomba scholarship ikiwa hujapenya wizarani?

Hujajibu swali hili.
Ok!
Uturuki walitangaza ufadhili wa masomo ambao watu iliwataka kuingia kwenye Türkiye Bursları
Je hapo Wizara inahusikaje wakati ukitazama guidlines zao zipo hivi
1722589760848.png


Nisaidie Mkuu Wizara ya Elimu inaingia sehemu ipi?!
 
Ndugu yangu hapa TZ hakuna anayetaka utoboe zaidi ya mama yako, roho za korosho sana zimejaa huko maofisi ya serikali...hizo nafasi zipo sana tu na Wala hazijazwi sababu ya roho ya kutu, mbongo anaona Bora asijaze mtu kuliko kupata wewe mtu Baki na ndivyo ilivyo si tu kwenye suala kama Hilo bali ni katika masuala chungu nzima, tuna mentality za hovyo za kwamba Bora tukose wote tu.

Adui wa mtanzania ni mtanzania mwenzake.
Safi sana!
 
Ok!
Uturuki walitangaza ufadhili wa masomo ambao watu iliwataka kuingia kwenye Türkiye Bursları
Je hapo Wizara inahusikaje wakati ukitazama guidlines zao zipo hivi
View attachment 3059402

Nisaidie Mkuu Wizara ya Elimu inaingia sehemu ipi?!
Hilo ni tangazo la Waturuki kwa dunia nzima.

Kwa Tanzania, mchakato unaanzia Wizarani. Wizara imetaka ku streamline scholarships ukienda ubalozi wa Uturuki watakuuliza kama umepitia wizarani. Hilo ni sharti walilopewa na wizara.
 
Hilo ni tangazo la Waturuki kwa dunia nzima.

Kwa Tanzania, mchakato unaanzia Wizarani. Wizara imetaka ku streamline scholarships ukienda ubalozi wa Uturuki watakuuliza kama umepitia wizarani. Hilo ni sharti walilopewa na wizara.
Nimekuelewa vyema sana Mkuu! Ndo kitu ambacho ni cha ajabu hiki kwa wizara!
 
Hizo scholarships wametaka kuzi control wizarani kwa sababu wanataka kupeana kindugu.

Hizi ndizo wamesomea hao kina Dr. Hussein Mwinyi.

Mnashangaa watoto wa watu fulani tu wanapata scholarships, wengine hawapati.
Watanzania ni wachoyo sana sijui kwanini!? Hapo unakuta hata watoto wa kina fulani wameshaandaliwa kupewa nafasi
 
Back
Top Bottom