pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 282
- 561
Binafsi naiheshimu sana sanaa kwani ni ubunifu ambao mtu anajigundua nao kisha anautumia kwa kujitafutia ridhiki huyu mchekeshaji maarufu kama MC pili pili nimemuona kwenye video moja inayozunguka mitandaoni akimuuliza bi harusi amesoma wapi, kisha akajibiwa kwamba amesoma chuo cha usimamizi wa fedha IFM halafu kwa kejeli akasema mtu aliyesomaVETA hawezi kujifananisha na huyu mtu kasomea ufund, ni kwamba hajui kama veta ni mamlaka ya elimu ya ufundi Tanzania iliyo chini ya wizara ama?
Hakuishia hapo alienda kwenye harusi nyingine akasema amesoma tu shule ya maana kwani mtoto aliyesoma sinza mapambano hawezi kuwa na muonekano wa hivi...rai yangu kwako kabla mamlaka husika haijakuchuulia hatua unapojitaftia ridhiki usitoe matamko ya dharau na kebehi kwa taasisi za serikali....kuna vyuo na taasisi nyingi tu za elimu ambazo mamlaka inapingana nazo kwani hazijasajiliwa ungeweza kuzitolea mfano
Hakuishia hapo alienda kwenye harusi nyingine akasema amesoma tu shule ya maana kwani mtoto aliyesoma sinza mapambano hawezi kuwa na muonekano wa hivi...rai yangu kwako kabla mamlaka husika haijakuchuulia hatua unapojitaftia ridhiki usitoe matamko ya dharau na kebehi kwa taasisi za serikali....kuna vyuo na taasisi nyingi tu za elimu ambazo mamlaka inapingana nazo kwani hazijasajiliwa ungeweza kuzitolea mfano