Wizara ya elimu, BASATA MC pilipili achukuliwe hatua

Wizara ya elimu, BASATA MC pilipili achukuliwe hatua

Vituko vya kwenye sherehe, na vihoja vyake huishia hukohuko kwenye sherehe. Kwani maneno mengi yanayosemwa na MC si ya kweli na wala hayalengi kumchafua mtu yoyote lakini yanalenga kuwaburudisha na kuwafanya maharusi na familia yao, waone ile ni siku yao muhimu na kwa siku ile anakuwa wa muhimu na wa heshima kuliko wote. Ndio maana hukalia viti vya kifalme na kimalkia na kuvikwa mataji. Lakini baada ya hapo taabu na dhiki zinaanza. Mwenye matatizo ni wewe unayeleta mambo ya harusini hapa. Ninyi ndio mnakuwa mnaangalia mikanda ya harusi ya watu wengine baada ya harusi unakuta limtu linasema ona hapa nimependeza, nyambafu harusi ilikuwa yako? hata kama ulialikwa kwenye kamati, mkanda wa harusi waachwe maharusi waangalie siku wanatimiza jubilei ya miaka 50 ya ndoa
Umeisema iliyo kweli Mkuu. Na ndivyo ilivyo.
 
Ushauri mzuri sana!
Lakini kumbuka MC Pilipili ni "mshereheshaji" (MC) lakini pia ni "mchekeshaji" (comedian). Kwa hiyo anapokuwa jukwaani/ktk shughuli za harusi/function yoyote hujaribu kutumia mazingira ya sehemu/mahala alipo ili kuufurahisha umma ulioko mbele yake.

Hivyo, nafikiri kuwa siyo dharau wala kebehi kwa yale anayoyafanya bali ni namna tu anavyoweza kuyatumia mazingira ili kunogesha sherehe husika. Na kwamba, sidhani kama anakuwa na lengo la kumdhaki mtu au taasisi fulani bali lengo kuu la kufanya hivo ni kufurahisha wanasherehe pekee na si vinginevyo....

Mawazo yangu lakini....
Ni makosa na anaweza akashtakiwa kwa kuharibu image ya hiyo taasisi ya serikali.

Duniani kote vyuo vya ufundi vinaheshiwa sana kwa kuwa ndio injini ya engineering industry.

Kwa taarifa yako mhitimu wa hivi vyuo vya VETA wanaajirika kirahisi kuliko mhitimu wa vyuo vyovyote unavyovijua hata kama ni chuo kikuu
 
kuchekesha watu ni kazi ngumu, msameheni tu. Na wewe mleta mada hizo harusi za watu ufuatilia za nini.
 
Sasa mkuu cha kujiuliza ni je huyo pilipili kaja lini hapa Daslama? Ukijua kua nae ni wakuja hawezi kukupa shida
 
Mleta maada ni mpumbavu mkubwa...wivu tu unakusumbua!


The Vocational Educational and Training Authority (VETA) was established by an Act of Parliament No. 1 of 1994 charged with broad tasks of coordinating, regulating, financing, Promoting and providing vocational education and training in Tanzania. The history of VETA dates back to 1940 when the Apprenticeship Ordinance was enacted to guide training in the industry. The Vocational Training Act of 1974, which established the National Vocational Training Division was replaced by the Vocational Educational and Training Act. of 1994.
Mission: To ensure provision of quality Vocational Education and Training that meets labour market needs, through effective regulation, coordination, financing, and promotion, in collaboration with stakeholders".
Vision: An excellent Vocational Education and Training system that is capable of supporting national social economic development in a global context"
 
Huwezi kumkubari kila mtu kwenye industry/sanaa/kazi au fani yoyote. Mfano, Messi10 na CR7 ktk fani ya mpira wa miguu. Wapo wanaomkubali CR7 lakini hawamkubali Messi10.

Nafikiri umenipata Mkuu...


Hapa umechemsha mkuu, yule dogo MC Pilipili hachekeshi hata kidogo, analazimisha tu.
 
Back
Top Bottom