Wizara ya elimu mpo wapi

Wizara ya elimu mpo wapi

incharge

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2011
Posts
5,017
Reaction score
8,442
Kuna tatizo kubwa kwenye ubora wa elimu yetu, mimi siyo muandishi mzuri ila nimeona mfumo wetu wa elimu unajenga watu kukariri ili ufaulu mtihani na siyo kujifunza au kuelimisha

Hii imepelekea mashule yamejikita kufanya njia yoyote hata ya haramu ili mradi wanafunzi wao wapate ufaulu wa juu na hili linachochewa na elimu kuwekwa sana kama biashara na si kwenye ubora

Leo nimeshangaa rafiki yangu mmoja nimemkuta analala kazini kumuuliza eti mtoto wake yupo shule fulani hapa Dar ambayo wameambiwa wanaanza masomo saa kumi na mbili kamili asubuhi na kutoka saa tatu usiku

Sasa nikajiuliza huyu mwanafunzi anaenda kupata elimu au kukaririshwa? Atapumzika saa ngapi? Ina maana kwa hali ya kawaida mzazi wa huyu mwanafunzi na yeye anakuwa kama anasoma

Wizara ya elimu embu jitahidini ili kufanya elimu iwe bora siyo kukariroshana
 
Tatizo ni lugha tu hakuna kingine, watoto wanajifunza mambo wasiyoyafahamu kwa lugha wasiyoifahamu, hapa hakuna miujiza zaidi ya kutumia muda mwingi kukariri.
 
Tatizo ni lugha tu hakuna kingine, watoto wanajifunza mambo wasiyoyafahamu kwa lugha wasiyoifahamu, hapa hakuna miujiza zaidi ya kukariri tu.
Ndio mtoto mdogo aamke saa kumi alfajiri ili aingie darasani saa kumi na mbili, na unamsomesha nini hadi saa tatu usiku kweli? Ndio hizi habari za vita vya majimaji?
 
Wafanye lugha moja kama watafanya kiswahili... Kama Kiingereza sawa. Lugha mbili zinachanganya kwenye masomo.
 
Ndio mtoto mdogo aamke saa kumi alfajiri ili aingie darasani saa kumi na mbili, na unamsomesha nini hadi saa tatu usiku kweli? Ndio hizi habari za vita vya majimaji?
Kwasababu anatakiwa kukariri inamuhitaji atumie muda mwingi shuleni au akariri mwenyewe akiwa nyumbani ambapo ni ngumu
 
Huu ujinga unafanyika kwenye shule za EMs pekee. Msiwege mnawapeleka watoto wenu Huko.

Haya Sasa twende Kazi. Kimbia haraka Sana Hadi kwenye shule ya Ems nenda kamtoe Huko kisha mrudishe Kayumba.

Thank me later

🙏🙏🙏🙏
 
Kuna tatizo kubwa kwenye ubora wa elimu yetu, mimi siyo muandishi mzuri ila nimeona mfumo wetu wa elimu unajenga watu kukariri ili ufaulu mtihani na siyo kujifunza au kuelimisha

Hii imepelekea mashule yamejikita kufanya njia yoyote hata ya haramu ili mradi wanafunzi wao wapate ufaulu wa juu na hili linachochewa na elimu kuwekwa sana kama biashara na si kwenye ubora

Leo nimeshangaa rafiki yangu mmoja nimemkuta analala kazini kumuuliza eti mtoto wake yupo shule fulani hapa Dar ambayo wameambiwa wanaanza masomo saa kumi na mbili kamili asubuhi na kutoka saa tatu usiku

Sasa nikajiuliza huyu mwanafunzi anaenda kupata elimu au kukaririshwa? Atapumzika saa ngapi? Ina maana kwa hali ya kawaida mzazi wa huyu mwanafunzi na yeye anakuwa kama anasoma

Wizara ya elimu embu jitahidini ili kufanya elimu iwe bora siyo kukariroshana
Wazazi wachunguze vizurii sijawahi ona shule ya mpka saa 3 usiku, iwe private hata Serikalini, isije kuwa Mwalimu anampango maalum.
 
Wazazi wachunguze vizurii sijawahi ona shule ya mpka saa 3 usiku, iwe private hata Serikalini, isije kuwa Mwalimu anampango maalum.
Tena shule maarufu tu na inaheshimika ,ila hii ya kuingia saa kumi na mbili asubuhi na kutoka saa tatu usiku ni uchizi kabisa, yani na mzazi wa huyo mtoto na wewe unageuka mwanafunzi, fikiria uamke saa kumi za usiku kumuandaa mtoto, na ukitoka kazini umsubiri mtoto hadi saa tatu usiku ndio mrudi nyumbani ,hapo hadi mfike home saa tano za usiku sasa hiyo no elimu au uchizi?
 
Back
Top Bottom