Wizara ya Elimu, Taasisi ya Elimu. Mapendekezo yenu ya Rasimu ya mabadiliko ya Mitaala bado yana mapungufu mengi

Wizara ya Elimu, Taasisi ya Elimu. Mapendekezo yenu ya Rasimu ya mabadiliko ya Mitaala bado yana mapungufu mengi

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Nimesoma Rasimu ya Mitaala inayopendekezwa, kufuatia kile kinachoitwa mabadiliko ya mitaala ya Elimu nchini

Nilichokiona katika mabadiliko hayo naweza kusema kuwa bado hakikidhi mahitaji ya Watanzania katika kupata Elimu bora ya kuwakomboa.

Katika Rasimu hiyo inayoelezea mitaala ya Elimu kuanzia Elimu ya awali hadi sekondari nimeona mapungufu tafuatayo.

1. Rasimu inawajaza watoto wetu kujua Lugha nyingi sana za Kigeni bila sababu za msingi.

Katika rasimu hii , watoto watatakiwa tangu shule za msingi kujifunza kiingereza, Kifaransa, Kiarabu na Kichina. Hizi lugha zote za kazi gani ili iweje?.

Kwa maoni yangu watoto wanatakiwa wajifunze lugha moja tu ya Kigeni, nayo ni kiingereza. Wajifunze vuzuri lugha moja, waimudu vyema.

Hii hoja eti Wachina wanakuja juu kiuchumi kwa hiyo lazima watu wetu wajue kichina ni Nonsense. Kwa maendeleo ya sasa ya tekinolojia na AI, Ukijua lugha moja ya Kigeni vizuri unaweza kuwasiliana na yeyote duniani kwa msaada wa Wa Tehama hasa Artificial Intelligence. Siku hizi kuna vifaa mtu anaongea lugha moja kifaa kinatafsiri lugha nyingine

Pili muda ambao Watoto wetu watapoteza kujifunza lugha za kichina, Kifaransa na Kiarabu wautumie kujifunza mambo mengine ya maana zaidi kama vile stadi za kazi na Kilimo

2. Rasimu haizungumzii chochote juu ya Elimu ya Ujasiriamali katika elimu ya msingi.

Nimeisoma rasimu, nimeirudia lakini hakuna mahali wala msisitizo wa kufundisha watoto wetu elimu fedha au biashara katika ngazi hii ya Elimu. Sasa kama huwezi kufundisha skills za Enterpreneurship watoto tangu wakiwa wadogo unadhani huko mbeleni utaweza kumudu kutengeneza wajasiriamali wa maana hata kama utafubdisha elimu hii baadae?

3. Rasimu haizungumzii popote namna ya kujenga Critical thinking kwa watoto wetu. Haielezi utaratibu wa midahalo tangu wakiwa wadogo. Nashangaa Rasimu imezipa lugha za kigeni nafasi kubwa lakini haitoi nafasi ya kuwajengea uwezo watoto kudanya fikra tunduizi.

4. Rasimu imekwepa kabisa kufundisha watoto wa shule za msingi Haki zao, na Wajibu wao kwa Jamii na Taifa. Sijaona popote haki za binadamu zikitajwa, Haki ya kupata viongozi wanaotokana na wao ikitajwa. Haki nyingine za kiraia na wajibu wa raia kwa Taifa havijatajwa. Kiufupi Rasimu haimjengi mtoto kujitambua kama raia.

5. Rasimu imekwepa Kufundisha watoto kuhusu Stadi za msingi za maisha za kuwaondia watu katika umasikini kama vile kilimo, ufugaji, uvuvi na ufundi. Nashangaa Rasimu inazungumzia habari za kufundisha watoto kuchonga vinyago ba kucheza ngoma lakini haifundishi hata kidogo SAYANSI KIMU, KILIMO, UFUNDI n.k

6. Hii Rasimu imeshindwa kufundisha watoto vivutio vya Utalii, watoto wajue wana vivutio gani, viko wapi n.k

7. Hii Rasimu haiinstill values kwa watoto.

Values kama vile Uchapakazi, Ukweli, Kuchukia rushwa, kukataa uzembe, Kulinda mali ya jamii na umma, kuchukia uonevu, rushwa n.k

Kiufupi, Hii Rasimu haikidhi mahitaji, na matakwa ya Watanzania wa sasa hata wa kesho. Wizara ya Elimu, na Taasisi ya Elimu jipangeni upya mje na vitu vya msingi. Hayo mambo ya kutuletea Lugha za Kigeni tupu wakati utajiri wa Utamaduni uliomo katika Makabila yetu mkiacha kabisa kuugusia hauwezi kutusaidia.

Rasimu yenyewe hii hapa chini:
 

Attachments

Duh.... Sijabahatika kuipitia lakini kama unayoyasema ni kweli, hayakuzingatiwa basi tuna safari ndefu sana ya kujikomboa. Tatizo ni kwamba hawa waliotengeneza hiyo rasimu bado ni wa kizazi kile ambacho kinaamini kufanikiwa hakupaswi kuwa kwa wote.

Yaani unakuta mtu ni profesa wa chuo kikuu lakini hataki kuona mtu wa chini yake anausogelea au hata kuufanania huo uprofesa. Yaani wana imani kuwa wakifanikiwa wengi kwenye nyanja flani basi itaonekana kama fani hiyo haina maana sana na wao watashuka kithamani.

Tunaona jinsi watu kama wanasheria na school of law walimu wao wasivyo patwa hata na mshtuko kidogo kuona namna watu wanavyofeli kila mwaka. This country needs some maombi....
 
Duh....Sijabahatika kuipitia lakini kama unayoyasema ni kweli, hayakuzingatiwa basi tuna safari ndefu sana ya kujikomboa. Tatizo ni kwamba hawa waliotengeneza hiyo rasimu bado ni wa kizazi kile ambacho kinaamini kufanikiwa hakupaswi kuwa kwa wote.

Yaani unakuta mtu ni profesa wa chuo kikuu lakini hataki kuona mtu wa chini yake anausogelea au hata kuufanania huo uprofesa. Yaani wana imani kuwa wakifanikiwa wengi kwenye nyanja flani basi itaonekana kama fani hiyo haina maana sana na wao watashuka kithamani.

Tunaona jinsi watu kama wanasheria na school of law walimu wao wasivyo patwa hata na mshtuko kidogo kuona namna watu wanavyofeli kila mwaka. This country needs some maombi....
Wizara na taasisi ya elimu wajipange upya
 
Wasomi wetu wamefuzu kwa kukopi na kupesti, wamenunua maandiko, wameandikiwa CV, wamevua nguo, wamenunua nafasi na mitihani.

Tunaweza tengeneza mtaala safi wa;
  • UBADHIRIFU
  • UZEMBE
  • ULAMBA ASALI
  • UNAFIKI
  • ULAFI
  • UBAGUZI
  • UONEVU
  • MIPASHO
  • NGONO
Ingawa kwa hizi akili zetu, tukiandikiwa hayo ndo tutafanya vizuri zaidi katika utekezaji, tukiandika wenyewe, haitaeleweka!
 
Hii ni nchi ya kipuuzi sana. Yaani sijawahi kuona mitaala ya ovyo kama hii tangu nchi hii ipate uhuru kutoka kwa mkoloni mweupe.
 
Rasimu hii nimeipitia haijaonesha uwezo wa kumtengenezea mwanafunzi au muhitimu yeyote kiu na njaa ya kutafuta maarifa kwa kumpa stadi za awali katika kutafuta taarifa sahihi ili kukuza stadi za kufikiri kwa kina, kutatua matatizo kibingwa na kuwaza kinyumbufu

Ndio maana hii nchi hatuwezi kupata wabunifu na wagunduzi wa kuipeleka nchi yetu mbele

Kiukweli hakuna ukomo kwenye kuwaza au kufikiri na hata kutenda jambo lakini kunapaswa kuanzia shuleni

Yesu anasema hivi, heri wenye njaa na kiu ya haki maana hao watashibishwa. Maana yake kuna mambo ya Msingi lazima yajengwe kwa watu ili wamalizapo elimu fulani wawepo kwenda mbele kinamna nyingine kwa misingi na njia zao wenyewe baada ya kuhitimu mafunzo kwenye ngazi fulani

Rasimu hii hapana itatupeleka chaka na huoni nini tunajenga kwa kizazi chetu baada ya miaka kumi au ishirini ijayo
 
Rasimu hii nimeipitia haijaonesha uwezo wa kumtengenezea mwanafunzi au muhitimu yeyote kiu na njaa ya kutafuta maarifa kwa kumpa stadi za awali katika kutafuta taarifa sahihi ili kukuza stadi za kufikiri kwa kina, kutatua matatizo kibingwa na kuwaza kinyumbufu

Ndio maana hii nchi hatuwezi kupata wabunifu na wagunduzi wa kuipeleka nchi yetu mbele

Kiukweli hakuna ukomo kwenye kuwaza au kufikiri na hata kutenda jambo lakini kunapaswa kuanzia shuleni

Yesu anasema hivi, heri wenye njaa na kiu ya haki maana hao watashibishwa. Maana yake kuna mambo ya Msingi lazima yajengwe kwa watu ili wamalizapo elimu fulani wawepo kwenda mbele kinamna nyingine kwa misingi na njia zao wenyewe baada ya kuhitimu mafunzo kwenye ngazi fulani

Rasimu hii hapana itatupeleka chaka na huoni nini tunajenga kwa kizazi chetu baada ya miaka kumi au ishirini ijayo
Hii Rasimu imepwaya sana.
Wataalamu wetu warudi kwenye drawing board.
 
Wange focus zaidi na stadi za maisha, values and morals kiundani, critical thinking ni muhimu, pia lugha moja inatosha.
In short elimu yetu ingejikita ku solve matatizo yetu yanayotuzunguka kuliko kuhangaika na ki china wakati hata ku masta mazingira yetu watu wameshindwa
 
Kwenye lugha za kimataifa wako sahihi

Serikali inachotaka kufanya ndicho kilichoko shule za kimataifa watoto hufunxwa lugha nyingi za kimataifa toka ngazi ya chini

Wazazi wengi hawana uwezo kupeleka watoto hizo shule ambazo ada kiwango cha chini ni milioni 16 kwa mwaka na watu hupeleka ili watoto wao waandaliwe kimatsifa ukiwemo uwezo wa lugha mbalimbali za kimataifa

Hilo la lugha nyingi libaki hivyo hivyo ili na watoto wa Kawaida wa mtanzania awe level moja na mtoto anayesoma interest school kwa upande wa kumudu lugha nyingi za kimataifa
 
Wange focus zaidi na stadi za maisha, values and morals kiundani, critical thinking ni muhimu, pia lugha moja inatosha.
In short elimu yetu ingejikita ku solve matatizo yetu yanayotuzunguka kuliko kuhangaika na ki china wakati hata ku masta mazingira yetu watu wameshindwa
Well said. Naunga mkono hoja yako.

Lugha nyingi za kimataifa ili iweje?. Ukijua Kiingereza vizuri, unaweza kuwasiliana na yeyote duniani, kusoma chuo chochote duniani, kufanya biashara popote duniani.

Hii ya kuwajaza watoto lugha za kigeni vichwani badala ya stadi za kazi na maisha itawasaidia nini?.

Hata hao wachina na waarabu wako busy kuwafundisha watoto wao kiingereza. Sasa sisi tunataka wasome lugha zote hizo za nini wakati sisi kama Taifa tuna vitu vingi sana muhimu vya kutaka kujifunza!
 
Well said. Naunga mkono hoja yako.
Na kingine ingetakiwa mitaala iwe physical mfano ujasiriamali, masomo ya michezo na talents ili wenye vipaji waanze kuanzia chini ili hata akimaliza form form licha ya kumaliza kile kipaji anaweza kujiajiri na kupunguza ajira,masomo ka cookery wakisoma tangu chini Hadi form four mtu anaweza kujiajiajiri hata mama ntilie, masomo ya ushonaji, makeup, na vitu kama ufundi hata mechanical, umeme vyote wakianza mapema Hadi hyo form four tayari watoto watajua mengi hii itasaidia kujiajiri. So serikali I focus na elimu ku solve changamoto zetu zaidi kuliko ku cremishana na mtoto kupata A zote huku hawezi ku solve changamoto yoyote.
 
Sidhani kama hayo masomo yote yatakuwa ya lazima. Kifaransa na kiarabu vipo kwenye mitaala hata sasa, lakini ni masomo ambayo mwanafunzi anao uhuru wa kuchagua.

Ni vema rasimu iweke wazi masomo yapi ni ya lazima kwa wote na yapi mwanafunzi anaweza kuchagua.

Mtu mmoja kujifunza kichina, kiarabu, kifaransa na kiingereza ni dalili za uendawazimu.
 
Nina mtizamo kama wako mkuu kwakweli sijaona sababu za msingi za kuwajazia watoto lugha zote hizo katika kipindi cha sayansi na technolojia, nilitegemea wangeangalia namna ya kuboresha hii lugha moja ya dunia ambayo ni kiingereza ambacho bado kwetu ni tatizo kuzungumzwa na wahitu wengi tu wa degree. Sasa humchanganyie mtoto kichina, kiarabu bado kifaransa sindokumpoteza kabisa l, unaweza kukuta watoto wanabuni lugha zao wenyewe kutoka kwenye huo mchanganyiko.

Mtaala unapaswa kujikita kwenye kutoa elimu ya tehama, biashara, ufundi, ufugaji na uvuvi haya ndio yanaakisi maisha ya familia nyingi tulizotoka, kumfundisha mtoto hizi lugha za kigeni ni kuanza kumtenga na jamii yake taratibu hapa tutaanza kupata wachina weusi waarabu weusi, wafaransa weusi, na tutatengeneza matabaka ya ajabu na kupata vijana wavivu wavivu, tutoe elimu itayotujengea kujiamini zaidi na kufanya kazi popote duniani lugha sio kikwazo kikubwa ikiwa mtu anaujuzi hizi lugha tuwaachie wale wanaotaka kuongoza watalii. Nchi yetu ni yawakulima, wavuvi, wafugaji, elimu yetu itilie nguvu huko kwa kufundisha technolojia ya kilimo na ufugaji kuanzia elimu ya awali
 
Nina mtizamo kama wako mkuu kwakweli sijaona sababu za msingi za kuwajazia watoto lugha zote hizo katika kipindi cha sayansi na technolojia, nilitegemea wangeangalia namna ya kuboresha hii lugha moja ya dunia ambayo ni kiingereza ambacho bado kwetu ni tatizo kuzungumzwa na wahitu wengi tu wa degree. Sasa humchanganyie mtoto kichina, kiarabu bado kifaransa sindokumpoteza kabisa l, unaweza kukuta watoto wanabuni lugha zao wenyewe kutoka kwenye huo mchanganyiko.

Mtaala unapaswa kujikita kwenye kutoa elimu ya tehama, biashara, ufundi, ufugaji na uvuvi haya ndio yanaakisi maisha ya familia nyingi tulizotoka, kumfundisha mtoto hizi lugha za kigeni ni kuanza kumtenga na jamii yake taratibu hapa tutaanza kupata wachina weusi waarabu weusi, wafaransa weusi, na tutatengeneza matabaka ya ajabu na kupata vijana wavivu wavivu, tutoe elimu itayotujengea kujiamini zaidi na kufanya kazi popote duniani lugha sio kikwazo kikubwa ikiwa mtu anaujuzi hizi lugha tuwaachie wale wanaotaka kuongoza watalii. Nchi yetu ni yawakulima, wavuvi, wafugaji, elimu yetu itilie nguvu huko kwa kufundisha technolojia ya kilimo na ufugaji kuanzia elimu ya awali
Well said.
Naunga mkono hoja!
 
Nimesoma Rasimu ya Mitaala inayopendekezwa, kufuatia kile kinachoitwa mabadiliko ya mitaala ya Elimu nchini

Nilichokiona katika mabadiliko hayo naweza kusema kuwa bado hakikidhi mahitaji ya Watanzania katika kupata Elimu bora ya kuwakomboa.

Katika Rasimu hiyo inayoelezea mitaala ya Elimu kuanzia Elimu ya awali hadi sekondari nimeona mapungufu tafuatayo.

1. Rasimu inawajaza watoto wetu kujua Lugha nyingi sana za Kigeni bila sababu za msingi.

Katika rasimu hii , watoto watatakiwa tangu shule za msingi kujifunza kiingereza, Kifaransa, Kiarabu na Kichina. Hizi lugha zote za kazi gani ili iweje?.

Kwa maoni yangu watoto wanatakiwa wajifunze lugha moja tu ya Kigeni, nayo ni kiingereza. Wajifunze vuzuri lugha moja, waimudu vyema.

Hii hoja eti Wachina wanakuja juu kiuchumi kwa hiyo lazima watu wetu wajue kichina ni Nonsense. Kwa maendeleo ya sasa ya tekinolojia na AI, Ukijua lugha moja ya Kigeni vizuri unaweza kuwasiliana na yeyote duniani kwa msaada wa Wa Tehama hasa Artificial Intelligence. Siku hizi kuna vifaa mtu anaongea lugha moja kifaa kinatafsiri lugha nyingine

Pili muda ambao Watoto wetu watapoteza kujifunza lugha za kichina, Kifaransa na Kiarabu wautumie kujifunza mambo mengine ya maana zaidi kama vile stadi za kazi na Kilimo

2. Rasimu haizungumzii chochote juu ya Elimu ya Ujasiriamali katika elimu ya msingi.

Nimeisoma rasimu, nimeirudia lakini hakuna mahali wala msisitizo wa kufundisha watoto wetu elimu fedha au biashara katika ngazi hii ya Elimu. Sasa kama huwezi kufundisha skills za Enterpreneurship watoto tangu wakiwa wadogo unadhani huko mbeleni utaweza kumudu kutengeneza wajasiriamali wa maana hata kama utafubdisha elimu hii baadae?

3. Rasimu haizungumzii popote namna ya kujenga Critical thinking kwa watoto wetu. Haielezi utaratibu wa midahalo tangu wakiwa wadogo. Nashangaa Rasimu imezipa lugha za kigeni nafasi kubwa lakini haitoi nafasi ya kuwajengea uwezo watoto kudanya fikra tunduizi.

4. Rasimu imekwepa kabisa kufundisha watoto wa shule za msingi Haki zao, na Wajibu wao kwa Jamii na Taifa. Sijaona popote haki za binadamu zikitajwa, Haki ya kupata viongozi wanaotokana na wao ikitajwa. Haki nyingine za kiraia na wajibu wa raia kwa Taifa havijatajwa. Kiufupi Rasimu haimjengi mtoto kujitambua kama raia.

5. Rasimu imekwepa Kufundisha watoto kuhusu Stadi za msingi za maisha za kuwaondia watu katika umasikini kama vile kilimo, ufugaji, uvuvi na ufundi. Nashangaa Rasimu inazungumzia habari za kufundisha watoto kuchonga vinyago ba kucheza ngoma lakini haifundishi hata kidogo SAYANSI KIMU, KILIMO, UFUNDI n.k

6. Hii Rasimu imeshindwa kufundisha watoto vivutio vya Utalii, watoto wajue wana vivutio gani, viko wapi n.k

7. Hii Rasimu haiinstill values kwa watoto.

Values kama vile Uchapakazi, Ukweli, Kuchukia rushwa, kukataa uzembe, Kulinda mali ya jamii na umma, kuchukia uonevu, rushwa n.k

Kiufupi, Hii Rasimu haikidhi mahitaji, na matakwa ya Watanzania wa sasa hata wa kesho. Wizara ya Elimu, na Taasisi ya Elimu jipangeni upya mje na vitu vya msingi. Hayo mambo ya kutuletea Lugha za Kigeni tupu wakati utajiri wa Utamaduni uliomo katika Makabila yetu mkiacha kabisa kuugusia hauwezi kutusaidia.

Rasimu yenyewe hii hapa chini:
Asante sana. Hongera kwa kuleta mada hii muhimu na uchambuzi makini.

Nitaisoma na kuwasilisha maoni/michango na ushauri accordingly.
 
Na kingine ingetakiwa mitaala iwe physical mfano ujasiriamali, masomo ya michezo na talents ili wenye vipaji waanze kuanzia chini ili hata akimaliza form form licha ya kumaliza kile kipaji anaweza kujiajiri na kupunguza ajira,masomo ka cookery wakisoma tangu chini Hadi form four mtu anaweza kujiajiajiri hata mama ntilie, masomo ya ushonaji, makeup, na vitu kama ufundi hata mechanical, umeme vyote wakianza mapema Hadi hyo form four tayari watoto watajua mengi hii itasaidia kujiajiri. So serikali I focus na elimu ku solve changamoto zetu zaidi kuliko ku cremishana na mtoto kupata A zote huku hawezi ku solve changamoto yoyote.
Sahihi sana!
 
Back
Top Bottom