Wizara ya Madini imesema inafuatilia jiwe la bilioni 240 linalopigwa mnada Dubai, yasema ilipata taarifa mtandaoni

Wizara ya Madini imesema inafuatilia jiwe la bilioni 240 linalopigwa mnada Dubai, yasema ilipata taarifa mtandaoni

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo wa mbunge Mkinga, Dastan Kitandula ameuliza bungeni kuhusu jiwe la Tanzania linalopigwa mnada Dubai, Uarabuni. Naibu waziri wa madini amesema nao waliona mtandaoni na wanafatilia.

=====

Dansatan Kitandula: Mheshimiwa spika, jiwe la ruby lenye uzito wa kilo 2.8 lipo kwenye maonesho kwasasa Dubai na jiwe hili linasadikika linatoka Tanzania na kwamba siku chache zijazo kutakuwa na mnada wa kuuza jiwe hili. Je kama nchi tunanufaika vipi na mnada huo?

Naibu waziri wa Madini: Ni kweli mnamo tarehe 13 April mwaka huu wizara ya madini ilipata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kwamba kuna jiwe la madini ya ruby lenye uzito wa kilo 2.8 na ambalo linadaiwa kuwa na thamani ya dola milioni 120 sawa na zaidi ya bilioni 240 ambalo limepewa jina la bald al hamal na ambalo linakwenda kuwekwa mnadani ndani ya siku 30 baada ya mfungo na jiwe hilo kudaiwa limetoka Tanzania.

Mara baada ya kupata habari hizi, wizara ya Maliasili imechukua hatua za haraka kutafuta kama habari ni za kweli na kama jiwe hili limetoka Tanzania na kwasababu jiwe hili limeshavuka mipaka lipo kwenye nchi nyingine.

Taarifa hizi sasa ambazo tunazikusanya zinahusisha nchi za Dubai na tayari tunafanya mawasiliano na ubalozi wetu kufuatilia ukweli, pia tumebaini mmiliki wa sasa wa jiwe hilo yuko nchini Marekani na mawasiliano naye tumeshafanya tangu jana.

Tutapopata nyaraka za usafirishaji kama kweli limetoka Tanzania, thamani na asili, nyaraka za mauzo tutaleta taarifa bungeni na kama ni la kwetu niwahakikishie watanzania haki yao haitapotea.

Pia, soma=> Ruby yenye thamani ya bil 276 ilisafirishwa kimagendo huko Dubai? Serikali haina taarifa ilifikaje

=> Mali yetu inauzwa mnada wa Dubai Madini ya Ruby

 
Smuggling ya gemstone, fuel, arms, illegal drugs na human trafficking ndiyo biashara zinazongoza kwa ukubwa duniani.

Kupambana na hizi ni kazi ngumu sana. You can win some and lose some
 
Smuggling ya gemstone, fuel, arms, illegal drugs na human trafficking ndiyo biashara zinazongoza kwa ukubwa duniani.

Kupambana na hizi ni kazi ngumu sana. You can win some and lose some
Is this a justification?
 
Hii nchi usanii, wizi na upuuzi ndio mahala pake....

Kama ni wizi na liliibiwa si angalau hata jina limetumika kwamba ni Tanzania (yaani angalau tunapata promo kuhusu kuna kitu kama hiki ) kuliko hata promo hio isingepatikana...

Hivyo hii issue iwe handled delicately kama ni uzushi hii kitu haijatokea Tanzania (basi wa-mute) kama ni ujambazi jamaa alifanya basi wasubiri aingie kwenye 18 zao..., ila kusema hawajui na waliona tu kwenye mitandao inaonyesha vipi hawapo informed huenda wangejua na wao wangepeleka Tanzanite zao huko zikapigwe minada
 
Wizara inapata taarifa mitandaoni.

Hizi ndio wizara imara kabisa za awamu ya sita.

Mkuu yupo huko ananadi filamu.
 
... tulipata taarifa "kupitia mitandao ya kijamii". Mbona yule mwehu alitamani ifungiwe?
Alitaka ifungwe kwa sababu haina maana ndio hata Samia anasema wanaodai katiba mpya sio wananchi huku mitaani bali mitabdaoni huko kwa maana haina uzito.
 
Back
Top Bottom