Tetesi: Wizara ya Mambo ya ndani kupitia Idara ya Uhamiaji yapiga "stop" utoaji wa Passport

Tetesi: Wizara ya Mambo ya ndani kupitia Idara ya Uhamiaji yapiga "stop" utoaji wa Passport

barafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2013
Posts
6,739
Reaction score
32,880
Kuna uzi uliletwa humu JF siku kadhaa zilizopita ukieleza kuwa Idara ya Uhamiaji imesimamisha utoaji wa hati ya kusafiria(Passport) kwa sababu ya upungufu/ukosefu wa karatasi za kuandalia passport hiyo.Hii ilikuwa hata ukituma maombi kwenye ofisi za mikoa kuja makao makuu,majibu ilikuwa kwa sasa zoezi la kutoa "passport" limesimamishwa mpaka hapo Idara itakapopata karatasi za kuandalia passport hizo.

Hata wale "vishoka" wenye kujua mbinu za kupenyeza mpaka kitengo cha kuandalia passport Makao Makuu ya Uhamiaji Kurasini wanasema hata kwa dau lolote kwa sasa passport ni ngumu kupatikana.Wenye njia za mkato waliokuwa na uwezo wa kupenyeza "rupia" ili kufanyiwa msaada wa haraka nao wamegonga mwamba kuwa hata kwa "hela ya kiwi" kwa sasa passport ni ngumu sbb "zoezi la utengenezwaji" limesamamishwa kwa sbb ya uhaba wa "malighafi" za kutengenezea.

Tetesi za ndani ya Idara hiyo zinasema ni agizo toka "juu" kuwa zoezi hilo limatakiwa kusimama kwa muda,kwani ktk mikono ya watu wengi kwa sasa,kuna hati za kusafiria kwa watu ambao sio raia halali wa Tz na wamepata hati hizo katika mazingira ya rushwa na tatanishi.Hivyo zoezi la kutoa hati hizo limesitishwa kwa muda ili kutengeneza utaratibu mpya wa kupatikana kwa hati hizo kwa wale waombaji wa mara ya kwanza na wale wanaotaka kuhuhisha.

Maana kwa kipindi kirefu ilikuwa inawezekana kupata hati ya kusafiria ndani ya siku tano ili hali kiuhalisia zoezi huchukua wiki mbili hadi mwezi ili wenye mamlaka kujiridhisha uhalali wa muombaji.Ngawila ilikuwa ni moja ya kigezo cha kupata hati ya kusafiria ya Tz na wala si uraia wa mtu.

Tutege sikio na kusubiri juu ya "Tetesi" hizi.Muhimu ni "JF be the first to know"
image.jpeg
 
Japo pasipoti ni haki ya kila mtanzania lakin serikali lazima ijiridhishe na waombaji japo kwa mfumo wa tanzania ni vigumu ku monitor maana kama wangetaka wangeanza kutengeneza mifumo tangu mtoto anapozaliwa kuwe na system ya kuupdate taarifa kwa kila hatua ya makuzi ya mtoto hadi kuwa mtu mzima
 
Huenda kuna jambo wameliona kuwa na dosari na sasa wanalishughulikia, tujipe muda naamini wanafanya kwa nia njema yenye maslahi kwa watanzania
 
Kuna hii miziki ya vijana mtu mmoja alisema sjui ni umaarufu sjui ni nini mtanisaidia mmaojua haya mambo.

Alisema kuwa umaarufu sjui ni mzigo wa miba ukiubeba utafanyaje sjui, hebu vijana wekeni sawa hii sentensi/tungo. Sahihisha hapa.
 
Haya matamko ya mfulizo sijajua mwisho wake utakuwaje!
 
Ina maana hata kama mtu ana dharura ya kwenda kutibiwa nje ya nchi na hana passport ataachwa afe?!
 
Nchi inakosa karatasi za kutengenezea passport?
 
Namshukuru Mungu yangu nimerenew mwaka huu
 
Kuna hii miziki ya vijana mtu mmoja alisema sjui ni umaarufu sjui ni nini mtanisaidia mmaojua haya mambo.

Alisema kuwa umaarufu sjui ni mzigo wa miba ukiubeba utafanyaje sjui, hebu vijana wekeni sawa hii sentensi/tungo. Sahihisha hapa.
Fid Q usuper staà mzigo wa mibaa
 
Back
Top Bottom