Wizara ya Nishati kuajiri vijana 139 kusimamia miradi ya Umeme vijijini

Wizara ya Nishati kuajiri vijana 139 kusimamia miradi ya Umeme vijijini

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Waziri wa Nishati, Januari Makamba ametangaza kuajiri vijana 139 watakaosambazwa katika Halmashauri zote nchini ili wawe waratibu wa Miradi ya REA katika maeneo yao.

Makamba amesema hayo Julai 13, 2022 akizingumza Bariadi Simiyu

“Vijana hawa 139 kazi yao ni kufuatilia miradi imefikia hatua gani, mfano kama vifaa vya umeme vimefika katika maeneo yao, kama nguzo zimechimbiwa mashimo, kama zimesimamishwa na kama nyaya zimevutwa, vijana hawa watakuwa pia kiungo cha mawasiliano kati ya Wizara, Tanesco, viongozi wa Serikali na kisiasa pamoja na wadau wengine wanaohusika na miradi hii” amesema Makamba

Chanzo: Instagram ya Wizara ya Nishati Tanzania
 
Kwani hakuna viongozi wa Tanesco huko wilayani na vijijini?

Mbona Tarura wanajenga barabara bila kuajiri hao vijana 139? Kwa ngonjera hizi vijiji 2000 vilivyobaki havitaisha kupata umeme mpaka tunafika 2025
 
Kwani hakuna viongozi wa Tanesco huko wilayani na vijijini?

Mbona Tarura wanajenga barabara bila kuajiri hao vijana 139? Kwa ngonjera hizi vijiji 2000 vilivyobaki havitaisha kupata umeme mpaka tunafika 2025
Kwani hata wewe hutaki ajira Etweege,ngoja wasio na ajira wakushukie na kwenda na wewe kusikojulikana🤔
 
Waziri wa Nishati, Januari Makamba ametangaza kuajiri vijana 139 watakaosambazwa katika Halmashauri zote nchini ili wawe waratibu wa Miradi ya REA katika maeneo yao.

Makamba amesema hayo Julai 13, 2022 akizingumza Bariadi Simiyu

“Vijana hawa 139 kazi yao ni kufuatilia miradi imefikia hatua gani, mfano kama vifaa vya umeme vimefika katika maeneo yao, kama nguzo zimechimbiwa mashimo, kama zimesimamishwa na kama nyaya zimevutwa, vijana hawa watakuwa pia kiungo cha mawasiliano kati ya Wizara, Tanesco, viongozi wa Serikali na kisiasa pamoja na wadau wengine wanaohusika na miradi hii” amesema Makamba

Source: Instagram ya Wizara ya Nishati Tanzania
Hii strategy mbovu kabisa
 
Kwani hakuna viongozi wa Tanesco huko wilayani na vijijini?

Mbona Tarura wanajenga barabara bila kuajiri hao vijana 139? Kwa ngonjera hizi vijiji 2000 vilivyobaki havitaisha kupata umeme mpaka tunafika 2025
Acheni wivu nyie wachawi....tunahitaji maendeleo nchi hii sio usanii wa yule mchawi.
 
Deal la kuwatafutia ulaji maswahiba zake!

Na utakuta hao vijana watafanya pia kazi ya kumkampenia kwa ajili ya urais!
 
Deal la kuwatafutia ulaji maswahiba zake!

Na utakuta hao vijana watafanya pia kazi ya kumkampenia kwa ajili ya urais!
Mtakufa nacho kijiba cha roho... halafu nna wasiwasi wewe ndio etwege.
 
Eagle House wazee wa Kaunda suti,vipi wameshindwa kazi.
Nchi ngumu hii!!!
 
Kwani hakuna viongozi wa Tanesco huko wilayani na vijijini?

Mbona Tarura wanajenga barabara bila kuajiri hao vijana 139? Kwa ngonjera hizi vijiji 2000 vilivyobaki havitaisha kupata umeme mpaka tunafika 2025
Leo wanaajiri mnalalamika?!

Kweli hamna shukrani
 
Nini kazi ya DSO na vijana wake????

Uncoordinated Government?
Sijui watakuwa wanafanya kazi gani kwa kweli..

Labda Makamba anataka specialization hapa..na hao vijana wa DSO ukute ni only security and safety watchers na sio miradi ya maendeleo
 
Nilikuwa nikimuona huyu jamaa kichwa, kumbe ni vice versa, anakuja mkakati wa dharura kwa sekta mtambuka kama hii inayohitaji mipango ya muda mrefu, kwa nchi hii bila kuifumua Tanesco na kuruhusu sekta binafsi kama ilivyofanywa kwenye mitandao ya simu, bado tutaendelea na matatizo umeme kwa miaka 1000 zaidi ijayo! Tanesco ndio jipu la matatizo yote ya umeme nchini! Na serikali haitaki kuukubali ukweli huu mchungu kuibinafsisha. maana ndilo shirika mama serikali inapovuta pesa muda wowote inapojiskia.
 
Back
Top Bottom