Habari wakuu, kumekuwa na malalamiko mengi sana kuhusu bodi kutokufanya marejesho ya baadhi ya wanufaika ambao walikatwa fedha za ziada baada ya kumaliza mkopo, yani kama mtu alikuwa anadaiwa milioni kumi, unakuta bodi wamemkata ziada labda 10.6m. Kikawaida hiyo laki 6 inatakiwa irejeshwe kwa mwenyewe baada ya kufikisha malalamiko. Lakini kimekuwa ni kilio cha wengi kuwa wameshapeleka malalamiko lakini bodi hairudishi fedha zao za jasho. Hivyo ni vyema bodi wajitafakari au mamlaka za dola ziingie kazini.