World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

Brazil leo ipigwe tu,tumechoka sana.
ikifanya fujo itapigwa tu
 
Leo sina mpango na timu za leo, ngoja nikalale nisubiri mtifuano wa kesho.
 
TANESCO wamekata umeme.... Sijui wana mpango gani na mechi ndo inakaribia.
 
Jamani mwenzenu nipo teamHOLLAND, sina muda na hao waSABAto..!!!
 
Wesley Sneijder sidhani kama atacheza kwa sababu ya hamstring kwenye "match build-up"
 
Watu wanashangaa kwa nini Brazil kumetulia...kuna aina ya kipigo ambacho ni kama dawa. Kama wangefungwa bao moja tu ama mbili kusingekalika lakini saba! Hiyo inaitwa "shock treatment" na inachukua muda kurudiwa na fahamu. Ni kama kugusa waya wa umeme, inachukua muda kuzinduka na hata utakapozinduka ni vigumu kuamini/kuelezea kilichokupata. Mnara wa Babeli uliochukuwa miaka zaidi ya hamsini kuujenga ghafla umeporomoka...kaazi kweli kweli! Ziko timu zilikuwa zinafungwa na Brazil hata kabla ya pambano kwa sababu tu ya hofu...Brazil! Lakini sasa zote zimepata nguvu...alaa kumbe na yenyewe inaweza kubebeshwa kapu la magoli kama timu nyingine tu. Hiyo hofu sasa imehamia kwenye kambi ya Brazil yenyewe...kumbe timu yetu ni ya kawaida tu kama timu zingine!
 
You believe on Jamvi la wageni?

Hahahahahahahaaa! Poleni sana wadau!

Kilichotokea Jumanne hakitatokea tena.

Unless waache tena kucheza kama walivyoacha kucheza siku ile.

Timu yoyote inayoacha kucheza kwenye mchezo wa ushindani hushindwa vibaya.

Na baada ya kuadhirishwa siku ile, sidhani kama wako tayari kuadhirishwa tena.

I am telling you that loss will bring the best out of Brasil in the future.

Russia 2018 is our year.
 

Nakubaliana na wewe hapo. Kile kipigo ni lazima upooze maana hata waliokitoa (Wajerumani) nao hawakuamini yaliyotokea na sidhani hata wao wamesha-recover kutoka kwenye mshangao wao.

Magoli manne ndani ya dakika sita? Are you kidding me?
 
Nakubaliana na wewe hapo. Kile kipigo ni lazima upooze maana hata waliokitoa (Wajerumani) nao hawakuamini yaliyotokea na sidhani hata wao wamesha-recover kutoka kwenye mshangao wao.
Magoli manne ndani ya dakika sita? Are you kidding me?
Mshangao sawa, lakini wa aina gani? Positive or negative? Unatia moyo au unakatisha tamaa...hiyo ndiyo tofauti kati ya Germany na Brazil!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…