World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

Serilakali ya Ghana imepeleka washangiliaji 500 Brazil kwaajili ya hawa Black stars, sasa wakitolewa mapema watarudi nao hao.
Nini Serikali ya Ghana ya Kenya Imepeleka timu ya Taifa ili wapate moto wakutaka kufika WorldCup Kenya sie tungewapeleka Bongo Flava na sio timu ya mpira.
 
Tuseme ukweli tusipende majina makubwa bila kuangalia mchango wao na ushiriki wao kwenye hii timu. Prince Boateng, kwa muda mrefu aliomba kujiuzulu kwenye timu ya taifa ya Ghana, ila alivyoona Ghana inakaribia kufuzu akarudi tena, na hata ile mechi ya kwanza ambayo waliibomoa Misri hakucheza alikuwa benchi na mechi ya pili kule Misri alianzia benchi.

Essien mchango wake naye umekuwa mdogo kwa hii timu, na nani asiyejua kwamba amechuja kias kwamba god father wake Mourhino aliamua kumtema.

Gyan naye anachezea jina, aliamua kufuata hela kucheza ligi za umangani na kukimbia changamoto za ligi za ulaya na hasa alipokuwa EPL, na si ajabu kiwango chake kimeshuka.
 
Wakuu nimeanza kuogopa.nilidhani hatupati nafasi za kufunga lakini pale tunapopata nafasi halafu tunapiga fyongo,naogopa maana kuweka mpira wavuni ni "ancient nightmare" kwa waafrika.
 
Wamarekani wamechoka hawa, hawajazowea kucheza katika joto .... Ghana shambulia shambulia
 
Jamani eeh na sisi leo tuna gundu kama Greece tu kwa kweli, mabao tumekosa mengi.
 
Nasikia chants za USA USA USA USA USA USA USA USA USA USA USA.......................
 
Walau kwa sasa ghana wanaelekea kwenye matumain
 
angalau Boateng anaanza kuwachezesha wenzake football ya maana sio ya viwanja vya magunia Msasani!
 
Alimchukua kwa ajili ya plan B, pale plan A inaposhindwa kuleta mafanikio. 2010, England ilikwenda South Afrika, wakaona hawana kiungo, walimwita Scholes, lakini yeye alikataa kwa sababu hakushiriki kwenye michezo ya awali ya kwenda Bondeni ili asiwavunje moyo wachezaji wa England. Kwetu huku hakuna atakayekuelewa ukimwacha mchezaji wa kiwango cha Prince hata Raisi anaweza kuingilia kati.
 
Hatuwezi kuendelea kupoteza hizi nafasi, tutazijutia Waafrika... Sitaki kusikia huu upuuzi katika news za leo usiku na kesho asubuhi, maana Marekani wakishinda hii itakuwa siku nzima kuanzia ESPN hadi CNN
 
Back
Top Bottom