6am-9am and 3pm-7pm Ali Hassan Mwinyi Road will be closed, Ohio closed off/on ,Nyerere road closed off/on.
· Mwenge area near mlimani city,Buguruni ,Uhuru and the city centre will be impassable during certain hours.
muda ndo huo hapo 12-3 asubuhi, na jioni saa 9-1 usiku kuazia tarehe 4-7 May 2010 mbona mtakoma uko dar?
Hii imekaa wazi kabisa. Mbona mnashindwa kuiona?
Watu sasa hivi Dar wataanza kuongelea Ugeni na foleni za Dar na si MGOMO. Media zote zitajadili ugeni huo na kuacha kuongelea Mgomo. Naungana na wengine wanaoombea Mvua ya gharika inyeshe ili hao WAGENI wasiotutakia mema Tanzania (nina uhakika wanafahamu kwa nini wanakuja/mgomo) basi wakione cha moto. Na ikinyesha basi watu tapisheni vyoo vyenu kwa nguvu hasa Nyerere Road.
Hii hufanywa na nchi nyingi sana. Wakati wa Yeltsin huko Russia, baada ya kugundua maasi yanaweza kufanyika, basi Yeltsin aliona dawa ni kuwa karibu na jeshi. Hilo bunge acha wajitenge (duma). Baada ya Yeltsin kutumia mabavu kuvunja bunge bila kufuata katiba, bunge liliamua kumuondoa yeye na kumuweka makamu wa Rais (mwaka 1993) na matokeo yake Jeshi liliingilia kati.
Kuhusu maasi kutokea, yeltsin alifahamu mapema na akawa hana jinsi ya kujisogeza karibu na wanajeshi. Akasuka mipango yake (nafikiri alishirikiana na USA) na wakaona dawa ni kumpeleka Marehemu Michael Jackson. President Yeltsin kwa kutumia kisingizio cha kuandaa UGENI WA MICHAEL JACKSON, akawa kajisogeza karibu sana na wanajeshi. Wale wabunge na jamaa waliovamia White house na kujifungia, vilitumwa vifaru na vikarusha risasi chache na jengo likawaka moto kidogo tu. Ugomvi ukaisha na mtu aliyesaidia kuzimisha akawa Michael Jackson. Sijui hata alifahamu kuwa alitumika au laa ingawa MJ mara nyingi sana walimtumia. Kila nchi iliyokuwa na uhusiano mbaya na USA, alitumwa huko MJ na wale waliokuwa wakichoma bendera ya USA jana, basi kesho yake walikuwa wanaonekana wakifurahia concert na kubeba bendera ya USA.
Picha ya kwanza: Vifaru vinashoot Russian White house.
Jengo lilivyokuwa baada ya vifaru kuondoka.
Michael akiwa kazini kumsafishia njia (hapa kashasafisha tayari, Mageneral wote wako kwa Yeltsin) President Yeltsin.
Huu ugeni unaokuja kesho na kesho kutwa unaanza mgomo, hauna tofauti sana na bwana hapo juu mwenye miwani na Rungu la dola.