ikiumasema
JF-Expert Member
- Oct 9, 2015
- 923
- 1,299
Katika kesi hii ya Feisal nina maswali mengi sana ya kujiuliza?Mimi namtizama Fei Kama mchezaji kiongozi kwa wachezaji wengi wa kitanzania kwa Sasa.
Vijana wengi wadogo wanavutiwa na uwezo wake
Sasa nini kilimkuta Feisal mpaka haya yanayomtokea sasa hivi?
Feisali alipata ushauri kwa Nani au Ni utashi wake tu?
Nimemsikia wakili wake akisema hakushitikishwa katika kile wanachokiita kuvunja mkataba je hakuona umuhimu wa ushauri wa kisheria?
Baada ya kushindwa TFF je akienda FIFA akishindwa itakuwaje?
Mimi naona Kama Feisali alikuwa na room mzuri sana ya kuondoka Yanga bila mikwaruzano yeyote..
1. Angewataarifu viongozi wake kwamba anataka kuondoka huku akiwapa muda Fulani mfano baada ya msimu kukamilika akatafute changamoto Mpya nje ya Yanga.....hii ingempa nafasi ya kuwa na uhusiano mzuri na klabu na pia viongozi haraka wangefikiria mbadala wake kikosini na isingeathiri muenendo wa timu...kiufupi hapa angekuwa amewaanda Yanga
2. Kuomba kujadiliana na Yanga auvunje/ aununue mkataba wake.....hapa wangezungumza na wangefikia muafaka hata Kama Yanga wangekataa ila ingemsaidia sana maana vitu vingekuwa documented na isingeonekana anashawishiwa,hapa Fei hata angevunja mkataba kungekuwa na prior information ambayo ingemfanya awe na reference ya kujitetea.
Hizo njia mbili naona zingemsaidia sana Fei huku akiwa na watu wanaomshauri vema nadhani suala lake lingemalizika bila misuguano sana.
NB: Fei ana nafasi ya kukata rufaa kuomba review ya maamuzi ya kamati ya TFF.....asiporidhika pia anaweza kwenda CAS. Ila pia ashauriwe vizuri maana baada ya maamuzi ya CAS hatakuwa na pa kwenda Kama maamuzi hayatakuwa upande wake Ila yakiwa upande wake kwangu Mimi na wengine wengi tutashuhudia mabadiliko makubwa katika sekta ya michezo hasa kwenye wachezaji kuvunja mikataba yao...
I stand to be corrected!
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Vijana wengi wadogo wanavutiwa na uwezo wake
Sasa nini kilimkuta Feisal mpaka haya yanayomtokea sasa hivi?
Feisali alipata ushauri kwa Nani au Ni utashi wake tu?
Nimemsikia wakili wake akisema hakushitikishwa katika kile wanachokiita kuvunja mkataba je hakuona umuhimu wa ushauri wa kisheria?
Baada ya kushindwa TFF je akienda FIFA akishindwa itakuwaje?
Mimi naona Kama Feisali alikuwa na room mzuri sana ya kuondoka Yanga bila mikwaruzano yeyote..
1. Angewataarifu viongozi wake kwamba anataka kuondoka huku akiwapa muda Fulani mfano baada ya msimu kukamilika akatafute changamoto Mpya nje ya Yanga.....hii ingempa nafasi ya kuwa na uhusiano mzuri na klabu na pia viongozi haraka wangefikiria mbadala wake kikosini na isingeathiri muenendo wa timu...kiufupi hapa angekuwa amewaanda Yanga
2. Kuomba kujadiliana na Yanga auvunje/ aununue mkataba wake.....hapa wangezungumza na wangefikia muafaka hata Kama Yanga wangekataa ila ingemsaidia sana maana vitu vingekuwa documented na isingeonekana anashawishiwa,hapa Fei hata angevunja mkataba kungekuwa na prior information ambayo ingemfanya awe na reference ya kujitetea.
Hizo njia mbili naona zingemsaidia sana Fei huku akiwa na watu wanaomshauri vema nadhani suala lake lingemalizika bila misuguano sana.
NB: Fei ana nafasi ya kukata rufaa kuomba review ya maamuzi ya kamati ya TFF.....asiporidhika pia anaweza kwenda CAS. Ila pia ashauriwe vizuri maana baada ya maamuzi ya CAS hatakuwa na pa kwenda Kama maamuzi hayatakuwa upande wake Ila yakiwa upande wake kwangu Mimi na wengine wengi tutashuhudia mabadiliko makubwa katika sekta ya michezo hasa kwenye wachezaji kuvunja mikataba yao...
I stand to be corrected!
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app