Yafuatayo ni mambo ya msingi kwa Yanga ili waweze kufuzu kesho

Yafuatayo ni mambo ya msingi kwa Yanga ili waweze kufuzu kesho

Smt016

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2016
Posts
3,012
Reaction score
4,300
Hapo awali nilileta uzi humu kuwa Yanga wanashindwa kufanya vizuri kwasababu wanakosa vinasaba vya michuano ya kimataifa. Nilipondwa sana na wana Yanga wenzangu lakini mpaka sasa akili zinawakaa sawa baada ya kuona Simba kwake kufuzu klabu bingwa imekuwa kama jambo la kawaida hata akiwa na kikosi cha kuunga unga.

Michuano ya kimataifa unapaswa uwe na mikakati pamoja na mipango ya kutosha kuanzia ndani mpaka nje ya uwanja. Lakini viongozi wa Yanga hakuna mwenye huo uzoefu wa kujua ni nini kinapaswa kifanyike na kwa wakati gani.

Kilichopo kwasasa ni kuiga tu kwa Simba kwa vile vitendo vilivyokuwa wazi lakini wanashindwa kukaa nao chini kuomba siri za vita ili na wao watoboe kama wenzao. Hili linawashinda kwasababu walishaleta ujuaji katika jambo wasilolijua.

Goli alilofunga Mayele ambalo lilikatiwa kuwa ni offside, lilipaswa kuwa ni goli. Kama likitokea goli kama lile limefungwa na Al Hilal huko Sudan basi hilo litahesabika kuwa goli halali kama japokuwa ni kweli ni offside.

Mambo haya kwenye mpira wa Africa yapo. Kule Africa kusini kulikuwa na VAR lakini Simba walilia na kusaga meno kwa maamuzi yaliyotokea. Hapa nawakumbusha viongozi wa Yanga muamke, mjifunze ni nini mnapaswa kufanya mnapocheza mchezo wa kimataifa.

Tuje kwenye mada yangu juu ya mechi ya kesho. Hii mechi imegawanyika katika makundi mawili ya utimamu

1) utimamu katika upande wa saikolojia ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi.
Wakienda kwa mawazo ya hujuma hujuma itawafanya watoke katika morali ya mchezo. Viongozi, wachezaji na benchi la ufundi wanatakiwa waonane na mtalamu wa saikolojia ili wajengwe kifikra na kiakili ili waiendee mechi kwa utulivu mkubwa sana bila kupaniki. Hiki kipengele ni kipengele muhimu mno kwa wachezaji na benchi la ufundi na ndiyo itakayotengeneza hali za wachezaji.

2) Mbinu na ufundi
Nabi akubali tu kuwa timu yake ya msimu huu imekuwa timu inayoruhusu magoli kirahisi mno na hii inatokana na sababu ya safu mbovu ya ulinzi. Jambo la kwanza upande wa kipa mpange Mshery badala ya Diarra. Pamoja na uokozi wake za mmoja dhidi ya mmoja lakini mara nyingi namuona kama hayupo mchezoni, una cross za kucheza hazichezi na ushapu hana. Tena ni kama vile mechi ya fainali ya Azam Confederation imefungua kufuli zake zote za uimara. Na pengine hana tena bahati kwasasa, Mshery achukue nafasi yake kwa mechi ya kesho.

Mpira wa sasa kucheza bila ya kiungo mkabaji halisia ni kuwachosha mabeki. Bangala arudishwe kwenye nafasi ya kiungo kwasababu Aucho sio mkabaji.

Mechi ya awali kocha alifanya kosa kubwa sana kiufundi kwa kutompanga Bangala kwenye kiungo mkabaji, na pia kumaliza silaha zako kwa pamoja na hakuna wa kubadilisha mchezo. Hivyo mechi ya kesho unapaswa kuwa vyema kwanza kwenye kiungo cha ukabaji, ili timu iweze kutulia hasa mabeki.

Mechi ya kesho Yanga wanahitaji utulivu wa akili, upangaji bora wa timu, na kutumia kila nafasi. Michuano ya kimataifa haitaji upate tano ili upate goli moja, bali kila nafasi unaipata kwako inatakiwa uitendee haki.

Mwisho namalizia kwa kusema kuwa Mayele anapaswa kuacha uroho na uchoyo wa kutaka kuzungumziwa yeye tu kwa kufunga bali anapokuwa eneo la goli ampe mchezaji mwenzio aliyepo katika eneo zuri zaidi la kukwasha mpira nyavuni.
 
Hawa ni Sikio La Kufa bro..... Hawashauriki..! Hlf Ushauri sasa hivi ndo umeshachelewa maana kichwa kimeshaelekezwa Kibra.

Ila sio mbaya wakichukua ushauri na kuufanyia kazi huko shirikisho watakakosukumiziwa..!
 
Hapo awali nilileta uzi humu kuwa Yanga wanashindwa kufanya vizuri kwasababu wanakosa vinasaba vya michuano ya kimataifa. Nilipondwa sana na wana Yanga wenzangu lakini mpaka sasa akili zinawakaa sawa baada ya kuona Simba kwake kufuzu klabu bingwa imekuwa kama jambo la kawaida hata akiwa na kikosi cha kuunga unga.

Michuano ya kimataifa unapaswa uwe na mikakati pamoja na mipango ya kutosha kuanzia ndani mpaka nje ya uwanja. Lakini viongozi wa Yanga hakuna mwenye huo uzoefu wa kujua ni nini kinapaswa kifanyike na kwa wakati gani.

Kilichopo kwasasa ni kuiga tu kwa Simba kwa vile vitendo vilivyokuwa wazi lakini wanashindwa kukaa nao chini kuomba siri za vita ili na wao watoboe kama wenzao. Hili linawashinda kwasababu walishaleta ujuaji katika jambo wasilolijua.

Goli alilofunga Mayele ambalo lilikatiwa kuwa ni offside, lilipaswa kuwa ni goli. Kama likitokea goli kama lile limefungwa na Al Hilal huko Sudan basi hilo litahesabika kuwa goli halali kama japokuwa ni kweli ni offside.

Mambo haya kwenye mpira wa Africa yapo. Kule Africa kusini kulikuwa na VAR lakini Simba walilia na kusaga meno kwa maamuzi yaliyotokea. Hapa nawakumbusha viongozi wa Yanga muamke, mjifunze ni nini mnapaswa kufanya mnapocheza mchezo wa kimataifa.

Tuje kwenye mada yangu juu ya mechi ya kesho. Hii mechi imegawanyika katika makundi mawili ya utimamu

1) utimamu katika upande wa saikolojia ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi.
Wakienda kwa mawazo ya hujuma hujuma itawafanya watoke katika morali ya mchezo. Viongozi, wachezaji na benchi la ufundi wanatakiwa waonane na mtalamu wa saikolojia ili wajengwe kifikra na kiakili ili waiendee mechi kwa utulivu mkubwa sana bila kupaniki. Hiki kipengele ni kipengele muhimu mno kwa wachezaji na benchi la ufundi na ndiyo itakayotengeneza hali za wachezaji.

2) Mbinu na ufundi
Nabi akubali tu kuwa timu yake ya msimu huu imekuwa timu inayoruhusu magoli kirahisi mno na hii inatokana na sababu ya safu mbovu ya ulinzi. Jambo la kwanza upande wa kipa mpange Mshery badala ya Diarra. Pamoja na uokozi wake za mmoja dhidi ya mmoja lakini mara nyingi namuona kama hayupo mchezoni, una cross za kucheza hazichezi na ushapu hana. Tena ni kama vile mechi ya fainali ya Azam Confederation imefungua kufuli zake zote za uimara. Na pengine hana tena bahati kwasasa, Mshery achukue nafasi yake kwa mechi ya kesho.

Mpira wa sasa kucheza bila ya kiungo mkabaji halisia ni kuwachosha mabeki. Bangala arudishwe kwenye nafasi ya kiungo kwasababu Aucho sio mkabaji.

Mechi ya awali kocha alifanya kosa kubwa sana kiufundi kwa kutompanga Bangala kwenye kiungo mkabaji, na pia kumaliza silaha zako kwa pamoja na hakuna wa kubadilisha mchezo. Hivyo mechi ya kesho unapaswa kuwa vyema kwanza kwenye kiungo cha ukabaji, ili timu iweze kutulia hasa mabeki.

Mechi ya kesho Yanga wanahitaji utulivu wa akili, upangaji bora wa timu, na kutumia kila nafasi. Michuano ya kimataifa haitaji upate tano ili upate goli moja, bali kila nafasi unaipata kwako inatakiwa uitendee haki.

Mwisho namalizia kwa kusema kuwa Mayele anapaswa kuacha uroho na uchoyo wa kutaka kuzungumziwa yeye tu kwa kufunga bali anapokuwa eneo la goli ampe mchezaji mwenzio aliyepo katika eneo zuri zaidi la kukwasha mpira nyavuni.
Hiyo namba 2 ina ukweli ndani yake kumhusu mlinda mlango wetu namba 1, ila ndiyo hivyo tena! Kesho ataanza yeye. Lakini pia Yannick Bangala ndiyo kiungo mkabaji pekee wa kueleweka! Sasa wanapo pangwa watu kama Aucho au Bigirimana kukaba, madhara yake ndiyo yale ya timu kuelemewa kule nyuma.

Binafsi hiyo kesho natarajia kulala mapema. Mtanipa matokeo keshokutwa iwapo tunaenda makundi, au tunaenda mtoano tena kombe la shirikisho.
 
Yanga wasithubutu kutumia mfumo wa 4-2-3-1 kwani wakiutumia Mayele atawekwa kisiwani na hatapata mipira na wachezaji wa Al Hilal wataenda mbele kushambulia lango la Yanga kwa muda mwingi sana.

Lkn wakitumia mfumo wa 4-4-2 itabidi timu ya Al Hilal iwe na fikra ya kujilinda zaidi hali ambayo itawafanya viungo wa Yanga wapate fursa ya kukaa na mpira na kutengeneza nafasi za kufunga.

Washambuliaji wa Yanga wawe na concentration kali sana na kamwe wasicheze na nafasi yoyote wanayopata kama Mayele afanyavyo mara nyingi na wakifanya hivyo lazima watayaaga mashindano rasmi.

Pia mlinda mlango Diarra ana tabia ya kuwa na kiwewe cha kutoka golini mara wanaposhambuliwa na kufuata mpira ambapo uwezekano wa kuukosa ni mkubwa na kusababisha goli.

Kocha Nabi asiwe na tabia ya kuchelewa kufanya substitution wakati ikionekana mambo yanaenda ndivyo sivyo, pia waepuke sana sana kupaki basi kwa hali yoyote ile.
 
Hiyo namba 2 ina ukweli ndani yake kumhusu mlinda mlango wetu namba 1, ila ndiyo hivyo tena! Kesho ataanza yeye. Lakini pia Yannick Bangala ndiyo kiungo mkabaji pekee wa kueleweka! Sasa wanapo pangwa watu kama Aucho au Bigirimana kukaba, madhara yake ndiyo yale ya timu kuelemewa kule nyuma.

Binafsi hiyo kesho natarajia kulala mapema. Mtanipa matokeo keshokutwa iwapo tunaenda makundi, au tunaenda mtoano tena kombe la shirikisho.
Inabidi kwanza tuone kikosi kitakachopangwa ndio tufanye maamuzi ya kulala au kuangalia mechi. Diarra ni kama vile kama amekuwa na gundu la kufungwa fungwa. Kocha bora ampange Mshery hata mimi nimejaribu kuangalia mechi za msimu huu sio Diarra yule aliyetamba kwa kucheza cross, u sharp, na timing nzuri. Lakini msimu huu kazubaa mno. Kuhusu Bangala kwakweli kocha hatutendei haki hata kama hatuna taaluma ya ukocha lakini kuna vitu viko wazi sana havihitaji uwe na leseni ya ukocha kuona. Yanga hakuna kiungo mkabaji kama Bangala. Tumepiga sana kelele msimu huu kuhusu Bangala kucheza kama mkata umeme lakini yeye aona kama wakina Aucho wanaweza kukaba. Yaank dah

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Nabi chezesha 4-3-3
Beki: Djuma, Dickson, Mwamnyeto, Lomalisa
Kiungo: Bangala, Aucho, Feitoto
Mbele: Falid, Mayele, Kisinda

Benchi: Morrison, Aziz Ki, Moloko, Sure Boy, Kibwana,

Waliopo benchi wanaweza kuingia na kubadilisha mchezo badala ya kufanya makosa ya mechi ya kwanza ya kuingiza silaha zote kipindi cha kwanza
 
Nabi chezesha 4-3-3
Beki: Djuma, Dickson, Mwamnyeto, Lomalisa
Kiungo: Bangala, Aucho, Feitoto
Mbele: Falid, Mayele, Kisinda

Benchi: Morrison, Aziz Ki, Moloko, Sure Boy, Kibwana,

Waliopo benchi wanaweza kuingia na kubadilisha mchezo badala ya kufanya makosa ya mechi ya kwanza ya kuingiza silaha zote kipindi cha kwanza
Kisinda kabaki jina tu. Haiwezi hiyo mechi

Sent from my Redmi Note 9 Pro using JamiiForums mobile app
 
Kesho mikeka yangu miwili itakua hivi.
[emoji116]
1.direct win Al hilal.
1.direct win Simba.
fillet 50k.

Al hilal Vs Uto over 1.5
Simba Vs De Agosto 1.5
fillet 50k.
navaa msuli wangu na kibaghalishia cha kisudan naagiza supu ya mkia wa bata nasubiri mpunga uingie.
 
Hiyo namba 2 ina ukweli ndani yake kumhusu mlinda mlango wetu namba 1, ila ndiyo hivyo tena! Kesho ataanza yeye. Lakini pia Yannick Bangala ndiyo kiungo mkabaji pekee wa kueleweka! Sasa wanapo pangwa watu kama Aucho au Bigirimana kukaba, madhara yake ndiyo yale ya timu kuelemewa kule nyuma.

Binafsi hiyo kesho natarajia kulala mapema. Mtanipa matokeo keshokutwa iwapo tunaenda makundi, au tunaenda mtoano tena kombe la shirikisho.
Natumai hautakuja kuleta visingizio vya safari kama ile mechi iliyopita.
 
Yanga wasithubutu kutumia mfumo wa 4-2-3-1 kwani wakiutumia Mayele atawekwa kisiwani na hatapata mipira na wachezaji wa Al Hilal wataenda mbele kushambulia lango la Yanga kwa muda mwingi sana.

Lkn wakitumia mfumo wa 4-4-2 itabidi timu ya Al Hilal iwe na fikra ya kujilinda zaidi hali ambayo itawafanya viungo wa Yanga wapate fursa ya kukaa na mpira na kutengeneza nafasi za kufunga.

Washambuliaji wa Yanga wawe na concentration kali sana na kamwe wasicheze na nafasi yoyote wanayopata kama Mayele afanyavyo mara nyingi na wakifanya hivyo lazima watayaaga mashindano rasmi.

Pia mlinda mlango Diarra ana tabia ya kuwa na kiwewe cha kutoka golini mara wanaposhambuliwa na kufuata mpira ambapo uwezekano wa kuukosa ni mkubwa na kusababisha goli.

Kocha Nabi asiwe na tabia ya kuchelewa kufanya substitution wakati ikionekana mambo yanaenda ndivyo sivyo, pia waepuke sana sana kupaki basi kwa hali yoyote ile.
Angalau sasa mmeanza kuuona ubovu wa chama lenu
 
Hapo awali nilileta uzi humu kuwa Yanga wanashindwa kufanya vizuri kwasababu wanakosa vinasaba vya michuan

Goli alilofunga Mayele ambalo lilikatiwa kuwa ni offside, lilipaswa kuwa ni goli. Kama likitokea goli kama lile limefungwa na Al Hilal huko Sudan basi hilo litahesabika kuwa goli halali kama japokuwa ni kweli

Mambo haya kwenye mpira wa Africa yapo. Kule Africa kusini kulikuwa na VAR lakini Simba walilia na kusaga meno kwa maamuzi yaliyotokea. Hapa nawakumbusha viongozi wa Yanga muamke, mjifunze ni nini mnapaswa kufanya mnapocheza mchezo wa kimataifa.
pole sana kwa haya mawazo hasi... ndugu yale magoli waliyofungwa azam katika shirikisho na ile team ya libya Al khadar uliyaona..??? al khadar alikuwa home na goli 2 zilikataliwa.... vip na wenyewe waje wajifunze mbinu kwa simba..?? kuwa kwanini goli zao mbili zilikataliwa.. vipi kuhusu De agosto goli lao lililo kataliwa uliliona au ulifumba macho..? ukaona goli la mayele tu lililokataliwa..

usiishi kwa kukalili soka la zamani kwa marefa kuzibeba kijinga tem za home.. kwa sasa marefa wa CAF hawana huo ujinga... funga goli la halali litahesabika na sio janja janja..
 
Natumai hautakuja kuleta visingizio vya safari kama ile mechi iliyopita.
Kesho nategemea kulala saa 2 tu usiku. Maana niko Kijijini kwa sasa, na uwezekano wa kwenda kibanda umiza ni mdogo.

Wangekuwa wanacheza mapema, ningeenda kuwaangalia.
 
Yanga wasithubutu kutumia mfumo wa 4-2-3-1 kwani wakiutumia Mayele atawekwa kisiwani na hatapata mipira na wachezaji wa Al Hilal wataenda mbele kushambulia lango la Yanga kwa muda mwingi sana.

Lkn wakitumia mfumo wa 4-4-2 itabidi timu ya Al Hilal iwe na fikra ya kujilinda zaidi hali ambayo itawafanya viungo wa Yanga wapate fursa ya kukaa na mpira na kutengeneza nafasi za kufunga.

Washambuliaji wa Yanga wawe na concentration kali sana na kamwe wasicheze na nafasi yoyote wanayopata kama Mayele afanyavyo mara nyingi na wakifanya hivyo lazima watayaaga mashindano rasmi.

Pia mlinda mlango Diarra ana tabia ya kuwa na kiwewe cha kutoka golini mara wanaposhambuliwa na kufuata mpira ambapo uwezekano wa kuukosa ni mkubwa na kusababisha goli.

Kocha Nabi asiwe na tabia ya kuchelewa kufanya substitution wakati ikionekana mambo yanaenda ndivyo sivyo, pia waepuke sana sana kupaki basi kwa hali yoyote ile.
Makocha wa online ukipewa hata timu ya ndondo chali
 
pole sana kwa haya mawazo hasi... ndugu yale magoli waliyofungwa azam katika shirikisho na ile team ya libya Al khadar uliyaona..??? al khadar alikuwa home na goli 2 zilikataliwa.... vip na wenyewe waje wajifunze mbinu kwa simba..?? kuwa kwanini goli zao mbili zilikataliwa.. vipi kuhusu De agosto goli lao lililo kataliwa uliliona au ulifumba macho..? ukaona goli la mayele tu lililokataliwa..

usiishi kwa kukalili soka la zamani kwa marefa kuzibeba kijinga tem za home.. kwa sasa marefa wa CAF hawana huo ujinga... funga goli la halali litahesabika na sio janja janja..
Marefa sasa hivi wapo fair nmeangalia mechi ya Mazembe na Vipers ni kwamba Yanga wakiwa wazuri uwanjani game bado mbichi hii
 
Hahaaaa!!!!yaan kujitia ujasiri wote hapa jukwaani,kumbe muoga hvyo????
Hiyo namba 2 ina ukweli ndani yake kumhusu mlinda mlango wetu namba 1, ila ndiyo hivyo tena! Kesho ataanza yeye. Lakini pia Yannick Bangala ndiyo kiungo mkabaji pekee wa kueleweka! Sasa wanapo pangwa watu kama Aucho au Bigirimana kukaba, madhara yake ndiyo yale ya timu kuelemewa kule nyuma.

Binafsi hiyo kesho natarajia kulala mapema. Mtanipa matokeo keshokutwa iwapo tunaenda makundi, au tunaenda mtoano tena kombe la shirikisho.
 
Back
Top Bottom