Yajue Makabila Yanayopatikana Tanzania Visiwani ( Zanzibar )

Yajue Makabila Yanayopatikana Tanzania Visiwani ( Zanzibar )

MKURABITA

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2010
Posts
317
Reaction score
126
Wadau,

Naomba mnisaidie hili swala, Hivi Zanzibar kuna makabila kama ilivyo Bara? Na kama yapo ni mangapi.?

Kuhusu Lugha Ukanda wa Pwani.

Unaposema kabila katika uwanda wa mwambao wa pwani lugha halisi ni kiswahili lakini tofauti ni lahaja kwa unguja kuna kiunguja,kihadimu,kipemba bara huku kuna kimtangata, kimrima, kiamu nk. Kuna wengi suala la mabila hasa ya wenyeji wa mwambao hawaelewi pengine maelezo yafuatayo yatatoa mwanga:-

Swahili ni Taifa la makabila yaliopo katika Pwani ya Afrika ya Mashariki na visiwa vyake tokea Barawa hadi Sofala. Baadhi ya makabila hayo ni Wabarawa, Wapate, Waamu, Wagiriama, Wadigo, Waduruma, Wakauma, Wakambe, Wachoni, Warabai, Waribe, Wajibana, Wakilindini, Wajomvu, Wamtwapa, Wachangamwe, Watangana, Wamvita, Wapokomo, Wavanga, Wamakunduchi, Wapemba na Wangazija. Kabila hizi zote zilikuwa zikizungumza lugha ilokuwa ikijulikana kama Kingozi. Hata hivyo, makabila yote haya yalikuwa na ndimi (dialect) zao na miji yao; baadhi yao bado wangali na ndimi zao na miji yao. Ndimi zote hizi zina ukhusiano au ukuruba mkubwa wa maneno na maana zake. Kwa mfano, utakuta kwamba kuna ukuruba fulani baina ya Kipemba na Kiamu.

Kila kabila ina ndimi yake, dasturi zake, mila zake, tungo zake, na kadhalika. Haya yote ni kabla ya Waarabu na Washirazi hawajaanza kuhamia kimaisha katika Pwani ya Afrika ya Mashariki - takriba karne nane hadi kumi zilizopita (yaani baina ya miaka 800 hadi 1000).

Washirazi hawakuathiri mno mila, dasturi, mapisi, na lugha hiyo ya Watu wa Pwani. Waarabu ndiyo walioathiri sana, khususa Makabila ya Kati na Kati (kwa mfano, Wamvita, Watangana na Wakilindini). Makabila haya yaliathirika mno hadi ya kuwa majina haya yalipotea na ndimi zao za kiasili zilipotea vilevile. Ndimi ambazo bado zipo ingawa zimeazima maneno fulani ya Kiarabu (kama ambavyo pengine Kiarabu kimeazima kutoka Lugha ya Kingozi) ni ndimi za kaskazini na zile za kusini.

Ndimi za Kaskazini ambazo bado zipo na wenyewe wanatambuliwa ni kama vile Kibarawa, Kiamu, Kipokomo, na kadhalika. Ama Ndimi za Kusini ambazo hazikuathiriwa mno ni Kingazija, Kimakunduchi, Kipemba na Kivanga. Ndimi za Kati na Kati ambazo bado zikalipo ni kama vile, Kigiriama, Kiduruma, Kijibana; hizi ni miongoni mwa kabila ambazo leo zajiita au zatambuliwa kama Mijikenda (yaani miji tisia).

Utakuta ya kuwa katika makabila ya kati na kati, yale ambayo hayakuathiriwa sana ni yale ambamo watu wake hawakuwa Waislamu. Na ndiyo maana mpaka hii leo utaona ya kuwa makabila ya Mijikenda (isipokuwa Digo), ni makabila ambayo wengi katika watu wake si Waislamu. Hii ni kwa sababu makabila kama ya Mvita, Tangana na Changamwe hayakujitahidi au kujishughulisha kufanya usambazaji wa Risala ya U-Islam kwa makabila haya; Waarabu piya walipokuja hawakuwa na lengo hilo la kuingia vijijini kufanya Da'wah. Lengo lao kubwa ilikuwa ni biashara. Kama tujuavyo U-Islam ulifika Kaskazini Mashariki mwa Bara la Afrika kabla haujafika katika sehemu nyengine za bara Arabu kama vile, Yemen, Omani na hata katika mji wa Madina na sehemu nyingi za nchi tunayoijua leo kama Saudi Arabia. Yaani U-Islam ulifika Abisinia (Ethiopia ya leo) katika mwaka wa 615, miaka mitano tu baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.) kupewa risala (610). Mtume alizaliwa mwaka wa 570. Ingawa wale Waislamu waliokuja kuomba hifadhi Abisinia walikwenda zao Madina baada ya kutawazwa kwa serikali ya kwanza ya Islam mwaka wa 623 (huu ni mwaka wa kwanza wa Hijria), walikuwa washawasilimisha watu kadha wa kadha (akiwemo Mfalme wao, Najash); hii ndiyo ilikuwa ni sababu ya kuanza kusambaa kwa U-Islam katika bara la Afrika. Kwa hivyo ni muhimu kutambua na kuamini ya kuwa makabila fulani ya Afrika ya Mashariki yalisilimu kabla ya kuja kwa Waarabu hawa tuwajuwao leo, waliokuja kwa biashara katika pwani ya Afrika ya Mashariki kutoka Yemen, Omani, na kadhalika.

Na khususa ni Waarabu hao wa Yemen na Omani ndiyo waloowana na baadhi ya hao Wangozi, au wanaojulikana leo kama Waswahili. Kwa hivyo, baadhi ya Waswahili wana damu za Kiarabu na baadhi yao hawana damu ya Kiarabu. Katika dasturi za Kizungu za kufuata ukoo, mtu anapotanganya tu damu na asekuwa Mzungu, basi azaliwae katika mtanganyiko huo katu hakubaliwi kuwa ni Mzungu. Na ndiyo twaona ya kuwa ingawa kuna asili mia thalathini (30%) ya Wamarekani Weuse (African-Americans) ndani ya Marekani, lakini wanasibishwa na U-Afrika na U-weuse (Blacks) pekee, na katu hawanasibishwi na uzungu. Kwa Waarabu nao ni rahisi zaidi kunasibishwa na taifa hilo ikiwa mtu lugha yake ya kwanza ni Kiarabu. Ama kwa Waswahili tukati na kati, yaani aghlabu mtu hunasibishwa na Uswahili kwa lugha na asili. Kwa hivyo leo wako baadhi ya Waswahili wenye damu za Kiarabu ambao wametagua, kwa sababu mbalimbali, kujinasibisha zaidi na U-Arabu kuliko U-Afrika; kadhalika, kuna baadhi yao, kwa sababu moja au nyengine, wameamua kujinasibisha zaidi na U-Afrika kuliko U-Arabu.

Hakuna yoyote atakayekataa ya kuwa neno Swahili au Sawahel ni neno lenye asili ya Kiarabu, ambalo lina maana ya Pwani au Mwambao. Kwa hivyo, ni wazi kabisa kuwa jina au neno Swahili halikuapo kabla ya kuja kwa Waarabu. Hivyo basi, wema mmoja ambao Waarabu waliwafanyia wenyeji wa Mwambao wa Afrika ya Mashariki na visiwa vyake ni kuwabandikiza neno lililoanza kutumika kama jina la taifa la wenyeji hao, litambulikanalo leo hii kama Taifa La wa-Swahili, yaani Taifa La wa-Mwambao. Watu wa taifa hili ni Waswahili, yaani Wamwambao, au kwa jina la kiasili, Wangozi. Na hapo pao napo paitwa Uswahilini. Na mila na dasturi zao ndiyo Uswahili. Na lugha ya watu hawa ni Kiswahili. Ni lugha ambayo maneno yake zaidi yatokamana na ndimi za makabila ya kati - kama vile Kimvita, Kichangamwe na Kitangana; halafu ikatukua na maneno ya Kiamu, Kivanga, Kipemba, Kingazija, Kibarawa, Kigiriama, na kadhalika. Kwa hivyo, Kiswahili ni kile kile Kingozi, tofauti ni jina tu; timbuko lake ni mtanganyiko wa ndimi za makabila ya Pwani. Piya kuna maneno ya Kiarabu, Kishirazi, Kiingereza, Kireno, na lugha za bara ya Afrika ya Mashariki. Kiswahili kimeazima maneno ya lugha nyegine kama ambavyo lugha zote zimefanya hivyo. Wao na Wahindi piya wameazimiana katika Upishi. Yayumkinika kuwa katika Kireno, Kiarabu na lugha nyenginezo kuna maneno ya Kimvita, Kijomvu, Kiamu, na kadhalika. Hili ni suala ambalo halihitaji mjadala mkubwa kwani liko waziwazi. Ikiwa baba Adamu (a.s.) na mama Hawaa walizungumza lugha moja kwa nini leo tuwe na lugha, makabila na mataifa tungu nzima? Tazama katika Quraani [Al-Hujuraat aya 13 na Ar-Rum aya 22].

Kwa mfano ukiangalia namna mataifa ya Arabu na Yahudi yalivyoanza utaona ya kuwa ni kama mtezo. Historia na dini yatueleza kuwa Mayahudi na Waarabu wanatokamana na Mtume Yaaqub (a.s.) na Mtume Ismael (a.s.). Ikiwa hii ni kweli, kwa nini iwe hivi na wote wawili wanatokana na Mtume Ibrahim (a.s.) ambae taifa lake hatulijui wala hatukuelezwa. Kwa nini wajukuu, vitukuu, vilembwe, na vilembwekeza vya Nabii Ibrahim wawe na taifa tofauti na yeye? Tena tofauti yenyewe si ya taifa moja bali mataifa mawili, angalau!

Mwana Ismael azae Waarabu na mjukuu Yaaqub (mtoto wa Is-haka) azae Mayahudi. Hii yote hapa ni kuwa tunajaribu kuonyesha ya kuwa kunahitajika sababu ndogo mno (pengine hata isiyoingia akilini mwetu) kuzaliwa kwa taifa jipya au kabila mpya. Lakini hii ni kazi ya Allah (s.w.t.) kama aya za hapo juu zinavyoonyesha. Halafu isitoshe, baada ya kuzaliwa kwa Taifa la Arabu, kukaanza Makabila kama vile Qureish, Aws, Khazraj, na kadhalika. Bado haijatosha, kukazaliwa Koo mbali mbali, kama vile kwenye kabila ya Qureish kuna koo kama Umayya, Makhzum, Alawi, Hashim na kadhalika. Ikiwa haya yote yawezekana, kwa nini visiwezekani kuapo kwa taifa la Swahili na makabila kama vile Mvita, Ngazija, Giriama, na Makunduchi? Au kwa nini kusiwe na koo kama vile Mwinjaa, Wanyali, Wamuyaka, na kadhalika?

Hii leo ni jambo gani linalomuunganisha Muarabu kutoka Sudan na yule wa kutoka Lebanon na yule wa kutoka Hijaz? Sio dini, wala rangi, wala nywele, wala tabia, wala mapishi! Huenda moja au zaidi ya mambo haya yakafanana, lakini jambo kubwa linalowafanya wote wakaitwa Waarabu ni Lugha, na labuda Asili. Labuda na Mayahudi ni vile vile, mtukue Yahudi wa Palestine, na yule wa Habashi na yule wa Urusi; kitu kitakacho waunganisha ni Asili, na pengine lugha na dini.

Kwa hivyo Swahili ni taifa ambalo lipo, na lenye makabila yasiopungua kumi na tano, tokea mji wa Barawa (kaskazini) mpaka mji wa Sofala (kusini). Ni taifa ambalo makabila yake yametapakaa katika nchi sita: Somalia, Kenya, Tanganyika, Zanzibar, Ngazija (Comoro Islands), na Msumbiji (Mozambique). Kwa hiyo, nasema tena ya kuwa Swahili ni Taifa. Ni muhimu kufahamu ya kuwa mtu anaposema kuwa yeye ni Mswahili haimaanishi kuwa kabila yake ni Swahili bali ni kuwa anatokamana na Taifa La Waswahili. Na kitu kinachowaunganisha watu katika taifa hili ni: Asili na Lugha.

 
Kitabu cha historia cha zamani cha darasa la tano, historia ya jamii za waafrika hadi mwaka 1880, kiasema zenji kulikuwa kuna makabila ya wahadimu, watumbatu ,wamvita na jingine nimelisahau, ila wazenji wengine wanakataa wanadai haya si makabila ila ni jamii tu.

Kumbuka waafrika wa asili waliokuwa zanzibar miaka mingi nahisi walichukuliwa utumwani wakauzwa arabuni au elsewhere na wale walioko kule ni wale watumwa waliopelekwa kule kufanya kazi kwenye mashamba ya mikarafuu na minazi ili kuwa wakwezi na kutengeneza mbata (labda ndio maana weusi wengi kule wana asili ya unyamwezi) au watu walioenda zanzibar kutafuta maisha(mfano abeid karume inadaiwa alitoka malawi).

Istand to be corrected
 
Wadau, naomba mnisaidie. Hivi Zanzibar kuna makabila kama ilivyo Bara? kama wachaga, wahaya, jaruo, wakwere n.k. Na kama yapo ni mangapi.

Nadhani yapo sabab kuna lahaja toafuti za kiswahili zinazungumzwa hata ndani ya zenj. hizo lahaja za kiswahili zinaweza kuchukuliwa kama makabila.
 
kitabu cha historia cha zamani cha darasa la tano, historia ya jamii za waafrika hadi mwaka 1880, kiasema zenji kulikuwa kuna makabila ya wahadimu, watumbatu ,wamvita na jingine nimelisahau, ila wazenji wengine wanakataa wanadai haya si makabila ila ni jamii tu

kumbuka waafrika wa asili waliokuwa zanzibar miaka mingi nahisi walichukuliwa utumwani wakauzwa arabuni au elsewhere na wale walioko kule ni wale watumwa waliopelekwa kule kufanya kazi kwenye mashamba ya mikarafuu na minazi ili kuwa wakwezi na kutengeneza mbata (labda ndio maana weusi wengi kule wana asili ya unyamwezi) au watu walioenda zanzibar kutafuta maisha(mfano abeid karume inadaiwa alitoka malawi),

i stand to be corrected

Kwa hiyo kimsingi Zanzibar ilikuwa shamba la karafuu. Sasa hili shamba la karafuu linawezaje kuwa na makabila?

Mkuu wa shamba hili la karafuu sasa hivi anaitwa Daktari Shein. Msaidizi wake wa karibu au katibu muhtasi anaitwa Sefu Sharifa Hamadi.
 
Zanzibar hakuna makabila kuna Watu wanaotoka Kisiwa cha Unguja na kisiwa cha Pemba na Wenyewe wanajuwana kwa Lugha ya Kiswahili chao wanachozungumza Mtu wa Unguja ndie anayezungumza Kiswahili Fasaha kuliko Mtu kutoka kisiwa cha pemba wenyewe kwa

wenyewe hutaniana, kwa kusema wewe watoka Pemba mimi natoka unguja. au Wewe ni mpemba na mimi ni Muunguja hakuna kitu kabila. Ila kulikuwa na Waarabu walioleta Biashara

ya utumwa kuwachukuwa watu kutoka Tanganyika kuwaleta Visiwani Pemba na Unguja na baadhi yao ndio hao waliokuwepo mpaka hivi sasa wengi wa Watu wanaotoka Visiwa vya Unguja na Pemba wanatoka huku Tanzania bara.
 
jamani mbona nasikia 'waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba?' hakuna waarabu huko, au uarabu si kabila?
 
Kwikwikwi.

Kutoka na research zangu yapo makabila. Neno kabila ni neno lilokopwa kutoka kwenye kiarabu (family group characterised by a common family name). Hivyo basi watu kuzungumza lugha moja haina maana kuwa hakuna makabila. Ukoo unaotumia jina moja unatosha kuunda kabila.

Maisha ya waAfrika yalikuwa yapo kwenye ukoo. Lakini upangaji wa makabila ya sasa yametokana na ujio wa wakoloni. Wakoloni walikusanya watu wenye kuzungumza lugha moja na kuita kabila. Lakini hivyo sisi wenyewe tulivyojigawa.

Kwa mfano kabila la wahaya lilianzishwa na wakoloni. Lakini ndani ya wahaya kuna wa Kanyigo, kuna wanyambo n.k

Kule Nigeria kuna waIbo. Lakini hili halikuwa kabila moja mpaka wakoloni walipogawa watu kwa kutumia lugha.

Sasa ukija pwani ya Afrika mashariki, tayari kulikuwa na city-states. Katika city-states hizi tayari watu walikuwa wanaishi kwa koo zao na kutumia kiswahili.

Wakati wagiriki wanatembelea Azania, zaidi ya miaka 2000 iliyopita tayari city states hizi zilikuwepo na watu walikuwa wanazungumza kiswahili. Hivyo si kweli nadharia mnazozitoa hapa.

Katika kitabu chake cha Isimu ya Lugha, Father Nkwera anasema kuwa wakati Ibn Batuta anatembelea East Africa alikuta watu wanalonga kiswahili.

Na ni mkoloni aliyechagua kiswahili cha unguja kuwa ni standard swahili. Na hii ndio sababu mtu wa unguja anaona kuwa kiswahili chake ni bora. Lakini hakuna ubora wowote ule kwa sababu kiswahili kilichozungumzwa katika city-state zingine zilikuwa ni lugha kamili katika states hizo.
 
Kwikwikwi.

Kutoka na research zangu yapo makabila. Neno kabila ni neno lilokopwa kutoka kwenye kiarabu (family group characterised by a common family name). Hivyo basi watu kuzungumza lugha moja haina maana kuwa hakuna makabila. Ukoo unaotumia jina moja unatosha kuunda kabila.

Maisha ya waAfrika yalikuwa yapo kwenye ukoo. Lakini upangaji wa makabila ya sasa yametokana na ujio wa wakoloni. Wakoloni walikusanya watu wenye kuzungumza lugha moja na kuita kabila. Lakini hivyo sisi wenyewe tulivyojigawa.

Kwa mfano kabila la wahaya lilianzishwa na wakoloni. Lakini ndani ya wahaya kuna wa Kanyigo, kuna wanyambo n.k

Kule Nigeria kuna waIbo. Lakini hili halikuwa kabila moja mpaka wakoloni walipogawa watu kwa kutumia lugha.

Sasa ukija pwani ya Afrika mashariki, tayari kulikuwa na city-states. Katika city-states hizi tayari watu walikuwa wanaishi kwa koo zao na kutumia kiswahili.

Wakati wagiriki wanatembelea Azania, zaidi ya miaka 2000 iliyopita tayari city states hizi zilikuwepo na watu walikuwa wanazungumza kiswahili. Hivyo si kweli nadharia mnazozitoa hapa.

Katika kitabu chake cha Isimu ya Lugha, Father Nkwera anasema kuwa wakati Ibn Batuta anatembelea East Africa alikuta watu wanalonga kiswahili.

Na ni mkoloni aliyechagua kiswahili cha unguja kuwa ni standard swahili. Na hii ndio sababu mtu wa unguja anaona kuwa kiswahili chake ni bora. Lakini hakuna ubora wowote ule kwa sababu kiswahili kilichozungumzwa katika city-state zingine zilikuwa ni lugha kamili katika states hizo.

Nashukuru sana wadau kwa michango yenu nimepata kuelimika.
 
Jamani Zanzibar kuna makabila wahamiaji kama Waluguru, Wachaga., Sukuma,NYamwezi, Watumbatu, Wapare nimeshuhudia Demu wangu yeye ni Mchaga lakini tokea enzi zile baba mzaa babu yake alizaliwa kule na sasa wao ukiwaona ni Zanzibar piwa lakini ukimchimba anakwambia yeye ni mchaga ila hapajui Kilimanjaro na kabisa na majina ya Ukoo hawatumii kwahiyo kwa urahisi uwezi kumjua mpaka umchimbe. WE NEED CHANGES :A S angry:
 
Wadau, naomba mnisaidie. Hivi Zanzibar kuna makabila kama ilivyo Bara? kama wachaga, wahaya, jaruo, wakwere n.k. Na kama yapo ni mangapi.


Kwikwikwi.

Kutoka na research zangu yapo makabila. Neno kabila ni neno lilokopwa kutoka kwenye kiarabu (family group characterised by a common family name). Hivyo basi watu kuzungumza lugha moja haina maana kuwa hakuna makabila. Ukoo unaotumia jina moja unatosha kuunda kabila.

Maisha ya waAfrika yalikuwa yapo kwenye ukoo. Lakini upangaji wa makabila ya sasa yametokana na ujio wa wakoloni. Wakoloni walikusanya watu wenye kuzungumza lugha moja na kuita kabila. Lakini hivyo sisi wenyewe tulivyojigawa.

Kwa mfano kabila la wahaya lilianzishwa na wakoloni. Lakini ndani ya wahaya kuna wa Kanyigo, kuna wanyambo n.k

Kule Nigeria kuna waIbo. Lakini hili halikuwa kabila moja mpaka wakoloni walipogawa watu kwa kutumia lugha.

Sasa ukija pwani ya Afrika mashariki, tayari kulikuwa na city-states. Katika city-states hizi tayari watu walikuwa wanaishi kwa koo zao na kutumia kiswahili.

Wakati wagiriki wanatembelea Azania, zaidi ya miaka 2000 iliyopita tayari city states hizi zilikuwepo na watu walikuwa wanazungumza kiswahili. Hivyo si kweli nadharia mnazozitoa hapa.

Katika kitabu chake cha Isimu ya Lugha, Father Nkwera anasema kuwa wakati Ibn Batuta anatembelea East Africa alikuta watu wanalonga kiswahili.

Na ni mkoloni aliyechagua kiswahili cha unguja kuwa ni standard swahili. Na hii ndio sababu mtu wa unguja anaona kuwa kiswahili chake ni bora. Lakini hakuna ubora wowote ule kwa sababu kiswahili kilichozungumzwa katika city-state zingine zilikuwa ni lugha kamili katika states hizo.

Mkuu Zakumi, maelezo yako kwa swali la Mkurabita yanatia mwangaza kwenye swala zima la historia ya Kiswahili chetu na makabila. Lakini hata hivyo naona maelezo yako yanakwepesha swala la msingi ndani ya swali lake, kama jinsi nilivyolielewa mimi na baadhi ya wachangiaji wengine hapo juu.

Mkurabita ameuliza na kutolea mfano utofauti wa kikabila pragmatically, kama vile Wachaga, Wahaya, Wajaruo na Wakwere. Basi kwa jinsi nilivyomuelewa mimi anachotaka kujua ni lugha zipi hizo (mimi sizifahamu) mbali na lahaja au lafudhi mbalimbali za Kiswahili zilizopo Zanzibar na Tanzania Bara (kama zipo au zilikuwepo huko Zanzibar). Tukumbuke kwamba regional accents zipo kila pahala duniani. Akina Bush wa Texas hawana lafudhi sawa na kina Palin huko Alaska, vivyo hivyo watu wa NY wanaongea tofauti na watu wa Miami. Ma-scouser wa Liverpool ni tofauti na ma-cockney wa London, Waspanish wa Madrid nitofauti kabisa na waongeao kihispania kule Venezuela n.k. Hizi ni variations au lahaja za lugha na zinatokana na mkusanyiko wa koo mbalimbali zenye kutumia lugha hiyo. Hivyo maelezo yako kwa jinsi nilivyoyaelewa mimi yamejikita katika kuelezea asili na tofauti hizi katika Kiswahili. Wakati swali la Mkurabita nikutaka kujua uwepo wa lugha nyinginezo za Kibantu (au asili nyingine) mbali na Kiswahili. Lakini kwasabau Kiswahili nayo ni lugha, na kama ndiyo pekee iliyokuwepo/iliyopo Zanzibar, basi uniwie radhi maana maelezo yako yanatosheleza kabisa, yakwamba lugha hiyo huko Zanzibar ni Kiswahili (ila kwa koo tofauti tofauti na lahaja tofauti tofauti).

Swala jingine, nakubaliana nawe kuwe maisha ya Waafrika yalikuwa yapo kwenye koo.Si hivyo tu, bali mpaka sasa koo nyingi bado zinaendelea kuwepo. Mkuu ningelipenda utoe maelezo pale unaposema kuwa upangaji wa makabila uliopo sasa hivi umetokana na ujio wa wakoloni. Je, unataka kutueleza kuwa kabla ya wakoloni kuja, koo hizi unazosisema zilikuwa zimetapakaa huku na kule kila pahala ila wakoloni ndiyo walizikusanya? Mfano, baadhi ya Wahaya na Wasukuma bila kujali chimbuko lao walikuwa Pwani na Nyanda za kusini na wengine kanda za maziwa makuu, ila wakoloni ndiyo waliwakusanya na kuwaweka pamoja wote kanda za ziwa Victoria? (kama mfano). Na si kwamba, hizi koo zinazoongea lugha moja na kuelewana (achilia mbali Kiswahili) zilikuwa zimejikusanya kanda mbalimbali kwa common interest kabla ya hata hao wakoloni kuja?!

Vinginevyo, nashukuru kwa mwangaza wa maelezo yako hapo juu.

Steve Dii
 
Mkuu Zakumi, maelezo yako kwa swali la Mkurabita yanatia mwangaza kwenye swala zima la historia ya Kiswahili chetu na makabila. Lakini hata hivyo naona maelezo yako yanakwepesha swala la msingi ndani ya swali lake, kama jinsi nilivyolielewa mimi na baadhi ya wachangiaji wengine hapo juu.

Mkurabita ameuliza na kutolea mfano utofauti wa kikabila pragmatically, kama vile Wachaga, Wahaya, Wajaruo na Wakwere. Basi kwa jinsi nilivyomuelewa mimi anachotaka kujua ni lugha zipi hizo (mimi sizifahamu) mbali na lahaja au lafudhi mbalimbali za Kiswahili zilizopo Zanzibar na Tanzania Bara (kama zipo au zilikuwepo huko Zanzibar). Tukumbuke kwamba regional accents zipo kila pahala duniani. Akina Bush wa Texas hawana lafudhi sawa na kina Palin huko Alaska, vivyo hivyo watu wa NY wanaongea tofauti na watu wa Miami. Ma-scouser wa Liverpool ni tofauti na ma-cockney wa London, Waspanish wa Madrid nitofauti kabisa na waongeao kihispania kule Venezuela n.k. Hizi ni variations au lahaja za lugha na zinatokana na mkusanyiko wa koo mbalimbali zenye kutumia lugha hiyo. Hivyo maelezo yako kwa jinsi nilivyoyaelewa mimi yamejikita katika kuelezea asili na tofauti hizi katika Kiswahili. Wakati swali la Mkurabita nikutaka kujua uwepo wa lugha nyinginezo za Kibantu (au asili nyingine) mbali na Kiswahili. Lakini kwasabau Kiswahili nayo ni lugha, na kama ndiyo pekee iliyokuwepo/iliyopo Zanzibar, basi uniwie radhi maana maelezo yako yanatosheleza kabisa, yakwamba lugha hiyo huko Zanzibar ni Kiswahili (ila kwa koo tofauti tofauti na lahaja tofauti tofauti).

Swala jingine, nakubaliana nawe kuwe maisha ya Waafrika yalikuwa yapo kwenye koo.Si hivyo tu, bali mpaka sasa koo nyingi bado zinaendelea kuwepo. Mkuu ningelipenda utoe maelezo pale unaposema kuwa upangaji wa makabila uliopo sasa hivi umetokana na ujio wa wakoloni. Je, unataka kutueleza kuwa kabla ya wakoloni kuja, koo hizi unazosisema zilikuwa zimetapakaa huku na kule kila pahala ila wakoloni ndiyo walizikusanya? Mfano, baadhi ya Wahaya na Wasukuma bila kujali chimbuko lao walikuwa Pwani na Nyanda za kusini na wengine kanda za maziwa makuu, ila wakoloni ndiyo waliwakusanya na kuwaweka pamoja wote kanda za ziwa Victoria? (kama mfano). Na si kwamba, hizi koo zinazoongea lugha moja na kuelewana (achilia mbali Kiswahili) zilikuwa zimejikusanya kanda mbalimbali kwa common interest kabla ya hata hao wakoloni kuja?!

Vinginevyo, nashukuru kwa mwangaza wa maelezo yako hapo juu.

Steve Dii
Nashukuru kwa kunielewa vema mkuu, hili ndo hasa lilikuwa lengo la swali langu.
 
Mkuu Zakumi, maelezo yako kwa swali la Mkurabita yanatia mwangaza kwenye swala zima la historia ya Kiswahili chetu na makabila. Lakini hata hivyo naona maelezo yako yanakwepesha swala la msingi ndani ya swali lake, kama jinsi nilivyolielewa mimi na baadhi ya wachangiaji wengine hapo juu.

Mkurabita ameuliza na kutolea mfano utofauti wa kikabila pragmatically, kama vile Wachaga, Wahaya, Wajaruo na Wakwere. Basi kwa jinsi nilivyomuelewa mimi anachotaka kujua ni lugha zipi hizo (mimi sizifahamu) mbali na lahaja au lafudhi mbalimbali za Kiswahili zilizopo Zanzibar na Tanzania Bara (kama zipo au zilikuwepo huko Zanzibar). Tukumbuke kwamba regional accents zipo kila pahala duniani. Akina Bush wa Texas hawana lafudhi sawa na kina Palin huko Alaska, vivyo hivyo watu wa NY wanaongea tofauti na watu wa Miami. Ma-scouser wa Liverpool ni tofauti na ma-cockney wa London, Waspanish wa Madrid nitofauti kabisa na waongeao kihispania kule Venezuela n.k. Hizi ni variations au lahaja za lugha na zinatokana na mkusanyiko wa koo mbalimbali zenye kutumia lugha hiyo. Hivyo maelezo yako kwa jinsi nilivyoyaelewa mimi yamejikita katika kuelezea asili na tofauti hizi katika Kiswahili. Wakati swali la Mkurabita nikutaka kujua uwepo wa lugha nyinginezo za Kibantu (au asili nyingine) mbali na Kiswahili. Lakini kwasabau Kiswahili nayo ni lugha, na kama ndiyo pekee iliyokuwepo/iliyopo Zanzibar, basi uniwie radhi maana maelezo yako yanatosheleza kabisa, yakwamba lugha hiyo huko Zanzibar ni Kiswahili (ila kwa koo tofauti tofauti na lahaja tofauti tofauti).

Swala jingine, nakubaliana nawe kuwe maisha ya Waafrika yalikuwa yapo kwenye koo.Si hivyo tu, bali mpaka sasa koo nyingi bado zinaendelea kuwepo. Mkuu ningelipenda utoe maelezo pale unaposema kuwa upangaji wa makabila uliopo sasa hivi umetokana na ujio wa wakoloni. Je, unataka kutueleza kuwa kabla ya wakoloni kuja, koo hizi unazosisema zilikuwa zimetapakaa huku na kule kila pahala ila wakoloni ndiyo walizikusanya? Mfano, baadhi ya Wahaya na Wasukuma bila kujali chimbuko lao walikuwa Pwani na Nyanda za kusini na wengine kanda za maziwa makuu, ila wakoloni ndiyo waliwakusanya na kuwaweka pamoja wote kanda za ziwa Victoria? (kama mfano). Na si kwamba, hizi koo zinazoongea lugha moja na kuelewana (achilia mbali Kiswahili) zilikuwa zimejikusanya kanda mbalimbali kwa common interest kabla ya hata hao wakoloni kuja?!

Vinginevyo, nashukuru kwa mwangaza wa maelezo yako hapo juu.

Steve Dii


Zakumi na Steve Dii mnapoints nzuri. Ingekuwa vizuri sana kama watanzania wengine tungekuwa na mwelekeo wenu.

Ukiangalia kwa undani unaweza kuona kuwa JKN alikuwa anajitahidi sana kuifanya Tanzania iwe Nation-state sio a Nation made up of states kama walivyotuacha waingereza, alikuwa anajaribu kuifanya Tanzania iwe kama Zanzibar ambako makabila yame-disolve kwenye uzanzibar.

Nafahamu kuwa kulikuwa na wamtan'gata, watumbatu, wanguja, na mengine lakini sasa hakuna. Pamoja na kuwa wenyewe wanaita jamii kwa ujumla kulikuwa na hall marks zote za makabila. Historia inaonesha hivyo.

Hata wazanzibari wa sasa ukiangalia kuna wengi ni wahamiaji toka bara, lakini ukiwauliza nyie kabila gani wanasema hawajui, lakini wamewahi kusikia kuwa baba au mama ni wa kabila fulani toka bara, au kabila fulani toka shelisheli and alike. Uzuri ni kwamba Zanzibar ni state, na watu wake ni wazanzibar, inagawa siku hizo wanasiasa wameanza kuwagawa kwa upemba na uunguja.

Huku bara misingi aliyoiacha JKNyerere sasa ina nyufa nyingi, umeanza udini na ukabila, kasi ya kuunda Nation state imepungua, tumeanza kuunda nation with states in it.
 
@ original pastor weye huwezi kupata demu wa kizenj hata siku moja labda useme ulikwenda zenj ukakutana na mnyamwezi mwenzio ambae amekwenda sawa na weye. Wacha kujipakazia weye **** nini?
 
kitabu cha historia cha zamani cha darasa la tano, historia ya jamii za waafrika hadi mwaka 1880, kiasema zenji kulikuwa kuna makabila ya wahadimu, watumbatu ,wamvita na jingine nimelisahau, ila wazenji wengine wanakataa wanadai haya si makabila ila ni jamii tu

kumbuka waafrika wa asili waliokuwa zanzibar miaka mingi nahisi walichukuliwa utumwani wakauzwa arabuni au elsewhere na wale walioko kule ni wale watumwa waliopelekwa kule kufanya kazi kwenye mashamba ya mikarafuu na minazi ili kuwa wakwezi na kutengeneza mbata (labda ndio maana weusi wengi kule wana asili ya unyamwezi) au watu walioenda zanzibar kutafuta maisha(mfano abeid karume inadaiwa alitoka malawi),

i stand to be corrected
Hao watu wanaodai kuwa hizo ni jamii tu na si makabila, hawaelewi maana ya neno kabila "Kabila" kama alivyo eleza Zakumi ni neno lililokopwa kutoka kwenye Kiarabu... Na maana yake ni mkusanyiko wa jamii za wahamihaji (nomadic families of the same blood). Tunapotaja koo hizi zinapatikana ndani ya kabila moja...!

Zanzibar makabila yapo mfano kuna Watumbatu, Wahadimu, Wapemba na Wadiba Gonga hapa unaweza kupata mwanga kidogo.
 
@ original pastor weye huwezi kupata demu wa kizenj hata siku moja labda useme ulikwenda zenj ukakutana na mnyamwezi mwenzio ambae amekwenda sawa na weye. Wacha kujipakazia weye **** nini?
Hawapatikani kivipi mkuu...? Ina maana ukipeleka posa kwa kuwa wewe unatokea bara upewi mke?
 
Nimeulizwa hili swali nikachemka,eti huko Zanzibar kuna makabila mangapi au ni Wapemba na Waunguja?
 
Kuna makabila mengi pamoja na WAHA, WANYAMWEZI na WASUKUMA. Wapemba au Waunguja siyo makabila ila ni watu wanaoishi Pemba na Unguja kama vile uanze kusema kuna kabila la Wamorogoro, Wairinga, Watabora nk
 
Waunguja, wagunja, washiraji, washihiri......................
 
Back
Top Bottom