Yajue makundi ya vyakula pamoja na faida za kula chakula bora

Yajue makundi ya vyakula pamoja na faida za kula chakula bora

Ndiyo maana wacheza tennis, mpira ngumi heavyweights kwa wazungu wakiwa kambini wanakuwa na dietitian anafanya kazi na mpishi kuhakikisha wanapata mlo unaowafaa.

Dietitians jamani TZ wapo wangapi my dear?

I wish nimpate mmoja nimlipe!

Sidhani kama tunao kiivyo my dear!
 
Mkuu

Naelewa unachokisema!

Kuhusu Body Builders kupata heart attacks mzee wala sio chakula wala uzito wa vyuma,ni STEROIDS!

Hilo ndio jibu sahihi!

Hayo mengine kuhusu body builders ni total fabrications!

Kama ulivyosema,ATP itumike yote then ile ziada ambayo ipo in form of FAT ndio itatumika,ni sahihi..Kunyanyua vitu vizito can guarantee that!

Kunyanyua vyuma inahitaji too much energy in such a way that inakula ile FAT yote na inavamia ile FAT na kuitumia yote kujenga muscles!

Zile muscles zinafanya mtu anapasuka.Na muscles sio FAT,ile ni kama pure steki,ambayo ni sawa!

Ukila chakula kawaida bila steroids za aina yoyote na ukanyanyua vyuma kadiri unavyoweza guarantee ya kumaliza fat na kujenga muscles ni 100% bila eti cha heart attack wala ujinga mwingine wa kupumua,etc!

Kunyanyua vyuma ni so intense kukuhakikishia burning ya ujinga wote called fat na pia upumuaji kuhakikisha cardio system ni well workout!

Tatizo labda ni kujua body yako inabeba uzito gani kwa muda gani,hiyo ndio unatakiwa ushinde Youtube upate elimu ya kutosha!

Vyuma ni so reliable ina guarantee 1 year kupata clean muscles na zero fat.

Thats true kwangu binafsi,nilijaribu yote hayo,kukimbia,aerobics,etc ila nikaona natumia muda mwingi kuzunguka zunguka bila true shredding down of fats,vyuma hasa vizito na ukasukuma haswa bila cheating,results ni inevitable!
oh basi watu watu wapige vyuma but mimi NO
 
Nimetafakari nikajua CHANZO CHA MARADHI MENGI NI WEWE MWENYEWE! Kwa nini nasema hivi? Ni kwa sababu maradhi mengi yanayowapata watu siku hizi yanatokana na namna tunavyoishi.

Mfano, unakula nini? Unakunywa nini? Je, unafanya mazoezi ya kutosha ili kuufanya mwili wako kuwa active? Unakunywa maji kiasi gani kwa siku?

Kwa kawaida tunakula milo miwili au mitatu kwa siku. Je, baada ya kula milo hiyo kwa siku, unapata haja kubwa mara ngapi kwa siku? Au ndiyo zinapita siku 2, 3, 4 hadi week nzima ndiyo upate haja kubwa?

Ok, labda unapata haja kubwa vizuri. Je, kinatoka chenyewe au unatumia nguvu kukisukuma ili kitoke? Kama unatumia nguvu kukisukuma jua kwamba tayari kuna tatizo kwenye mfumo wa mmeng'enyo wako wa chakula.

Naomba ujiulize maswali hayo kisha ujijibu mwenyewe then utatambua ni kwa namna gani chanzo cha maradhi mengi ni wewe mwenyewe.

Mlo kamili ni nini hasa? Mlo kamili hutokana na mchanganyiko wa chakula kutoka katika makundi mbalimbali ya vyakula. Kwa nini tunashauriwa kula mlo kamili? Ni kwa sababu mlo huo huupatia mwili virutubisho vyote vinavyohitajika kwa ajili ya lishe na afya bora.

Tunashauriwa kula walau milo mitatu iliyo kamili kwa siku. Ili kupata mlo huo kamili tunapaswa kuchagua vyakula kutoka katika makundi yafuatayo:

(1) vyakula vya nafaka mizizi na ndizi. Mfano mahindi, mihogo, viazi, mbatata, ndizi n.k

(2) vyakula vya jamii ya kunde na vyenye asili ya wanyama. Mfano soya, choroko, njegere, maharage n.k, samaki, nyama, mayai n.k.

(3) mboga mboga na matunda. Mfano aina zote za matunda, mboga zote za majani, karoti, hoho, biringanya, ngogwe, nyanya n.k

(4) mafuta na sukari. Mfano karanga, nazi, mafuta ya kupikia, miwa n.k.

(5) maji. Tunashauriwa kunywa maji kwa wingi kadiri mtu awezavyo lakini pia isiwe chini ya glass 8 kwa siku. Lakini pia sahani ya mlo kamili inapaswa kuwa na mboga mboga kwa wingi kuliko vyakula vya mizizi na nafaka hii ni kwa sababu mboga mboga zina nyuzinyuzi (fibre) za kutosha zinazosaidia mmenge'enyo wa chakula tumboni.

MUHIMU:

👉 tumia vyakula vinavyopatikana katika mazingira unayoishi.

👉 pendelea kula nyama nyeupe zaidi kuliko nyekundu.

👉 kula mboga mboga kwa kiasi kikubwa kuliko nafaka.

👉 zingatia usafi na usalama wa chakula na maji.

👉 tumia mafuta na sukari kwa kiasi.

👉 punguza matumizi ya chumvi, kahawa, chai na soda.

Baada ya kuangalia makundi hayo jaribu kujitathmini mwenyewe. Je, unayazingatia hayo? Kama siyo, anza sasa.
 
Naunga mkono hoja, asilimia kubwa watu hawali mlo kamili, unakuta mtu ananenepa tumbo tu.
Asubuhi muhogo
Mchana ugali na bamia
Usiku ugali wa muhogo na dagaa
Siku imeisha hapo
Vyakula vyote hapo asilimia kubwa vimejaa wanga kwa wingi, ndio maana tunadumaa.
 
Back
Top Bottom