Tempus Fugit
JF-Expert Member
- Jun 22, 2016
- 850
- 2,212
Mnamo mwaka 2019 Tanzania ilifanya marekebisho ya sheria yake ya Makampuni ya mwaka 2002 na kuleta mambo kadhaa mapya. Marekebisho hayo yaliletwa na sheria ya “The written laws (Miscellaneous Amendments) (No.3) Act, 2019" Kifungu cha 10 cha sheria hii kilileta kifungu kipya cha 400A katika sheria ya Makampuni ya mwaka 2002 ambacho kilileta mabadiliko kadha wa kadha.
Nchini Tanzania makampuni husajiliwa na Msajili wa Makampuni wa mamlaka iitwayo BRELA . Marekebisho hayo ya sheria ya makampuni yamempa msajili mamlaka ya kuifuta kampuni yoyote katika rejista ya makampuni endapo mazingira yafuatayo yatathibitika kutokea.
Je, ufanye nini endapo kampuni yako itafutwa na msajili kwa sababu hizo tajwa?
Kifungu cha 400A (2) cha Sheria ya makampuni ya Tanzania kinawapa wamiliki wa kampuni nafasi ya kufanya yafuatayo baada ya kupokea notisi ya kusudio la kufutwa kwa kampuni yao.
Kwa mujibu wa kifungu cha 400A (3) cha sheria ya Makampuni endapo kampuni itashindwa kutoa maelezo ya kwa nini isifutwe ndani ya siku 30 toka ipokee notisi ya kusudio la kufutwa na msajili, au endapo maelezo hayo hayatoi sababu zinazomridhisha msajili basi ataifuta kampuni hiyo katika rejista ya makampuni na kuchapisha maamuzi hayo katika gazeti la serikali.
Endapo kampuni, mwanahisa, au mtu anayeidai kampuni iliyofungwa hajaridhika na maamuzi ya msajili ya kuifuta kampuni, je achukue hatua zipi?
Kwa mujibu wa kifungu cha 400A (4) wahusika ambao hawajaridhika na maamuzi ya msajili ya kuifuta kampuni husika wanaweza kupeleka maombi Mahakamani kuomba kampuni iliyofutwa irejeshwe kwenye rejista ya makampuni. Maombi haya ni lazima yafanywe ndani ya miaka mitano (5).
Baada ya mahakama kupokea maombi ya kurejesha kampuni iliyofutwa je inaweza kutoa maamuzi gani?
Kifungu cha 400A (5) cha sheria ya Makampuni kinaelekeza kuwa Mahakama ikipokea maombi hayo inaweza kuamuru yafuatayo;
Kufanya mambo hayo matano nchini Tanzania kunaweza kuifanya kampuni yako kufutwa.
Nchini Tanzania makampuni husajiliwa na Msajili wa Makampuni wa mamlaka iitwayo BRELA . Marekebisho hayo ya sheria ya makampuni yamempa msajili mamlaka ya kuifuta kampuni yoyote katika rejista ya makampuni endapo mazingira yafuatayo yatathibitika kutokea.
- Endapo kampuni ilisajiliwa kiulaghai (Fraudulent registered company)
- Endapo kampuni inajihusisha na vitendo vya jinai kama utakatishaji fedha, kufadhili ugaidi, biashara ya madawa ya kulevya, biashara ya binadamu au jinai nyinginezo kama alivyoainisha waziri anayehusika na biashara.
- Upotoshaji/ulaghai wakati wa kusajiliwa kwa kampuni husika.
- Endapo wanahisa au ma dairekta wa kampuni hawaruhusiwi kuingia nchini Tanzania kwa matakwa ya kisheria.
- Endapo kampuni inafanya shughuli tofauti na zilizo ainishwa katika katiba yake.
Je, ufanye nini endapo kampuni yako itafutwa na msajili kwa sababu hizo tajwa?
Kifungu cha 400A (2) cha Sheria ya makampuni ya Tanzania kinawapa wamiliki wa kampuni nafasi ya kufanya yafuatayo baada ya kupokea notisi ya kusudio la kufutwa kwa kampuni yao.
- Kumuandikia msajili kwa maandishi sababu za kutosheleza za kwa nini kampuni hiyo isifutwe kwenye rejista ya makampuni.
- Kufungua shauri mahakamani kupinga notisi ya msajili ya kusudio la kuifuta kampuni husika.
Kwa mujibu wa kifungu cha 400A (3) cha sheria ya Makampuni endapo kampuni itashindwa kutoa maelezo ya kwa nini isifutwe ndani ya siku 30 toka ipokee notisi ya kusudio la kufutwa na msajili, au endapo maelezo hayo hayatoi sababu zinazomridhisha msajili basi ataifuta kampuni hiyo katika rejista ya makampuni na kuchapisha maamuzi hayo katika gazeti la serikali.
Endapo kampuni, mwanahisa, au mtu anayeidai kampuni iliyofungwa hajaridhika na maamuzi ya msajili ya kuifuta kampuni, je achukue hatua zipi?
Kwa mujibu wa kifungu cha 400A (4) wahusika ambao hawajaridhika na maamuzi ya msajili ya kuifuta kampuni husika wanaweza kupeleka maombi Mahakamani kuomba kampuni iliyofutwa irejeshwe kwenye rejista ya makampuni. Maombi haya ni lazima yafanywe ndani ya miaka mitano (5).
Baada ya mahakama kupokea maombi ya kurejesha kampuni iliyofutwa je inaweza kutoa maamuzi gani?
Kifungu cha 400A (5) cha sheria ya Makampuni kinaelekeza kuwa Mahakama ikipokea maombi hayo inaweza kuamuru yafuatayo;
- Amri ya kuirejesha kampuni iliyofutwa na msajili katika rejista ya makampuni
- Kutoa amri nyinginezo zozote itakazoona zinafaa kuhusiana na kampuni iliyofutwa.
Kufanya mambo hayo matano nchini Tanzania kunaweza kuifanya kampuni yako kufutwa.