Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Alhamisi Tarehe 13 Machi 2014 - Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti

Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Alhamisi Tarehe 13 Machi 2014 - Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti

Chabruma

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2013
Posts
5,660
Reaction score
1,780
Wadau mpooooo? Kama kawaida nianze kwa kuwatakia kila la kheri na shughuli zenu za kila siku na nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema siku ya leo. Wale wagonjwa kama kawaida yetu tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu ili awaponye haraka. Wale waliotangulia mbele ya haki tumuombe Mwenyezi Mungu awaondolee adhabu za kaburi na awaandalie makazi mema huko waendako.

Wadau, baada ya jana Mheshimiwa Sammuel John Sitta kushinda kwa kishindo katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum baada ya kupata kura 487 na kumshinda kwa mbali mpinzani wake Hashim Rungwe aliyepata kura 69, leo ni uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti. Kwa mujibu wa kanuni, kwa vile Mwenyekiti ametoka Tanzania Bara, Kinyang'anyiro cha Makamu Mwenyekiti kitakuwa ni kwa Wazanzibari pekee. Aidha, kwa mujibu wa Makubaliano yaliyofikiwa pale mjengoni, kwa vile Mwenyekiti ni mwanaume wa kutoka Tanzania Bara, Makamu Mwenyekiti atakuwa mwanamke kutoka Zanzibar. Hii ni kusema kuwa uchaguzi wa leo watu wenye sifa ya kugombea kwa mujibu wa kanuni na makubaliano ni wabunge wanawake kutoka Zanzibar.

Mpaka sasa, bado sijapata orodha ya wabunge waliochukua fomu, nitaendelea kufuatilia na nikipata taarifa za uhakika nitawajuza. Ila katika pitapita yangu, nimekutana jina la Samiha Sululu kama sijakosema. Jina hili ndo linatajwa sana kuwa ndiye atakayekuwa Makamu Mwenyekiti. Sitashangaa kusikia hapo baadaye kuwa ni mgombea pekee aliyechukua fomu na kukidhi vigezo na hivyo kutumia kura ya Ndiyo (kura ya wazi) kumpitisha.

Kama ilivyo ada, natarajia kuungana na wadau wengi katika tukio hili. Kwa sasa wapo wengi ambao ni vigumu kuwataja wakiongozwa na Mkuu Skype, kbm, Mkuu ya Kaya, Pasco, Deo Corleone, OKWI BOBAN SUNZU, Simiyu Yetu na wengine wengi ambao mniwie radhi kwa kutowataja. Kwa sasa tuendelee kufuatilia maoni ya wadau juu ya ushindi wa Sitta huku tukitafakari majukumu yaliyo mbele yake. Kama kawaida Mods wataendelea kuweka mambo sawa ili wadau wapate mtiririko ulio sawia. Hadi hapo baadaye, Stay Connected."

================================================================

UPDATES 1

Wadau, taarifa ambazo nilizipata mapema leo ni kuwa hadi muda wa kurejesha fomu unamalizika, kulikuwa na wanawake wawili ambao walikuwa wamechukua fomu za kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum. Wagombea hao ni Samia Suluhu wa na Amina Abdallah Amour. Bado naendelea kusaka taarifa ili kujua kama wamerejesha ndani ya muda uliopangwa na wamekidhi vigezo. Ila kwa sasa tujue tu kuwa mtifuano hapo baadaye ni kati ya Samiha Suluhu wa CCM na Amina Ally wa CUF.

UPDATES 2
matokeo yanatangazwa kama ifuatavyo;
Idadi ya wabunge wote ni 629
Waliopiga kura ni. 523
Kura zilizoharibika ni. 7
Amina Abdallah Amour. 126 (24.1%)
Samia Hassan Suluhu. 390 (74.6%)


Kwa matokeo hayo, Samia Suluhu Hassan ametangazwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum
 
Pamoja sana Mkuu. Hakika wadau tunafurahi sana jinsi mnavyolipamba jukwaaa hili. Mwanzo kulikuwa na wadau wachache sana kwenye Jukwaa la Katiba Mpya. Ila kwa siku ya jana pekee limetembelewa namwadaumzaidi ya elfu thelathini.
 
pamoja sana!hilo jina la samiha suluhu nadhani kuna magazeti yalilitaja kuwa ndilo lilikuwa limepitishwa na cc ya ccm kuwa ndo mgombea wake upande wa visiwani(rejea magazeti yalipobainisha sitta kuteuliwa mgombea pekee kutoka ccm ktk nafasi ya mwenyekiti),hii ilikuwa kabla ya suala la gender kuibuka bungeni wakati wa kupitisha kanuni!na kama utakumbuka vizuri siku ile wajumbe walipoibua suala la gender pale bungeni mhe asha rose migiro aliunga mkono hoja ya gender na akasema kama ananusanusa vizuri itakuwa iko vizuri! naaminialimaanisha kuwa kwa upande wao walishazingatia suala la gender!
 
Sio sahihi kwa Mwenyekiti na Makamu wake wote watoke kwenye kundi moja. Samweli Sitta na Samia Suluhu wote wanatoka CCM, ni wajumbe wa NEC na pia mawaziri kwenye serikali ya Muungano!

Maadam wameweka vigezo vya jinsia na asili ya mgombea, basi Makamu Mwenyekiti yes, awe ni mwanamke toka Zanzibar lakini asiwe wa kundi moja na Mwenyekiti. Vinginevyo huu mchakato wa katiba mpya unazidi kukosa uhalali mbele ya wananchi. Na huu mchakato ukihodhiwa na watu wachache wa kundi moja ni wazi ndani ya miaka 5 ijayo tutatumia mabilioni mengine tena kutunga katiba mpya.
 
CCM hawana siasa za kutumia utashi na mazigira, wao suala la katiba kwao ni la kichama zaidi , ni kweli ingekuwa busara huyo makamu mwenyekiti atoke makundi mengine nje na ccm
 
Sio sahihi kwa Mwenyekiti na Makamu wake wote watoke kwenye kund moja. Samweli Sitta na Samia Suluhu wote wanatoka CCM, ni wajumbe wa NEC na pia mawaziri kwenye serikali ya Muungano!

Maadam wameweka vigezo vya jinsia na asili ya mgombea, basi Makamu Mwenyekiti yes, awe ni mwanamke toka Zanzibar lakini asiwe wa kundi moja na Mwenyekiti.

kweli mkuu litakuwa bunge c cm siyo katiba lazima bunge lazima liwe na makundi yote!!
 
Sio sahihi kwa Mwenyekiti na Makamu wake wote watoke kwenye kundi moja. Samweli Sitta na Samia Suluhu wote wanatoka CCM, ni wajumbe wa NEC na pia mawaziri kwenye serikali ya Muungano!

Maadam wameweka vigezo vya jinsia na asili ya mgombea, basi Makamu Mwenyekiti yes, awe ni mwanamke toka Zanzibar lakini asiwe wa kundi moja na Mwenyekiti. Vinginevyo huu mchakato wa katiba mpya unazidi kukosa uhalali mbele ya wananchi. Na huu mchakato ukihodhiwa na watu wachache wa kundi moja ni wazi ndani ya miaka 5 ijayo tutatumia mabilioni mengine tena kutunga katiba mpya.
Mkuu, ni sahihi kabisa usemavyo. Ila katika masuala ya uchaguzi, watu hawaaminiani na ndo maana suala la vyama haliepukiki.
 
Ni kweli mkuu. Ila wabunge ndo wanachagua. Wanajua kwa nini wanachagua. Sisi tutaishia kutoa maoni yetu tu humu JF

ni kweli kabisaaa!
pia hatuwezi kulaumu chama cha siasa,kwa sababu kila kundi liko huru kuweka mgombea,na ikumbukwe kwamba ccm walipotoa hayo mapendekezo yao,hawakujua hata wagombea kutoka makundi mengine watakuwa kina nani!na wala hawakujua nani atashinda!suala na nani achaguliwe liko chini ya wajumbe wenyewe!wanamchagua wanayeona anafaa,regardless ya anatoka kundi gani!huo ndio utaifa!je hujaona ktk nafasi ya kugombea uenyekiti ,makundi mengi hayakuweka watu kugombea?ni kwa sababu walikuwa na imani na waliojitokeza kugombea alikuwepo waliyemuamini anaweza kuwaongoza!na ameshinda kwa kishindo kikubwa!so lets wait and see! swali langu ni je yule mwanamke aitwae bahati aliyeteuliwa na mhe sitta kusimamia uhesabuji wa kura zake ni wa wapi na anatoka kundi gani?pls kwa anayefahamu atujuze!
 
Kwa hivi vigezo Mama Makinda anabaki kuwa mjumbe tu......Kama kawaida jioni na mimi ntajimwaya mwaya kwenye uzi huu kuona kama utakimbia kwa spidi ya langa langa kama jana.
 
unatusaidia sana, mpe hi mkuu skype

Asante sana mkuu, salam zako nimezipata moja kwa moja na ninaahidi panapo majaliwa yake Mwenyezi Mungu, nitakua nanyi jioni muda wa matukio ukitimu. Karibuni na endeleeni na dondoo zinazokujieni toka kwa wadau popote walipo kule Dodoma.
 
Back
Top Bottom