Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Alhamisi Tarehe 13 Machi 2014 - Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti

Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Alhamisi Tarehe 13 Machi 2014 - Uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti

Pamoja sana mkuu Chabruma na wajumbe wote wa jf, hali yangu kiafya namshukuru Muumba niko salama, panapo majaliwa nitakuwa nanyi muda wa jioni, karibuni.
 
Last edited by a moderator:
Amani kwako mkuu chabruma kumeshakucha salama japo kwa sasa dodoma kamvua cha kiaina kipo ila kazi inafanyika tupo pamoja mkuu.
 
Sitapenda kusoma updates za Simiyu Yao!! Maana huyo jamaa ameharibiwa na magamba. Sijui ndo ID anayoingia nayo Mkwe.re?!!
Nafahamu kuwa bavicha wengi mnanigwaya na kunichukia kwa kuwapa ukweli ntaendelea kuwagonga za uso sana bavicha wote mtaipata tu mwaka huu kazi imeshaanza jana tumempata mzee wa viwango leo tutampata samia kila kitu kinakuwa ok.
 
Muheshimiwa Simiyu, habari yako bana!
Habari njema mkuu nimechelewa kidogo kuingia jukwaani siunajua vikao vya mikakati dodoma vingi kweli ila sasa mambo yako vema tunakwenda kumchagua samia mkuu.
mungu akupe afya ili twende pamoja mkuu.
 
Wadau mpooooo? Kama kawaida nianze kwa kuwatakia kila la kheri na shughuli zenu za kila siku na nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema siku ya leo. Wale wagonjwa kama kawaida yetu tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu ili awaponye haraka. Wale waliotangulia mbele ya haki tumuombe Mwenyezi Mungu awaondolee adhabu za kaburi na awaandalie makazi mema huko waendako.

Wadau, baada ya jana Mheshimiwa Sammuel John Sitta kushinda kwa kishindo katika kinyang'anyiro cha nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalum baada ya kupata kura 487 na kumshinda kwa mbali mpinzani wake Hashim Rungwe aliyepata kura 69, leo ni uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti. Kwa mujibu wa kanuni, kwa vile Mwenyekiti ametoka Tanzania Bara, Kinyang'anyiro cha Makamu Mwenyekiti kitakuwa ni kwa Wazanzibari pekee. Aidha, kwa mujibu wa Makubaliano yaliyofikiwa pale mjengoni, kwa vile Mwenyekiti ni mwanaume wa kutoka Tanzania Bara, Makamu Mwenyekiti atakuwa mwanamke kutoka Zanzibar. Hii ni kusema kuwa uchaguzi wa leo watu wenye sifa ya kugombea kwa mujibu wa kanuni na makubaliano ni wabunge wanawake kutoka Zanzibar.

Mpaka sasa, bado sijapata orodha ya wabunge waliochukua fomu, nitaendelea kufuatilia na nikipata taarifa za uhakika nitawajuza. Ila katika pitapita yangu, nimekutana jina la Samiha Sululu kama sijakosema. Jina hili ndo linatajwa sana kuwa ndiye atakayekuwa Makamu Mwenyekiti. Sitashangaa kusikia hapo baadaye kuwa ni mgombea pekee aliyechukua fomu na kukidhi vigezo na hivyo kutumia kura ya Ndiyo (kura ya wazi) kumpitisha.

Kama ilivyo ada, natarajia kuungana na wadau wengi katika tukio hili. Kwa sasa wapo wengi ambao ni vigumu kuwataja wakiongozwa na Mkuu Skype, Mkuu ya Kaya, Pasco, Deo Corleone, OKWI BOBAN SUNZU, Simiyu Yetu na wengine wengi ambao mniwie radhi kwa kutowataja. Kwa sasa tuendelee kufuatilia maoni ya wadau juu ya ushindi wa Sitta huku tukitafakari majukumu yaliyo mbele yake. Kama kawaida Mods wataendelea kuweka mambo sawa ili wadau wapate mtiririko ulio sawia. Hadi hapo baadaye, Stay Connected.
Nategemea kuwaona skype,chabruma na mkuu wa kaya mwanzo mwisho,pamoja sana.
 
Habari njema mkuu nimechelewa kidogo kuingia jukwaani siunajua vikao vya mikakati dodoma vingi kweli ila sasa mambo yako vema tunakwenda kumchagua samia mkuu.
mungu akupe afya ili twende pamoja mkuu.

wewe huna utashi wa kuchagua mpaka upate order au maelekezo?
 
habari zenu wooote wana jf humu jukwaani,
naombeni mnijuze kikao leo kitaanza mda gani?? na ni lini mheshimiwa sitta ataanza majukumu yake rasmi ya kuliongoza bunge la katiba???
 
Habari njema mkuu nimechelewa kidogo kuingia jukwaani siunajua vikao vya mikakati dodoma vingi kweli ila sasa mambo yako vema tunakwenda kumchagua samia mkuu.
mungu akupe afya ili twende pamoja mkuu.

Lakini muheshimiwa kwa nini unapenda kubishana sana na watu wanakwenda kinyume na itikadi zako? Huoni kua unajishushia hadhi? Nadhani ungejaribu kuiga busara za mzee Kificho au una maoni gani?
 
habari zenu wooote wana jf humu jukwaani,
naombeni mnijuze kikao leo kitaanza mda gani?? na ni lini mheshimiwa sitta ataanza majukumu yake rasmi ya kuliongoza bunge la katiba???

Kikao leo ni saa 10 jioni kwa saa za Afrika ya Mashariki, pia Sitta ataanza majukumu yake rasmi kesho mara baada ya kula kiapo.
 
BAADA YA MCHUANO MKALI BAINA YA WABUNGE WANAWAKE KUTOKA ZANZIBAR, HATIMAYE, MHESHIMIWA AMINA ABDALLAH AMOUR AMEFANIKIWA KUPEPERUSHA BENDERA YA UMAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM.

WAJUMBE WOTE WA BUNGE MAALUM MPENI KURA ZENU. (PICHA IMEAMBATANISHWA)View attachment KURA.doc

CV YAKE HIYO HAPO CHINI



MCHAGUE AMINA ABDALLAH AMOUR KUWA MAKAMU
MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM











AMINA ABDALLAH AMOUR
MGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM
MAELEZO BINAFSI KWA UFUPI:
Jina: Amina Abdallah Amour Tarehe ya Kuzaliwa: 01/01/1951 Elimu: 1. Stashahada ya Sheria (Bournemouth, England) 2. Shahada ya Uzamili (Masuala ya Fedha) "Master of Business Administration in Finance Management" – (USA) Uzoefu wa Kazi: § Nimefanya kazi Benki kwa miaka 23 hadi ngazi ya Meneja § Mbunge – Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu 2010 hadi sasa
"TAFADHALI NAOMBA KURA YAKO"
 
Kwa faida ya wadau wote waliochukua fomu mpaka mida hii Samia Suluhu - ccm,na Amina alyy- cuf.
 
Lakini muheshimiwa kwa nini unapenda kubishana sana na watu wanakwenda kinyume na itikadi zako? Huoni kua unajishushia hadhi? Nadhani ungejaribu kuiga busara za mzee Kificho au una maoni gani?

mkuu hapo unamshauri changudoa kuacha kuuza mbweche kazi ipo.
 
Lakini muheshimiwa kwa nini unapenda kubishana sana na watu wanakwenda kinyume na itikadi zako? Huoni kua unajishushia hadhi? Nadhani ungejaribu kuiga busara za mzee Kificho au una maoni gani?
Mkuu nashukuru kwa ushauri ngoja niachane nao make wanapenda uchokozi usio na maana.
 
Back
Top Bottom