Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

kwa niliyo yaona kwenye Uchaguzi huu Mdogo hakuna haja tena ya kuwa na Vyama vingi. ni bora CCM ikabaki yenyewe... .maana huu sio uchaguzi
Basi kaeni kimya muache siasa. Sio kulia lia kama watoto. Nani kawaambia muende si mngesusa TADEA wakafanya wenyewe.
 
Haya ndiyo mambo ya nchi za maziwa makuu. Bado tuna jamii yenye baadhi ya viongozi wajinga wajinga,wabnafsi na uroho wa madaraka as if wamezaliwa nao.
 
Umezungumza jambo la muhimu sana na kama likifuatwa litaleta majibu mazuri ,tatizo wenzetu wanatumia nguvu sisi tunahubiri mambo ya Mungu na tuna tarajia matokeo chanya ktk Dunia yenye Watu wanaoishi kinyam
Mkuu ndio lililobaki tuu. Kuna SAA unyama unalipwa kwa unyama, na hasa hawa waliopewa dhamana na kukiuka wajibu wao.
Nadhani watu wangemuuliza mkurugenzi wa Mwanza 2010 kwa nini alimtangaza Wenje wakati kulikuwavna shinikizo toka juu amtangaze Waziri Masha?
Alikuwa anaokoa familia yake iliyokuwa hatarini
 
Kuna haja kuwa na tume huru ya Uchaguzi ili kuwatendea watanzania haki kwa sababu hali inavyoendelea 2020 kuna kazi sana
 
Msimu huu ushindi lazima kwa njia yeyote ile tusipate fedheha ya kufuta uchaguzi- ccm oyee.
 
Hatari sana tume huru ya muhimu sana ? Mie naamin 2015 lowassa alishinda uraisi ila figisu ndo zilitendeka
 
Mkuu usisahau wizi wa kura pia wa hawa maharamia.

Wakuu leo ndiyo Ile siku ya kujua kama rais Magufuli ama anapendwa ama Tayari raia washamchoka. Tupia hapa kinachojiri katika zoezi la upigaji kura na matokeo, na vipi mwitikio wa wananchi
 
Jaamani tuwe hapa pamoja mpaka matokeo yatakapo tangazwa........
 
Sijaona picha......
 
Sijui ACT tutaambulia japo kata moja? We deserve at least one
 
Awamu ya magufuli imezika kabisa misingi ya muasisi wa taifa hili wa haki na usawa. Na kinachoonekana wazi ndani ya taifa la Tanzania ni kiu ya kiwango kikubwa ya kumwaga damu.
Wewe utakuwa RAIA wa Nchi jirani
 
Mwenye update za Zanzibar jamani maana nasikia hali sio shwari huko



WANANCHI JIMBO LA DIMANI, ZANZIBAR WAPIGA KURA KWA AMANI NA UTULIVU.

Zoezi la upigaji wa Kura katika vituo mbalimbali lilianza saa 1 asubuhi kwa hali ya Amani na Utulivu huku baadhi ya wananchi waliojitokeza kupiga kura wakipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzine (NEC) kwa maandalizi mazuri kufanikisha Uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Rufaa, Mhe. Semistocles Kaijage akizungumza kuhusu mwenendo wa Uchaguzi huo mara baada ya kutembelea vituo vya kupigia kura katika jimbo hilo na kuzungumza na Mawakala wa Vyama vya Siasa waliokuwepo vituoni, Waangalizi wa Uchaguzi na Wasimamizi wa Uchaguzi huo amesema Tume imeridhishwa na kazi nzuri iliyokuwa ikiendelea katika vituo mbalimbali vya kupigia Kura.

“ Viongozi wa Tume tumetembelea vituo mbalimbali vya kupigia Kura katika jimbo la Dimani; tumeona wenyewe upigaji wa Kura unaendelea vizuri, tumewauliza Mawakala, Watazamaji na Wasimamizi wa Vituo vya Uchaguzi kila mmoja amesema Uchaguzi unakwenda vizuri, nachoweza kuwaambia watanzania Uchaguzi Dimani unakwenda Vizuri” Amesema Jaji Kaijage.

Amesema Wasimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo hilo wanaendelea kufanya kazi zao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Maadili pia kushughulikia kwa haraka changamoto zilizokuwa zikijitokeza katika baadhi ya vituo vya kupigia Kura.

Ameeleza kuwa zoezi zima la upigaji wa Kura linaendeshwa kwa uwazi mkubwa, Utulivu na Amani na kuwawezesha wananchi kupiga kura bila vikwazo vyovyote.

Aidha, Mhe. Kaijage amebainisha kwamba endapo yatajitokeza malalamiko yoyote wakati zoezi la upigaji wa Kura likiendelea katika vituo mbalimbali , Mawakala wa Vyama vya Siasa ambao ni wasimamizi wa Maslahi ya Wagombea na Vyama vyao Vituoni watajaza fomu ya malalamiko Na. 14 kwa mujibu wa Sheria ambayo inatoa fursa ya kushughulikiwa kwa malalamiko hayo.

Aidha, amebainisha kuwa mara baada ya zoezi la upigaji wa kura kumalizika leo saa 10 jioni kazi ya kuhesabu Kura itafuata ili hatimaye wamnanchi wa Jimbo la Dimani waweze kupatiwa matokeo ya maamuzi waliyoyafanya kupitia Kura zao.

Mhe. Kaijage amesisitiza kuwa Wasimamizi wote wa Uchaguzi huo wamepewa mafunzo ya kuzingatia ili kuhakikisha wanaendesha zoezi hilo kwa ufanisi mkubwa na kuwezesha matokeo kutangazwa kwa wakati ili kuwawezesha wananchi kumjua mshindi wa Uchaguzi huo.

“ Endapo taratibu zote za Uchaguzi zitakuwa zimekamilika kwa mujibu wa Sheria, hakutakuwa na sababu yoyote ya kuchelewesha matokeo,mpaka sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi tumeridhishwa na mwenendo mzima wa zoezi la upigaji wa Kura na matokeo yatatolewa kwa wakati” Amesisitiza.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe akizungumzia zoezi la Upigaji wa Kura amesema kuwa Wapiga Kura wanaoruhusiwa kupiga kura ni wale waliokidhi Sifa na Vigezo vilivyoainishwa kisheria kuwawezesha kupiga Kura.

Amesema kwa mujibu wa Sheria Msimamizi wa Kituo ndiye mwenye mamlaka ya maamuzi katika kituo cha kupigia Kura ikiwa ni pamoja na kuamuru kuondolewa kwa mtu yeyote atakayeonekana kufanya fujo au kuzuia zoezi la uchaguzi kuendelea kituoni.

Katika Uchaguzi Uchaguzi huo mdogo wa Ubunge wa jimbo la Dimani jumla ya Wapiga Kura 9,280 wanatarajiwa Kupiga kura katika Vituo 29 huku vyama vya Siasa vyenye wagombea vinavyoshiriki Uchaguzi huo ni 11 huku Waangalizi wa Uchaguzi waliojitokeza kushiriki katika Uchaguzi huo ni zaidi ya 300.
 
Ninamuelewa Trump sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…