Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

Haya mambo hayakuanza jana wala leo, haya mambo yalianza muda mrefu tangu 2010 CHADEMA walipowatuhumu CUF ya Maalim kule Zanzibar ni CCM B. Baada ya Seif kukubali kushirikiana na CCM katika serikali ya umoja wa kitaifa.

Kuna kipindi CUF waliwahi kuitwa WALIBERALI wanatetea ushoga, hii ilikuwa bungeni.

Lakini hebu tuachane na hayo turudi katika uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata 22 uliofanyika. Kabla ya uchaguzi kuna mambo mengi yalijitokeza na maneno mengi kuzungumzwa ikiwemo.

1. Shaibu Mketo na Mtatiro walitoa msimamo wao kuwa hawatasimamisha mgombea yoyote wa CUF na wala wagombea waliosimamishwa na Lipumba hawatambuliki hivo akawaomba wanaCUF kutokuwaunga wagombea waliosimamishwa na Lipumba.

2. Kuna watu walizusha mitandaoni CUF imeshakufa pamoja na Lipumba amefilisika kisiasa.

3. Kuna watu walizusha maneno Lipumba kila anapokwenda kwenye kampeni kuwanadi wagombea wa chama anazomewa.

4. Kuna watu walizusha Lipumba akipata kura zaidi ya 5 katika kata watajiuzulu kwa maana Lipumba hatakiwi.

Baada ya uchaguzi haya ndo yalikuwa matokeo baadhi ya maeneo:

Kata ya Kimwani, Halmashauri ya Muleba
CUF 2898
CCM 2882
CHADEMA 108
Hapa CUF ilishinda.

Kata ya Malta, Halmashauri ya Kwimba
CCM 1997
CUF 1725
CHADEMA 422
ACT 305

Halmashauri ya Sengerema kata ya Kahumulo
CCM 2251
CUF 1987
CHADEMA 245

Geita mjini kata ya Nkome
CCM 5443
CUF 3035
CHADEMA 333

Dar es Salaam kata ya Kijichi
CCM 7647
CUF 4574
CHADEMA 3433

Halmashauri ya Mbinga kata ya Maguu
CCM 3783
CUF 3014
CHADEMA 358

Tukienda upande wa NCCR waliosema chama hakipo
Kata ya Lembeni
CCM 2403
CHADEMA 1080
NCCR 87
 
Baba alimkataa mwanaye na mtoto ndo kashinda sijui baba ataomba hela Ya matumizi....!!
 
Matokeo ya Jana kwenye uchaguzi wamewaacha makamanda midomo wazi wasiaamini. Mi nilijua lazima jamaa watuchape za USO. Na kweli wanatuchapa licha ya kubweka mitandaoni but jamaa tusiowapenda wanatuchapa.

Sawa, jamaa wanatume na wasimamizi ni wao...but licha hivyo hawa jamaa bado wanasupport kubwa sana. Bado wanakubadilika sana, tusije kukajijitea wanakubalika vijijini kwani huko siyo Tanzania.


Nchi zote ambazo wapinzani wameingia madarakani inabidi chama tawala kisiwe na support kabsa..au wachache sana. Kilichopo now ni kuijenga image ya chadema badala ya watu kujijenga wao ndani ya chadema.

Poleni makamanda..!! Hata km maccm yanaiba lakini tukubali bado yana wafuasi wengi kutuzidi..!!
Kuna wananchi wengi ambao hawana vyama ebu focus huko badala ya kutaka wakina lembeli wawe makamanda.
 
Ukawa utawaumiza roho sana, ccm hawatafanikiwa kuua ukawa, bado inakuja operesheni Kata funua
 
Vyama vya upinzani visipoungana kuidhinda CCM ni ndoto za alinacha...
Naomba chadema na Cuf tuache ubinafsi. uchaguzi huu ungekuwa ahueni kwa vyama vya upinzani kama wengeweza kusimamisha mgombea moja moja kila kata...
Wapinzani acheni ubinafsi na uchu wa madaraka....mjipange upya....
Acheni kuwapa Maccm njia nyeupe kushinda kila uchaguzi.
Naomba kabla ya kuanza kuzilalamikia vyombo vya dola na tume mbovu ya uchaguzi muungane kwanza muwe kitu kimoja.....
 
Hiyo CUF iliyoshinda huko bukoba ni ile ya Prof au ni ile Cuf ya chadema
sasa ndo ujiulize kama chadema walipata kura 108 na cuf akapata zaidi ya ccm na chadema na mgombea alianadiwa profesa lipumba hapo ndo pakujiulizaaa kama mketo na mtatiro walitamka wazi ya kuwa wagombea hawawatambui
 
Vyama vya upinzani visipoungana kuidhinda CCM ni ndoto za alinacha...
Naomba chadema na Cuf tuache ubinafsi. uchaguzi huu ungekuwa ahueni kwa vyama vya upinzani kama wengeweza kusimamisha mgombea moja moja kila kata...
Wapinzani acheni ubinafsi na uchu wa madaraka....mjipange upya....
Acheni kuwapa Maccm njia nyeupe kushinda kila uchaguzi.
Naomba kabla ya kuanza kuzilalamikia vyombo vya dola na tume mbovu ya uchaguzi muungane kwanza muwe kitu kimoja.....
MKUU HAPO UMEONENAA VIZULI SANA
 
Upinzani bila kujali tofauti zao ili waiondoe ccm ni lazma waungane, tena sio wasubir mpaka uchaguzi ufike ndio waungane no, waungane sasahivi maana baadae watakuwa wamechelewa
 
Hapana,, iwepo tu hiyo post. Ni challenge pia.
Wapinzani walipaswa kusimamisha mgombea moja moja kila kata, lakini hawakufanya hivyo...waligawana kura na MACCM wakatumia udhaifu huo kushinda.
Takwimu zinaonesha kwamba kama wapinzani wangeungana kwa kusimamisha mgombea moja moja wangegawana kata hizo na MACCM
wapinzani wanapaswa kujifunza kufanya kazi pamoja, waacha ubinafsi, chuki na unafiki wa kivyama..wakae chini wazungumze kuwa wamoja....lasivyo kuishinda CCM ni ndoto za alinacha.
 
Haki haiombwi hata siku moja. Hapa ni africa na mna deal na waafrica hawa sio wazungu hawa ni ccm ni kina barrow ni kina qaddafi ni kina mugabe.
Sasa mkidhani mtawashinda kwenye box la kura msahau.
Woga wetu ndio umaskini wetu
Mimi na nani? Unanijua mimi na crew yangu?
Tuligombea wapi?
Au ushakunaku tu

Kifupi ni kwamba mmevurugwa!!
 
Haya niliyategemea sana.Hivyo Siwezi kushangazwa nayo ila NEC ndiyo ya kulaumiwa na Wapinzani Wenyewe hawachulii issue ya Uchaguzi kama sensitive issue.
Mpaka marehemu wamepiga kura
 
baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa kata 22 za udiwani na hatimaye cuf kupata 1 na chadema 1 ,

jee ni kweli cuf kupitia profesa lipumba sasa imeanza kukubalika kwa wananchi kuliko chadema ,

ikubukwe ya kwamba kabla ya uchaguzi baadhi ya makada wakubwa wa cuf akiwemo julius mtatiro pamoja shaibu mketo waliwahi kutamka wazi kuwa cuf haijasimamisha mgombea na hivo kuwataka wananchi kuunga vyama vingine kupitia ukawa.

ikumbukwe pia kabla ya uchaguzi mdogo kumekuwepo na kundi la watu waliokuwa wakiwazomea wagombea wa cuf pamoja profesa lipumba kuonyesha ishara cuf haikubaliki lakini pia cuf ya lipumba imepoteza mvuto kwa wananchi.

sasa baada ya wagombea hawa kuingia katika kuingia katika uchaguzi matokeo yalikuwa hivi upande wa dar na kanda ya ziwa. ......

1.kata ya KIMWANI iliyopo halmashauli ya muleba uko bukoba kanda ya ziwa
CUF 2898
CCM 2882
CDM 208

2.KATA YA NKOME huko geita kanda ya ziwa hioo
CCM 5443
CUF 3035
CDM 333

3.HALMASHAULI YA SENGEREMA kanda ya ziwa hii kata ya kahumulo
CCM 3783
CUF 1987
CDM 358

4.HALMASHAULI YA KWIMBA kata ya malta.
CCM 1997
CUF 1725
CDM 422

5.DAR ES SALAAM kata ya kijichi
CCM 7647
CUF 4577
CDM 3433

ukiangalia kwa matokeo haya utagundua cuf amepata kura nyingi kuliko chadema ,

lakini pia ukiangalia kwa matokeo haya kama upinzani wangeweka mgombea mmoja tuu wangeweza kushinda ushauli wangu viongozi kwanini msiungane mkamaliza tofauti zenu hii hali inakatisha tamaa wapiga kura jamani ,.....

lipumba kaa wenzio mmalize tofauti zenu hii hali inatuumiza wapiga kura pia akina lisu mbowe unganeni na cuf
 
baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa kata 22 za udiwani na hatimaye cuf kupata 1 na chadema 1 ,

jee ni kweli cuf kupitia profesa lipumba sasa imeanza kukubalika kwa wananchi kuliko chadema ,

ikubukwe ya kwamba kabla ya uchaguzi baadhi ya makada wakubwa wa cuf akiwemo julius mtatiro pamoja shaibu mketo waliwahi kutamka wazi kuwa cuf haijasimamisha mgombea na hivo kuwataka wananchi kuunga vyama vingine kupitia ukawa.

ikumbukwe pia kabla ya uchaguzi mdogo kumekuwepo na kundi la watu waliokuwa wakiwazomea wagombea wa cuf pamoja profesa lipumba kuonyesha ishara cuf haikubaliki lakini pia cuf ya lipumba imepoteza mvuto kwa wananchi.

sasa baada ya wagombea hawa kuingia katika kuingia katika uchaguzi matokeo yalikuwa hivi upande wa dar na kanda ya ziwa. ......

1.kata ya KIMWANI iliyopo halmashauli ya muleba uko bukoba kanda ya ziwa
CUF 2898
CCM 2882
CDM 208

2.KATA YA NKOME huko geita kanda ya ziwa hioo
CCM 5443
CUF 3035
CDM 333

3.HALMASHAULI YA SENGEREMA kanda ya ziwa hii kata ya kahumulo
CCM 3783
CUF 1987
CDM 358

4.HALMASHAULI YA KWIMBA kata ya malta.
CCM 1997
CUF 1725
CDM 422

5.DAR ES SALAAM kata ya kijichi
CCM 7647
CUF 4577
CDM 3433

ukiangalia kwa matokeo haya utagundua cuf amepata kura nyingi kuliko chadema ,

lakini pia ukiangalia kwa matokeo haya kama upinzani wangeweka mgombea mmoja tuu wangeweza kushinda ushauli wangu viongozi kwanini msiungane mkamaliza tofauti zenu hii hali inakatisha tamaa wapiga kura jamani ,.....

lipumba kaa wenzio mmalize tofauti zenu hii hali inatuumiza wapiga kura pia akina lisu mbowe unganeni na cuf
Hoja yako ina mashiko.
 
Back
Top Bottom