Mallya: Kwenye Maelezo Yako umesema Kwamba Mlikuwa na Askari Wengine wa Moshi ni sahihi
Shahidi: Sahihi
Mallya: Kuna Sehemu Yoyote Umepata Kueleza Kwamba Mliachana Nao wapi hao Askari Wa Moshi
Shahidi: Sikueleza
Mallya: Idadi ya Askari Mliokutana nao Moshi Unakumbuka?
Shahidi: Sikumbuki Idadi yao
Mallya: Shahidi Washtakiwa Wanasema Mlikuwa watu zaidi ya 10 mliwavamia, na Kuwawekea Madawa na Bastola
Shahidi: Si kweli, Tulikuwa watano
Mallya: Jaji ataona wapi Kwamba Mlikuwa watano
Shahidi: Kwenye Statement Hakuna
My take: kama kati ya hao askari watano hakuna aliyetokea Moshi, basi watuhumiwa walisema ukweli kwamba askari waliowateka na kuwawekea madawa ya kulevya na bastola walikuwa 10 jumla. Wao kwenye maelezo yao yote walidai ni askari 5 ndiyo walioenda kuwakamata kina Adamoo. Huyu anasema askari wa Moshi walikuwepo pia.
Kaaazi kweli kweli!