Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Ndio Janja ya Kikwete kuwaondoa Wazee kamati kuu ...SASA mambo HAPA yote alipokuwa anapanga angemshirikisha mwinyi NA mkapa .,wangemshauri vema
 
Ebu tutoleeni upuuzi na tamaaa zenu za mafaraka hapa.
use your brain man,hata Kama unamshabikia MTU lakini sio lazima huyo huyo apate.
hivi lowasa ni nani mpaka asababishe machafuko nchini jina lake likikatwa,kwa nini anangangania kwenda ikulu?
Kama chama chake kimemkataa basi akubali..yaani ccm kukatana majina ndio kuchafue nchi???
yaani hii post imejaa kitoto Sana,not convincing at all
 

Wagombea wa CCM wanatafutwa na CC, NEC sio Ukawa..Ukawa wapo pembeni kuangalia yanayojiri..

Huyo anayeamini CCM atatoa rais sio UKAWA bali magamba wenzako waliovaa makoti ya UKAWA

Dr. Slaa huko uliko tambua kuwa wewe ndiye Rais wa Tano..
 
Pia TB Joshua na wachungaji fulani walioteshwa eti ENL ndiye raisi wa JMT awamu ya 5!

Unaushahidi au ulisikia maneno ya watu tu? Tupe ushahidi maana ibada za TB Joshua sio za siri ni live Emmanuel TV na videos YouTube. Tupatie source ya habari yako plz
 
kwa sababu,ili kulinda mali alizochuma,inabidi akichonge kinyago akipeleke ikulu na mali zake ziwe salama.
 
Kwa taarifa yako mleta mada Magufuli ni mwizi kama hao wengine. Ngoja uone nondo baadae leo
 
 
Hakuna mjumbe wa Ccm zaidi ya lowasa mwenyewe ambaye anaweza kusema hana imani na Jk hakuna coz whatver atakaye sema hilo ana majanga makubwa hizo ni mbwembwe tuu hakuna mjumbe anayeweza kusema hana imani na Jk
 
Kwlei sikio la kufa!

Yaan ibado unapendekeza muendelezo wa itikadi zilizoua taifa za kupeana madaraka kwa kulipana fadhila, kubebana na upozana bila kujali uwezo nia na sifa vitu ambavyo ni muhimu katika ufaninisi wowote?

Tadhalil bwana uwe serious.
 
Kosa la kumwacha Membe litaigharimu CCM bei kubwa mno. Walipoamua kumkata EL ilikuwa lazima Membe akatwe ili CCM iendelee kuwa moja. Wamefanya kosa, watajuta
 
Riziwani ndie yupo nyuma ya yote haya..dogo unataka kutuharibia nchi mbona?
 
Tatizo lako umejaaa Udini,Ukanda ,Ukabila

Tanzania we are past that

Again uache tabia yako ya kukomaa kuaminisha kwamba una uhakika sana na Mambo.........Kumbe ni bendera

Achana nae huyo ameshapoteza uhalali wa uchambuzi makini wa mambo ya siasa na amechanganyikiwa. Yeye anaamini katika siasa za ''umimi'' mtu ni bora kuliko chama au taasisi na pia ni mbinafsi na kigeugeu mkubwa sana. Sasa hivi ndio anazungumzia maswala ya zamu ya Zanzibar baada ya mtu wake kukatwa kwa aibu kubwa sana,wakati anatuaminisha humu ndani kuwa iwe mvua au jua usiku au mchana Lowasa lazima apite hakuongelea kabisa swala la zamu ya Zanzibar.
 
Habari, samahani mimi nipo nje Mada, nilikuwa nauliza hivi Upinzani ikishika dola, je madeni ya nchi inayodaiwa watayalipa au automatically yanafutwa nchi inakuwa haina deni kwani wanaotawala sio wa siku zote?? Nawasilisha.

Una umri mpaka sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…