Balozi Amina alihitimu Chuo Kikuu cha New Delhi , India - Shahada ya Uchumi (B.A), mwaka 1979, pia alisomea masuala ya utawala wa fedha na utafiti wa uendeshaji kwenye Taasisi ya Uongozi (Institute of Management) Pune, India mwaka 1980, pia mwaka 1981 alihitimu Chuo Kikuu cha Pune, India - (Symbiosis College of Management) -MBA in Marketing (Masoko) na mwaka 1983 Chuo Kikuu cha Helsinki, Finland - Diploma ya utafiti wa masoko na uuzaji wa bidhaa nje (mafunzo maalum ya PRODEC).
Nyadhifa alizoshika
Mwaka 1981 hadi 1982, Mchumi Mwandamizi -Tume ya Mipango Zanzibar, mwaka 1982 hadi 1983, Mkurugenzi Biashara za Nje - Wizara ya Biashara ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na mwaka 1983 hadi 984, Katibu Bodi ya Biashara Zanzibar- Wizara ya Biashara Zanzibar.
Nafasi nyingine ni, mwaka 1984 hadi 1985, Mchumi Mwandamizi - Tume ya Mipango, Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Zanzibar, mwaka 1985 hadi 1990- Mbunge Bunge la Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, mwaka 1985 hadi 1986- Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwaka 1986 hadi 1989- Waziri wa Nchi ,Wizara ya Mambo ya Nje.