Yaliyojiri kesi ya Halima Mdee na wenzake 18, Peter Kibatala anamkaanga Hawa Subira Mwaifunga

Yaliyojiri kesi ya Halima Mdee na wenzake 18, Peter Kibatala anamkaanga Hawa Subira Mwaifunga

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Katika mambo yaliyonishangaza kwenye kesi inayoendelea, ambapo Watu 19 wasio na Chama wanapigania roho zao Mahakamani kwa kung'ang'ania uanachama wa Chadema, huku wakiwa wametimuliwa kitambo, ni Makundi makubwa ya wana-CCM ndani na nje ya Mahakama wakifuatilia kesi hiyo.

Miongoni mwa wanachama hao wa CCM yumo anayeitwa ALLY BANANGA kutoka Arusha, ambaye bado haijajulikana sababu hasa za yeye kukurupuka kutoka Arusha hadi Dar kwa mambo yasiyomhusu.

Yako mengi yanayoendelea kwenye viunga hivi, kaeni mkao wa kula.

=====

Kesi inaanza. Jaji ameingia
Karani anasoma case number na aina ya Kesi. Tupo hatuaa ya Re-Examination
Mawakili wa pande zote wanaridhia kuwa wako tayari kuendelea.
Jaii anaandika

Anaepanda kikaangoni sasa ni Hawa Mwaifunga Shahidi wa 11. wakili Peter Kibatala anaanza kushughulika nae

Jaji: Jina lako?
Shahidi: Hawa Subira Mwaifunga
Jaji: umri wako?
Shahidi: Miaka 46
Jaji: Dini yako?
Shahidi; Mkristu
Jaji: utakula kiapo..
Shahidi anakula kiapo

WAKILI PETER KIBATALA AKIMUHOJI HAWA MWAIFUNGA MAHAKAMANI.
SEHEMU YA 1.

Kibatala;
Wewe ulikuwa Makamo Mwenyekiti wa BAWACHA?
Hawa; Ndio

Kibatala: Wakati Grace anatoa ushahidi ulikuwepo?
Hawa: Ndio

Kibatala: Uliusikia ushahidi wake
Hawa: Ndio

Kibatala: Wakati VIDEO zile mbili zinaonyeshwa uliziona?
Hawa: Ndio

Kibatala: Je, Ulisikia mzungumzaji yeyote yule kati ya waliozungumza akiwaita COVID 19?
Hawa: Walituita Wabunge 19.

Jaji: Sema Yes or No.
Hawa: Mheshimiwa Jaji, hakuna mzungumzaji aliyetuita COVID 19.

Kibatala: Kwa maelezo ya kiapo chako yanasema mliitwa Covid 19. [Kibatala anampelekea Shahidi akione Kiapo chake chenye maneno COVID 19.]

Kibatala: Je, Unamfahamu Covid 19 ni nani au ni akina nani?
Hawa: Mheshimiwa Jaji..... Mheshimiwa Jaji, samahani lakini; kuna majibu yenye maelezo. Huyo niliyemtaja kwenye Kiapo ndiye anamjua.

Kibatala: Je, na wewe ni mmoja wa hao COVID 19?
Hawa: Ndio, na Mimi ni mmoja wao

Kibatala: Isaidie Mahakama maana ya COVID 19
Hawa: COVID 19 ni Ugonjwa

WAKILI PETER KIBATALA AKIMUHOJI HAWA MWAIFUNGA MAHAKAMANI.
SEHEMU YA 2.


Mahakama imerejea...Saa 8:00pm. Kesi namba 36/2022 Halima Mdee na wenzake 18 dhidi CHADEMA.

Wakili Serikali: Mh Jaji Kwa upande wetu tuko vile vile kama awali..tuko tayari kuendelea
Wakili Panya: Na sisi pia Kwa upande wetu tuko kama tulivyokuwa asubuhi..
Wakili Peter Kibatala: Mh Jaji Kwa ruhusu naomba tumuongeze Wakili Hekima Mwasipu nasi Tupo tayari kuendelea
Jaji: mniwe radhi Kwa kuchelewa mambo ni mengi

Kibatala: Kuna Mjumbe yeyote wa Kamati Kuu aliyekuita COVID 19?
Hawa: Hakuna Mjumbe wa Kamati Kuu aliyetuita COVID 19

Kibatala: Je, Unamfahamu Shaban Othman? Je, ni Mjumbe wa Kamati Kuu
Hawa: Hapana, huyu sio Mjumbe wa Kamati Kuu.[Kibatala anampelekea Shahidi Kiapo chake aone alichokieleza.]

Kibatala: Mwambie au umuonyeshe Mheshimiwa Jaji kama kweli COVID 19 aliyesemwa na Shaban Othman ni wewe.
Hawa: Huyu aliandika maneno haya kipindi tumeitwa na Kamati Kuu ya Chadema.

Jaji anaandika.....

Kibatala: Msaidie Jaji ajiridhishe kwamba kweli COVID 19 ni wewe Hawa Mwaifunga ama wenzako wengine.
Hawa: Ili uamini alikuwa anamaanisha sisi, alisema hivyo wakati tumeitwa na Kamati Kuu ya Chadema

Jaji: Nimerekodi kwamba; kwa kuwa waliitwa pale na Kamati Kuu, hivyo wakajua ni wao wanasemwa

Kibatala: Je, neno COVID 19 ni muhimu kwenye Kesi yako ama sio muhimu?
Hawa: Kwa sababu ni kiambatanisho kwenye Kesi yangu

Kibatala: Hilo neno la COVID 19 nalo ulilikatia Rufaa?
Hawa: Nilikatia Rufaa kutopewa nafasi ya kusikikizwa

Kibatala: Shahidi mlivyokata Rufaa mlizipeleka kwa Mwakilishi wa CHADEMA
Hawa; Ndio

Kibatala: Je, ni kweli kwenye Aya ya 7 maneno John John Mnyika yalichapishwa kwenye Media za ndani na nje ya nchi?.
Hawa: Ndio, ni kweli

Kibatala; Kwa hiyo malalamiko yako ya msingi ni nini kwenye Kesi hii?
Hawa: Malalamiko yangu ni kutosikilizwa kabla ya kuhukumiwa

Kibatala: Je, kama suala ilikuwa ni wewe kusikilizwa, maneno ya John John Mnyika yalikuwa yanahusiana na nini?.
Hawa: Yalikuwa yanaleta taharuki kwa Wanachama

Kibatala: Kwa ufahamu wako; Kamati Kuu ina wajumbe wangapi? Na Kiapo chako hakuna mahali umeeleza Kamati Kuu ina wajumbe wangapi
Hawa: Hakuna sehemu nilipoonyesha Idadi ama majina ya wajumbe wa Kamati Kuu.

Kibatala: Je, Jaji atajuaje ni wangapi na ni akina nani?
Hawa: Kamati ni chombo kikubwa kinajulikana.

Kibatala: Ni sahihi chombo chochote kama Kamati Kuu kinaweza kuendelea na mdahalo pasipo mhusika kuwepo kutokana na mazingira fulani fulani?

Jaji: Swali linasema; Yapo mazingira ambayo Mahakama ama chombo chochote cha maamuzi kinaweza kuendelea na uamuzi wa jambo pasipo mhusika kuwepo?
Hawa: Mheshimiwa Jaji; Kwa swali hili, kusema ndio ama hapana inakuwa vigumu

Jaji: Nadhani unamaanisha kwamba huelewi
Hawa: Eeeeesh

Mahakama kicheko 🤣👋👋

Kibatala: Unajua kwa nini John John Mnyika alisema kupitia Press Conference kwamba; popote pale walipo wapate taarifa ya wito.
Hawa: Hapana

Kibatala: Mwambie Jaji sababu inayokufanya uamini kwmaba John John Mnyika alikuwa anafahamu uko wapi hiyo tarehe 25
Hawa: Alikuwa anafahamu

Kibatala: ni kweli ulimsikiliza John Mnyika aliwapa notes ya Kikao November 27 Cha nyie Kwa nini mlikwenda kuapa bungeni?
Shahidi: Kweli nilimsikia

Kibatala: Kweli ulimsikiliza John Mnyika akisema anafahamu kuwa nyie November 24,2020 mpo dodoma kuapa?
Shahidi: Nilimsikia na John Mnyika alikuwa anafahamu kuwa mm nipo dodoma naapa..

Kibatala: Nini kilikufanya ushindwe kufika mbele kikao kamati kuu Cha November 27..
Shahidi: Badaa kupata Barua November 25,2020 niliomba nipate muda kupitia hoja zake alizoniandikia ili nijbu.

Kibatala: ukitaka kuona Mtu amekutumia ujumbe WhatsApp umeupa unajuje?
Shahidi: itaonyenya jina au namba

Kibatala: Moja ya msingi wa Kesi yako ni wewe kitokupewa nafasi ya kusikilizwa?
Shahidi: Ni kweli sikupewa nafasi ya kujitetea Wala kusikilizwa hiyo habari kupata Barua Kwa WhatsApp ni kweli nilipata

Kibatala: Kwenye kiapo chako unasema kuwa Barua ulipata muda umeenda
Iliyohusu Kikao kuhamishwa kutoka Makao makuu kwenda Bahari beach
Shahidi: Barua ya ni November 27 Kwa njia WhatsApp

Kibatala: Nani amekuja mahakamani kulalamika kati wewe na CHADEMA
Shahidi: Mimi nimefungua Kesi na nipo chini kiapo..

Kibatala: Ulisha wahi kuambiwa Kuna kulipa gharama Kesi?
Shahidi: Ndio nasikia kwako

Kibatala: Ulimwandikia Katibu mkuu kuwa ulipata Barua November 27
Shahidi: Sikumwandikia

Kibatala: Umesema umekuwa CHADEMA Toka lini?
Shahidi: nimejiunga 2007

Kibatala: Unafahamu Zitto Kabwe alifukuzwa mwaka 2011 na Kamati kuu na kufungua Kesi mahakama hii?
Shahidi: Sikumbuki

Kibatala: Kifungu Cha katiba ya CHADEMA ibara 6.5.1 inaipa ruhusu Katiba ya CHADEMA kumchhukulia uamuzi mwanachama yoyote Kwa maslai ya Chama
Shahidi: Ndio

Kibatala: Ni kweli Kwa mujibu wa katiba hii CHADEMA inasema baraza kuu linaweza kufanya uamuzi bila kuwepo mrufaa?
Shahidi: Ni kweli baraza kuu linaweza kufanya hivyo.

Kibatala: Hicho kifungu kinasemaje?
Shahidi: ibara ya 6.5.1 b inasema kuwa mrufaa kupewa nafasi kujitetea

Kibatala: Rufaa yako ya kupinga kufukuzwa ulisikilizwa baraza kuu Kwa mdomo?
Shahidi: Sikilizwa mimi alisilizwa yule niliyemkatia rufaa ambaye ni kamati kuu..

Kibatala: Mtu ambaye ulimkatia rufaa akapeleka rufaa yako kwenye baraka kuu ambalo aliiandaa Kwa pesa nyingi Kwa nyie rufaa huko sio kusikilizwa?
Shahidi: Msimamo Wangu ule ule sikupewa nafasi ya kujitetea Wala kusikilizwa

Kibatala: Kwa mukhtasari huu kwenye kiapo chako na kiapo kinzani Cha CHADEMA kinanaksi kilichotekea kwenye kikao Baraza Cha Mei 11,2022
Shahidi: Ndio

Kibatala: kwaleo naomba kuishia Hapa.

Jaji: Anaandika kidogo.

Jaji: Naahirisha shauri hili mpaka Oktoba 21,2022

Jaji anatoka watu wote Mahakamani wanasimama juu.
 
Katika mambo yaliyonishangaza kwenye kesi inayoendelea, ambapo Watu 19 wasio na Chama wanapigania roho zao Mahakamani kwa kung'ang'ania uanachama wa Chadema, huku wakiwa wametimuliwa kitambo, ni Makundi makubwa ya wana-CCM ndani na nje ya Mahakama wakifuatilia kesi hiyo.

Miongoni mwa wanachama hao wa CCM yumo anayeitwa ALLY BANANGA kutoka Arusha, ambaye bado haijajulikana sababu hasa za yeye kukurupuka kutoka Arusha hadi Dar kwa mambo yasiyomhusu.

Yako mengi yanayoendelea kwenye viunga hivi, kaeni mkao wa kula.
Bananga hivi sasa ana lishwa na mkewe ambae nae yumo kwenye hilo kundi la wabunge wa NEC ya Magu.
Amehudhuria asije nyimwa msosi.
Bananga kawa mwanamume wa Dar. Ana lelewa.
 
Back
Top Bottom