Yaliyojiri Kesi ya Mbowe: RPC Kingai aeleza Mbowe alivyopanga kumdhuru Ole Sabaya. Kesi yaahirishwa hadi 27 Oktoba 2021

Yaliyojiri Kesi ya Mbowe: RPC Kingai aeleza Mbowe alivyopanga kumdhuru Ole Sabaya. Kesi yaahirishwa hadi 27 Oktoba 2021

Unaumia na nini kwani mpaka unasema yooote hayo? njaa mbaya sana wewe utakuwa ni wale wabunge wa chadema waliokosa ubunge 2020
Point of correction hakukuwa na uchaguzi mwaka 2020 bali ilikuwa uchafuzi ila Mungu fundi kabisa kabisa jina lake lihimidiwe
 
Kibatala: Uliwakamata na Kifaa gani kinachohusisha Kukata Miti

Shahidi: Sikuwakamata na Kifaa chochote
ha ha ha ha, Kingai hapa ulitakuwa umkamate Adamoo na shoka kubwa ile ya kukatia miti ya Mninga, mahakama haifanyi kazi kwa kuhisi, haipigi ramli mzee wangu, inataka kitu live live - lete shoka babaaa ama misumeno
 
Hili ni tatizo la kisiasa zaidi kuliko sheria, utatuzi wake utaegemea siasa zaidi kuliko ushahidi wowote ule wa kisheria.
Hii kesi ipo very technical kwenye baadhi ya maeneo shahidi aliposema alifukuzwa kazi kwa sababu za ugonjwa wa kichaa upande wa utetezi wajitahidi wapate hicho kielelezo waje wakitumie kwenye utetezi

kwa kuwa plan A ya kupinga kielelezo imeshindikana basi plan B wakati wa utetezi wajielekeze kwenye mental status ya mtuhumiwa wakati anahojiwa....

manake kwa kichaa kama huyu wakati anahojiwa hakuna uthibitisho wa kitaalam unaosapoti kwamba mentally alikuwa fit....

na shahidi wa jamuhuri hajazungumzia chochote aidha wakati wanamuhoji kulikuwa na medical proof kwamba alikuwa timamu..ushahidi wa kichaa thamani yake ni ndogo sana.

Vijana wa utetezi barabara hiyo nimewapa
 
ha ha ha ha, Kingai hapa ulitakuwa umkamate Adamoo na shoka kubwa ile ya kukatia miti ya Mninga, mahakama haifanyi kazi kwa kuhisi, haipigi ramli mzee wangu, inataka kitu live live - lete shoka babaaa ama misumeno
Hii kesi ukiisikiliza tu hata kama huna idea ya sheria unaielewa na maamuzi unayatoa hapohapo
 
tuendelee kuiamini serikali yetu kama ilitenda haki kwa Sabaya hata hapa naamini haitatuangusha...
 
Hii kesi ipo very technical kwenye baadhi ya maeneo shahidi aliposema alifukuzwa kazi kwa sababu za ugonjwa wa kichaa upande wa utetezi wajitahidi wapate hicho kielelezo waje wakitumie kwenye utetezi
Utimamu wa akili kwa shahidi hauna Mana kwa maelezo aliyotoa sababu aliachishwa kazi baada ya kuonekana ana matatizo ya akili pia alipokuwa sawa ndo akapata Hilo deal la mbowe hvyo hata cheti Cha uthibitisho kipatikane au kikosekane kwenye hayo mazingira ya kesi hcho cheti hakina maana.
 
Kibatala: Unakubaliana na Mimi Kuwa DNA ni Njia ya Kisasa Ya kuthibitisha Umiliki, na Jinai

SHAHIDI: ndiyo

KIBATALA: Umezungumzia Chochote Kuhusu DNA analysis

Shahidi: Hapana Mheshimiwa

Kibatala: Umemwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Adamoo amepata wapi hii Bunduki

Shahidi: Adamoo hakusema

Kibatala: Nikiangalia Kielelezo Cha Mahojiano nitaona Hilo swali?

Shahidi: Hapana Nilimuuliza Kama Mimi tu
duh, aisee kazi ipo - Kingai umeyatafuata haya !! Mwambie Jaji huna kifaa cha kupimia DNA ya vitu vyenye ncha kali - ha ha ha ha
 
Mawakili wa utetezi kesi ya mbowe wanatafuta credit kwa MAJORITY'S badala ya kutafuta credit kwa JAJI ambae ndio mwamuzi wa kesi yenyewe.

Hivyo hvyo wafuasi wa upande wa utetezi wanashupalia ushabiki ambao hauna mantiki kwenye kesi wanaacha maswala ya msingi kwenye kesi.

Nimeona mengi mno kwenye kesi ya sabaya na hii ya mbowe watu wanajikitika kwenye maswali na maelezo ambayo sio msingi wa kesi hvyo hayana maana.

Nipo hapa nafatilia taratibu.
 
RPC Kingai ameeleza hatua kwa hatua bila kuacha shaka jinsi Freeman Mbowe alivyopanga kumuuwa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Ole Lengai Sabaya kwa kutumia perfume ya sumu kwa madai kuwa Sabaya alikuwa anatishia nafasi ya Mbowe kuendelea kuwa mbunge wa jimbo la Hai.

====
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Ramadhani Kingai akisoma maelezo ya mshtakiwa wa pili katika kesi ya uhujumu uchumi, Adam Kasekwa amesema mtuhumiwa huyo alisema Freeman Mbowe alipanga kumdhuru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya.

Katika ushahidi alioutoa leo, Oktoba 26, 2021 katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Kingai amesoma maelezo ya mtuhumiwa huyo kwamba Mbowe alisema Sabaya anahatarisha nafasi yake ya kuendelea kuwa mbunge wa Hai.

Ifuatayo ni sehemu ya maelezo ya mshtakiwa Adamu kama yalivyosomwa na RPC Kingai:

“Mbowe alituelekeza tufuatilie nyendo zake na tumdhuru kwa spray ya sumu. Ling'wenya alifuatilia mtu wa kupata sumu. Tarehe 27 tulirudi Dar na magari mawili pamoja na Mbowe na mlinzi wake.

“Baada ya kufika Dar tulifikishwa Mikocheni mimi na Ling'wenya tulipewa Sh200,000 tujiandae.Baadaye tulipewa nauli turudi Moshi. Agosti Mosi saa 11 alfajiri Mbowe alituita akasema tutekeleze maelekezo ya kumdhuru Sabaya.

“Akituonesha picha ya Sabaya na maeneo anauyopenda kutembelea. Alituelekeza baada ya kazi ya Sabaya turudi Dar kutekeleza kazi nyingine nyeti kulipua vituo vya mafuta na kushinikiza maandamano ili Serikaki ionekane imeshindwa maana inatuchukia sisi wapinzani.

“Yeye aliondoka kurudi Dar sisi tukabaki kutekeleza kumdhuru Sabaya Tarehe 3 Atosti tulienda eneo la Rao Madukani kwa dada yake Ling'wenya ili kubana matumizi maana Mheshimiwa alituachia Sh150,000

“Tulikamatwa na askari tukituhumiwa kukutwa na dawa za kulevya na kupanga njama za ugaidi. Tuhuma hizo ni za kweli na pia kukutwa na silaha ni za kweli na nilikutwa na simu yangu ya Itel.

“Nilisaini hati ya kuchukuliwa mali na askari nao wakasaini. Nikachukuliwa kwenda Central Moshi. Uthibitisho haya maelezo ni ya kweli kwa saini.

“Muda wa kumaliza kuandika maelezo hayo ilkiuwa ni saa 3"

Wakili wa Serikali Mwandamizi SSA Kidando alimtaka ACP Kingai aelezee alichoelezwa na mshtakiwa huyo wa pili Adamu.

ACP Kingai :Alikiri kukutana na wenzake kwa ajili kwenda kwa Mbowe, alikiri kupewa nauli kwenda Moshi kukutana na Mbowe, alikiri kuwepo Moshi tarehe 24 -26 Julai 2020, alikiri kuwepo yeye na wenzake wawili akiwemo Ling'wenya na mtu mwingine.

“Alikiri tarehe 25 usiku kufanya mkutano yeye na Ling'wenya, Moses Lujenje maarufu Kakobe, Hassan Bwire na Freeman Mbowe"

SSA Kidando: Nini kiliendelea?

ACP Kingai : Alikiri kwenye mkutano alielekezwa na Mbowe kumdhuru DC Sabaya kwa njia yoyote ile.

SSA Kidando: Kitu gani kingine alikueleza?

ACP Kingai: Shahidi pia alikiri kupewa pesa na Mbowe Sh150,000 kukidhi mahitaji hapo Moshi, alikiri Agosti Mosi 2020 alfajiri Mbowe aliwaita tena na kuwapa maelekezo, kwamba wahakikishe wanayafanyia kazi.

“Kumdhuru Sabaya na ili wawe na uhakika Mbowe aliwaonyesha picha ya Sabaya kupitia simu yake, aliwalekeza wamalize kazi hiyo ya Moshi halafu warudi Dar kufanya kazi nyingine nyeti.

“Alitaja kazi hiyo kwamba walipanga wakalipue vituo vya mafuta, lakini pia kufanya vurugu kwenye masoko na maeno ya watu wengi”.
Ulikuwepo mahakamani kinuji au nikunifariji kwa kazi yenu ya ubambikiaji tu.
 
Kabisa mkuu yaani jamaa alieleza straight hakuna chenga onampaka mashahidi wa ukamataji upekuzi mwenyekiti wa mtaa walishuhudia unakwepaje hapo sasa uje useme uliteswa ili useme yaani kibatala kwaakili yake ndogo aliwalisha maneno wadanganye mahakama wakafeli sasaushahidi mwaaaaaaaaaaaaaa gaid jela
Uelekeo wa kesi haupimwi kwa namna hiyo, kuwepo kwa Mwenyekiti sio kila mara kunatoa tafsiri kuwa utaratibu ulifuatwa, nakumbuka mwaka 2015, nikiwa mahakama ya wilaya ya Bukombe. Polisi waliwaleta watuhumiwa wa ujangili wakiwa na nyara za serikali, silaha pamoja na magunia kadhaa ya bangi kama ushahidi.

Polisi waliokuja mahakamani kama mashahidi walieleza kuwa utaratibu wote ulifuatwa, zoezi la upekuzi lilifanyika kwa kumshirikisha mwenyekiti wa kijiji, ila wakati wa "cross examination" kuna askari mmoja aliulizwa ni namna gani waliingia kwenye nyumba ya watuhumiwa, ila kumbuka mashahidi wote waliotangulia walisema walifuata utaratibu na walifunguliwa, lakini askari wa mwisho alisema kuwa waliwaomba watuhumiwa wafungue mlango wakagoma, ndipo yeye alipovunja mlango na kuingia.

Sasa ukiangalia mtiririko wa ushahidi japo walijipanga kwa kuwaleta mashahidi kibao, ila waliteleza sehemu ndogo iliyoharibu kesi kwa upande wa serikali, kesi za jinai unaweza kuwa una kila aina ya ushahidi lakini upande mwingine ukiweza kuonyesha shaka dogo ushahidi wote unakuwa hauna maana kabisa. safari bado ni ndefu ni mapema mno kutabiri mwelekeo wa kesi hii.
 
Back
Top Bottom