Ligi ya mabingwa Africa round ya Kwanza Leo inatimua vumbi Kati mashetani wekundu kutoka Zambia Nkana Red Devils na wekundu wa msimbazi Simba. Mshindi wa jumla katika michezo 2 watakayocheza atafuzu moja kwa moja hatua ya makundi huku atakaeshinda atupwa kwenye kombe la shilikisho barani Africa.
Wachambuzi wa soka barani Africa waipa wanaipa nafasi kubwa kushinda mshezo huu wa Leo kutokana na kuwa na kikosi Bora huku wakitandaza soka maridadi la kuvutia kiasi kufanishwa na kikosi Cha Manchester city.
Simba Leo itawategemea golikipa namba moja wa taifa stars aishi manula, akilindwa na mchezaji kiongozi Paschal Wawa, katikati mkude kotei na Chama watakuwa wakitawala kwa pasi fupi fupi za uhakika na mbele okwi, kagere na Bocco wakiongoza mashambulizi ya uhakika.
Watabiri wa masuala ya kubet wameipa Simba ushindi mnono.
Mchezaji tishio wa Nkana ni Walter Bwalya Simba wamepewa tahadhari ya kuwa makini nae. Pia mtanzania Hasan kessy atakuwa akiiwakilisha Nkana FC
Usikose mtanage huu hapa hapa JF mida ya saa 10 kamili jioni na saa 9 kwa muda wa Zambia
View attachment 968731