Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi Afred Kapala wa tiGO atoa Ushahidi, Kesi kuendelea, Nov 03, 2021

Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi Afred Kapala wa tiGO atoa Ushahidi, Kesi kuendelea, Nov 03, 2021

Chief Hangaya acha kucheza na kodi zetu kabisa sisi kama sisi tunaomba uache kuichezea nchi na kesi zisizo na ukweli kwanza ulitakiwa uanze na yule aliekulisha maneno ya uongo kuhusu hii kesi tena kwa kutangaza hadhani ndio urudi kuifuta................ unajitahidi kufuta makosa ya mwenda lakini unaweka makosa mengine tena yenye aibu zaidi
Hapa bi mkubwa alilishwa tango pori
 
Ikiwa leo ni tarehe 2 November 2021 , kesi hii inayobeba sehemu kubwa ya habari za Tanzania inaendelea tena Mahakamani hapo .

Baada ya ushahidi wa Muuza Mbege wa Rau Kukamilika , Leo upande wa Jamhuri utaleta shahidi wa Tano miongoni mwa wale 24 waliopangwa kutoa ushahidi huo .

Kama kawaida JF itakuletea moja kwa moja kesi hii kutoka Mahakamani , usiondoke .

===========

Jaji ameingia Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Imeshatajwa

Wakili wa Serikali Robert Kidando Anatambulisha

1.Pius Hilla
2.Nassoro Katuga
3,Abdallah Chavula
4.Ester Martin
5.Jenitreza Kitali
6.Tulimanywa Majige

Kibatala anatambulisha Jopo lake

1. Michael Mwangasa
2.Seleman Matauka
3.Nashon Nkungu
4.Alex Massaba
5.Michael Lugina
6.Maria Mushi
7.Hadija Aron
8.Dickson Matata
9.Jonathan Mndeme
10.Fredrick Kihwelo
11. John Malya

Jaji Mashtakiwa 1,2,3 na 4 Wananyanyuka kuashiria uwepo wao

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tunashahidi Mmoja Kwa Leo Lakini Kabla ya Kuendelea Leo tuna ombi, Na Maombi yetu yatamuhusu Shahidi Wa Leo Mheshimiwa

Jaji: Wakati wa Kufile Mashahidi tuliorodhesha Majina Kama Frank Kapala

Jaji: Ndiyo

Wakili wa Serikali: na Kule Kwenye Comito Proceedings Katika Ukusara wa 32 wa zile proceeding za Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zilitaja Kama Frank Kapala Lakin kama tulivyo leta information Barua ya 11 August 2021 Ndiyo alitaja kama Frank Kapala Mheshimiwa Jaji Kwa Usahihi ....Shahidi huyu anaitwa Frank kapara.

Wakili wa serikali: Kwa hiyo tunaomba Kumbukumbu sahihi za Mahakama zi-note kama Frank Kapara Kwa kifungu 264 Sura ya 20 cha CPA Rev Ya 2009 Na Kwa sababu Ushahidi wa Shahidi huyu ulisomwa wakati wa Comito Proceedings tunaomba turuhusiwe Kuendelea na Shahidi huyu.

Jaji: Kifungu gani?

Wakili wa Serikali: 264 Sura ya 20 kama Ilivyofanyiwa marekebisho Mwaka 2009

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Maombi yetu ni hayo tu

Mtobesya: Tumesikia Maombi ya Upande wa Mashitaka na Kwa sababu Wanasema Substance ndiyo Iliyo contain Ushahidi Wake tangu Maelezo yake Polisi. Kwa Upande wetu hatuoni Kama inaathiri Haki za Mteja wetu, Hatupingi hilo Ombi Kwa niaba ya Mshitakiwa Wa Kwanza, Asante.

Wakili John Mallya: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili hatuna Pingamizi.

Wakili Fredrick Kihwelo: hatuna Pingamizi Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu.

Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi Kwakuwa wameleta Maombi Rasmi.

Jaji: Samahani Kidogo, Unachotaka Kirekebishwe Unaweza Ku-Spell

Wakili wa Serikali: FREDY KAPALA

Jaji: Basi maombi ambayo yameletwa Kurekebisha Kumbukumbu za Mahakama Kuwa Shahidi alikuwa Frank Kampala na Sasa atafahamika kuwa ni FREDY Kapala Na hiyo ndiyo Itakuwa kumbukumbu Mpya ya Mahakama, NATOA AMRI. Mawakili wote Wananyuka na Kukubaliana na Jaji.

JAJI: Shahidi aletwe sasa

Wakili wa Serikali: Ameenda Kuitwa

Jaji: Anakuwa Shahidi Wa Ngapi huyo

Wakili wa Serikali: Shahidi 05

Jaji: Utetezi Ndiyo..?

Kibatala: Ndiyo

Jaji: Majina yako

Shahidi: Naitwa Afredy Kapala

Jaji: Umri

Shahidi: 38yr

Jaji: kabila

Shahidi: Mpare

Jaji: Shughuli yako

Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya Tigo

Jaji: Dini yako

Shahidi: Mkristo

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni Kweli, kweli tupu Eenheeeee Mwenyezi Mungu nisaidie.

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Wakili Nasorro Katuga atamuongoza

Wakili wa Serikali Nasorro: Nitakuuliza Maswali

Wakili wa Serikali: Umesema Unashughulika na nini?

Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya kibiashara inaitwa TIGO

Wakili wa Serikali: Kwanini Unasema Kampuni ya kibiashara

Shahidi: Kwa sababu kampuni iliyosainiwa Brela ni MIC Tanzania

Wakili wa Serikali: Jina la Kibiashara ndiyo

Shahidi: Tigo

Wakili wa Serikali: Kampuni ya MIC Tanzania Ltd Inafanya Shughuli gani?

Shahidi: Mawasiliano ya Simu pamoja na Mihamala ya Kifedha

Wakili wa Serikali: Mwambie Mheshimiwa Jaji Umeajiriwa lini

Shahidi: March Mwaka 2012

Wakili wa Serikali: Umeajiriwa kama nani?

Shahidi: Kama Mwanasheria wa Tigo

Wakili wa Serikali: Katika Kitengo Kipi

Shahidi: Kitengo cha Sheria

Wakili wa Serikali: Umesema Kampuni yako inajishughulisha Kutoa Mawasiliano ya Simu na Mihamala ya kifedha Iambie Mahakama kwa nani?

Shahidi: Kwa Wateja Ambao wanamiliki line za Mitandao ya Simu

Wakili wa Serikali: Hawa wateja Wa Tigo Wanapatikana Vipi?

Shahidi: Wanapatikana Kwa Kununua line za Tigo na Wakaitumia basi Wanakuwa Wateja wetu. Na ili ifanye kazi lazima ifanyiwe Usajili.

Wakili wa Serikali: Kwenye Kusajili mnasajili Kitu gani?

Shahidi: Kwa mtu ambaye ana kitambukisho cha NIDA tunatumia NATIONAL IDENTIFICATION NUMBER. Mtu anaye sajili ataingiza Namba ya Kitambulisho Cha Taifa Itasoma Taarifa.

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama process za Manunuzi ya Line kama zipo?

Shahidi: Mtu yoyote anaweza Kufika kwenye Duka au sehemu ambayo kuna Wakala anauza hizo line za Tigo akiwa na Kitambulisho Cha Taifa, Lakini pia Kuna Wageni ambao wanatakiwa kutumia passport....

Wakili wa Serikali: Mtu anaye jua atafanya nini?

Shahidi: Ataweke Kidole Kigumba, Zitasoma Taarifa zote ambazo zipo Kwenye NIDA, Kama Jina Na tarehe ya kuzaliwa Kwa hiyo Taarifa hiyo itachukuliwa Na kuhifadhiwa Kwenye Mfumo wa Tigo kama Taarifa za Owner au Mtumiaji wa hiyo line.

Wakili wa Serikali: Mtu asiyejua NIDA, unaposema Zinaenda Kutally na Taarifa za NIDA unamaanisha Nini?

Shahidi: NIDA nimfumo wa Usajili wa Vitambulisho Vya Taifa ambao unatunzwa na Authority

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama unaposema Taarifa zile zitachukukiwa na Kuhifadhiwa Tigo, Nani atazichukua

Shahidi: Tunasema Ki Electronic kuna Mfumo wetu ikizipata na Ikatally inatunza Kwetu, Kwa hiyo Mifumo inawasiliana

Wakili wa Serikali: Jinsi ya Kusajili line Taratibu ziko Vipi

Shahidi: Ukishanunua Laini na Kwamba wewe sasa Unawasiliana, Tuna kutumia Meseji Kuwa kama Unataka Kutumia huduma ya Mihamala ya Fedha, Ukisema Okey tunakupa Vigezo na Masharti.

Wakili wa Serikali: Hiko Kitendo Mnakiitaje?

Shahidi: Umejiregister Kwenye Huduma ya Tigopesa

Wakili wa Serikali: Nikurudiahe kwako sasa wewe Mwenyewe, Tigo Umeajiriwa kama Mwanasheria Je Majukumu yako ni Yapi

Shahidi: Kushauri Viongozi Maswala Yanayohusu Sheria, Kutengeneza Kusoma, kupitia na Kusaini Mikataba Kufuatilia, Kusimamia Kesi zote zinazohusiana na Tigo ...Kumsaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama Katika Kupata Taarifa Mbalimbali Kutoka kwa Wateja zinapohitajika.

Wakili wa Serikali: Jingine, Baada ya kutoa hizo Taarifa

Shahidi: Kama Kuna Jinsi Yoyote Kusaidia Chombo chochote Katika Kutafuta Taarifa, Naweza Kusaidia Siyo VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama tu Bali hata Mtu Binafsi anaweza kupata Msaada wangu.

Wakili wa Serikali: Ni Vipi Mtu Binafsi, Mtu X anaweza kupata Taarifa za Mtu Y

Shahidi: Mtu Mmoja Kupata Taarifa za mtu Mwingine HAIWEZEKANI

Wakili wa Serikali: Kwa mujukumu hayo uliyoyataja, Unamajukumu gani au Ujuzi gani inayo Kusaidia katika Kutekeleza Majukumu yako

Shahidi: Kama Mwanasheria wa kampuni Nina Digrii ya Sheria, Nimesomea India JSS law college. Under MYSORI University, Ambayo niliipata 2009 Nilisoma Pia Advanced Computer Course, MYSORI University India 2007. Nilisoma Pia Advanced Diploma in Practice Nilimaliza Mwaka 2012 Baada ya hapo Kuna Training mbalimbali ambazo Nimezipata Nikiwa kazini 2012 nilipoanza Kazi

Wakili wa Serikali: Zitaje Training gani

Shahidi: Nilipopata kazi ilikuwa ni Majukumu yangu Nilikuwa nimeingia Kampuni ya Telecom Nilipata Training Ya Mwezi na nusu

Wakili wa Serikali: Ulisomea nini ktk hiyo Training

Shahidi: Mifumo ya Kujifunza Kutumia, ilikupata Taarifa Wa kwanza ni oracle Wa Kusaidia Kupata Taarifa mbalimbali zilizopo Sehemu za Kazi.

Shahidi: Kuna system Nyingine ambayo CONVIVER iliyokuwa Inasaidia Kupata Mihamala Yote ni soft ware BILL QUERY Iilikuwq Inasaidia Kujua matumizi Mbalimbali ya Mteja Upande wa Vocha Na SMAP ni Mfumo Sawa QUERY Kwa hiyo nilikuwa nasaidia VYOMBO Vya Ulinzi Na Usalama Kupata ...Information

Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka Ulikuwa unafanyiwa na nani

Shahidi: Ofisini na Mtu anaitwa Mr.....

Wakili wa Serikali: Ofisi za Tigo ziko wapi

Shahidi: Ofisi za Tigo Zipo Makumbusho DERM COMPLEX

Wakili wa Serikali: Unakumbuka Training Nyingine

Shahidi: 2015 palikuwa na Training Nyingine Baada ya Mifumo Kubadilika Baada ya oracle ikaja SQL Server CONVIVER ikaja Kubadirishwa Ikaja TELVIVER IKAJA ENVIVER ambayo sasa Ikaja Information Mbayo Ukiingia Unaona Matumizi ...na Kila Kitu. Wanakufundisha Kule Unakoenda Kuchukua zile Information Siyo Kila amtu anaruhusiwa Kwenda Kuchukua Unafundishwa Jinsi gani ya Kuzilinda.

Wakili wa Serikali: Baada ya Mifumo Kubadilika sasa

Shahidi: Ikabidi tupate Training, Jinsi zinavyofanya kazi na Tabia zake

Wakili wa Serikali: Katika Training zako ulipata Lolote Kuhusiana na Information ambazo unaenda kufanyia Kazi

Shahidi: Wanakufundisha General Overview

Wakili wa Serikali: Umetaja Training za 2012 na 2015 Je una Training Nyingine

Shahidi: Zipo Nyingine hizo ni Major Kila Siku Dunia Ikileta System Mpya tutaambiwa tu Kuna Training za Kila Siku Katika Majukumu ya kazi

Wakili wa Serikali: Nikurudishe Nyuma Wakati Unataja Majukumu Yako Unasema Unasaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama. Je Ni VYOMBO gani

Shahidi: VYOMBO Vyote Vya Usalama Ukijumlisha Polisi, Jeshi, Kama ni Anga kama ni Ardhi na VYOMBO Vyote Vinavyofanya Uchunguzi wa Kisayansi. 2.Taarifa za Mihamala ya Fedha, Kutuma na Kupokea fedha 3. Kuna Recharge ya Vocha na Kutumia pamoja na Matumizi yake 4. Taarifa za Usajili 5. Taarifa Nyingine zote zinazoambatana Kama NIDA, LOCATIONS, BILL MBALIMBALI ANAZOLIPA

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama sasa Unawasaidia Kuwapa Taarifa, Je ni Taarifa zipi Mnawapa, ulikuwa unatumia Neno zinazoruhusiwa Kisheria

Shahidi:
Zozote ambazo zitakuwa zinahitajika sisi tunazo 1.Kuna Kupiga na Kupokea Simu, Za wateja wetu zinaitwa Call Details ...

Wakili wa Serikali: Shahidi Iambie Mahakama Hizo Taarifa wewe unazitoa wapi

Shahidi:
(Tigo) Taarifa zote za kampuni pamoja na Wateja wake Zinakuwa Stored Kwenye Server

Wakili wa Serikali:
Iambie Mahakama Nani anaitoa Taarifa kwenye Server

Shahidi:
(Tigo) Taarifa zote Zinakuwa Served Automatically Mtu anapo piga Simu Mnara Unasima na Taarifa zinashuka na Zina switch kwenda Automatically Kwenda Kwenye Server Kuwa stored. Lakini pia Kuna watu ambao ni Observers wa kungalia na Ku Audit kazi Nzima ya Server

Wakili wa Serikali:
hizo Taarifa unazozitoa Unasema Zinakuwa self Generated, Je kiuadilifu kuwa hizi ni zile zilizojitengeneza, Uadilifu wake kwenye Server?

Shahidi: (Tigo) Kama kampuni ina Mifumo ya tofauti ilitengenezwa Mahususi Kulinda hizi Server na The Whole System
mbowe akifungwa upinzani utaendelea vizuri mbowe asipofungwa hakuna upinzani

Mbowe ndiye anaua upinzani kipindi cha korona ndipo chadema ilipokufa

Mbowe akiondolewa tu tiari upinzani unachukua nchi

Tunaitaji mawazo mapya na watu wapya hii mbowe ya kuwa kiongoxi miaka 25 inatudisha upinzani nyuma sana
 
Yeah... Ile kesi ndogo iliwachanganya zaidi upande wa utetezi...
 
1635841932580.png
 
Vijana wa chaggadomo, utasikia MIHAMALA🤣
 
Back
Top Bottom