Habari Wakuu,
Leo
09/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 9, 2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
- Wakili Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Ignasi Mwinuka
- Mawakili Wa Serikali Waandamizi
- Wakili Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na
- Wakili Michael Mwangasa
- Gaston Garubindi
- Evaresta Kisanga
- Maria Mushi
- John Masoud kwa Niaba ya Nashon Nkungu
- Clinton Kipengele Kwa niaba ya John Mallya
- Fredrick Kihwelo
- Dickson Matata
Jaji: anaandika, Kisha anaita Majina ya Mshitakiwa wote Wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili Kuendelea Kusikilizwa na tupo tayari Kuendelea
Peter Kibatala: Nasi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea
Shahidi anapanda kisha anasimama Kizimbani Jaji anaandika Kidogo
Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo
Shahidi: Sawa Mheshimiwa, Ila kuanzia Jana Jioni hali yangu haikuwa Nzuri lakini nitaendelea Kutoa Ushahidi
Kibatala: Good Morning Inspector
Shahidi: Morning
Kibatala: Nafikiri Unakumbuka Jana tulikuwa kwenye Swala la Mbowe Kuanzisha Ugaidi
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Tulijadili Mpaka Pale ambapo Washitakiwa Walikutana pale Morogoro na Luteni Denis Urio
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Upelelezi wako Uligundua hivyo
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Na aliye Waita pale alikuwa ni Luteni Denis Urio
Kibatala: Na Utakubaliana na Mimi Kuwa Mpaka Mshitakiwa Wa Kwanza, Wapili na watatu anakutana na Denis Urio Mbowe alikuwa hawajui na hajawahi Kukutana nao
Shahidi: sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana Walikuwa wanafanya Shughuli zao halali
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni sahihi Kwamba Luteni Denis Urio aliwaita Morogoro Kwa sababu Yeye Makazi yake yalikuwa Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwa namna yoyote Ile Freeman Mbowe Hakuwahi kuwa Morogoro kabla na baada ya hizo Tarehe walizokutana Morogoro
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Uliwahi Kugundua Kwa wewe Kuwa Pro Active au Kuhalifiwa na Luten Denis Urio Kwamba kabla ya Mohammed Ling'wenya Kuondoka Mtwara Kuja Morogoro, ilibidi awasiliane na Mzee Ling'wenya Kupata Ruhusa
Shahidi: Sikuwahi Kufahamu
Kibatala: Pia hufahamu Luteni Denis Urio alitoa Ushahidi Mahakamani akithibitisha
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo hata nikikwambia Kwamba Mzee Ling'wenya ilibidi aitishe Kikao cha Ukoo/Familia Kujadili suala la Mtoto wao Kwenda Kwa Luteni Denis Urio
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Pia ufahamu Kwamba Wakati Wanamtoa Walimtoa Kwa Uangalizi Kwamba Wanamkabidhi Kwa Luten Denis Urio na Kwa Freeman Mbowe, Kwa sababu ni watu wanao aminika
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Fafanua tena
Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio, alikutana na Makundi Mawali Kwa wakati tofauti
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: aliyewaambia Bwire na Moses Lijenje na aliyewaambia Adamoo na Ling'wenya alikuwa ni Luteni Denis Urio, Je ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unaposema Kwamba alipo wasiliana na Mbowe aliwasiliana Meseji, Telegram au Simu
Shahidi: Kwa Njia ya Mdomo na Pia kwa Njia ya Mawasiliano ya Jumbe za Telegram
Kibatala: Walipoongea Denis Urio na Freeman Mbowe wewe Ulikuwepo
Shahidi: Sikuwepo
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Ulishawahi Kusikia Neno Maarufu la Kiupelelezi la "Your Word against Mine"
Shahidi: Sijui
Kibatala: Kwa kuwa Wewe, Kingai, DCI hamkuwepo Wakati Mbowe anaongea na Urio
Shahidi: Hatukwepo lakini tulifanya Upelelezi
Kibatala: Watu Wawili wamezungumza, Na DCI hakuwepo, Kingai hakuwepo, na wewe hukuwepo Je si lazima sasa Tupime Maneno ya Denis Urio na Freeman Mbowe
Shahidi: Siyo lazima, Unaweza Kufanyia Kazi Maneno ya Denis Urio
Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Wakati Denis Urio anakutajia Kuwa Kuna Cassa Motel, Je Uliwahi Kwenda hata Kuthibitisha
Shahidi: Sijawahi Kwenda
Kibatala: Mgahawa ambao Denis Urio alitaja Wamekutana na Mbowe Wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Urio aliwahi Kukwambia Kwamba alipanda Tax Mgulani
Shahidi: sikwenda
Kibatala: Je aliwahi Kukwambia Kwamba alikuwa Mjini alipanda bodaboda
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je Uliwahi Kufika Kuona Kama Kuna Kituo cha Bodaboda
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Uliwahi Kwenda Cassa Motel Kuthibitisha Kama Gari ya Denis Urio lilifika pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Uliwahi Kwenda Mgulani Kuthibitisha Kwamba Denis Urio aliwahi Kufika na Kuishi Pale
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Nyie Kama Polisi mkipata Taarifa Mnairekodi au Kufanyia kazi
Shahidi: Tunafanya kazi
Kibatala: Je wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda 14 July 2020 Kule Ngerengere 92 KJ Ka kweli alikuwa kazini
Shahidi: Sikwenda
Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Baada tu ya Kurejea Kutoka Darfur alikamatwa Kikosini baada ya Kutajwa na Adam Kasekwa
Shahidi: Sifahamu nilifanya Uchunguzi
Kibatala: Kwakuwa umechunguza Kule 92 KJ uliongea na nani
Shahidi: Nisha sema Sikwenda
Kibatala: Kwa hiyo wewe hata 92KJ hufahamu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Makampuni ya Simu yanatunza Kumbukumbu za Mawasiliano
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Je Yanatunza Kwa Muda gani
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Je Wewe Kama Mpelelezi Uliomba Taarifa za Call Recordings katika Makampuni ya Simu Kati ya Freeman Mbowe na Denis Urio
Shahidi: Ndiyo Niliomba
Kibatala: Kwa Barua ya Tarehe Ngapi
Shahidi: Kwa Barua ya 13 August 2020
Kibatala: kwenda Kampuni gani
Shahidi: Kwenda Kwenye Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao
Kibatala: Kwa Inspector Ndowo?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo wewe Uliomba Taarifa Kwa Inspector Ndowo, Je yeye ndiye Mwenye Kuhifadhi
Shahidi: Yeye Ndiye aandike Barua kwenda Tigo na Airtel
Kibatala: kwa hiyo wewe Pamoja na Mambo yote Uli Mwomba Na Rekodi za Mawasiliano ya simu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je wewe Uliona Katika Barua yake kutoka Kwenu Terms of reference suala la Call Recordings lipo
Shahidi: Halipo
Kibatala: kwa hiyo Mliomba au Hamkuomba
Shahidi: Hatukuomba
Kibatala: Uwe sasa inasililiza kwa Makini.. Haya Unafahamu Kuhusu Sheria ya EPOCA