Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022

Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022

Mheshimiwa Nyendo ikikupendeza naitwa Farolito nipo na jopo la wana JF wapenda haki tupo tayari kuifuatilia kesi ya Mchongo mpaka mwisho.
Asante
 
Nipo nafasi ya kwanza leo. Wapi Mzee Mgaya johnthebaptist [emoji31]
Mkuu, nimechungulia mpaka chumba namba 36,sijamuona Mzee Mgaya!
Tetesi za chini ya kapeti zinadai, leo kama shahidi Swila akiwahi kumaliza kutoa ushahidi, anapanda yeye kizimbani, na anadai yeye ana ushahidi mzito kuliko hata wa Afande Sirro!
Tunaye mtakia mema Mwenyekiti Mbowe, tujiandae kisaikorojia!
 
Kesi zote huwa Ni pattern mkuu, maana hakim hakuwepo na mawakili hawakuwepo wakati wa matukio, kwa hyo wakiunga dot ndo wanapata majib, mkuu mbona Jambo rahisi tu hili??
Unajua maana ya kuunga unga dots?....kwa kesi kama hi huyu swila alipaswa kua na straight forward evidance ndo ailete mahakamani, evidance inayohitajika ili mtu awe convicted kwa aina ya kesi hi kwa lugha ya kisharia inaitwa watertighen evidance ambao hawana, wali kurupuka kumlaghai Raisi ili wapate vyeo, kwa ushahidi wa dots hi kesi haina hadhi kusikilizwa na kupoteza mali za Ummah
 
Hii kesi angekuwepo;

1) Tundu Lissu
2) Peter Kibatala
3) Nashon Nkungu
4) Fredrick Kihwelo.
5) Mtobesya.
6) John Malya.
7) Fatma Karume.

Jopo la mawakili watetezi lingekua poa sana, mashahidi wangeshikwa matumbo ya kuharisha.
YAANI huwa hata hamtumii akili hivi kweli mashahidi woote hao wanatoa ushahidi kama kesi ingekuwa ya kutengeneza ingeishia njiani tena mapema sana na hivi vitu inaonekana kabisa ni vya muda mrefu ukianza kuhusisha katiba mpya na ugaidi wa mbowe na ushahidiunaotolewani tofauti maana ya kwamba wakati anakamatwa mbowe na mkaanza kusema kakamatwa kwaa jili ya katiba mpya huo ushahidi tayari ulishakusanywa muda mrefu na wakati huo kina komandoo wapo ndani muda mrefu na mbowe aliwatelekeza hakuna mtu alikuwa anawafuatilia HIVI LEO UJE USEME KESI YA MCHONGO ? yaani mbowe hawezi kushindana na serikali kwa ushahidi uiokusanywa na serikali ikishindwa hii kesi watakuwa wameshindwa kizembe mbowe hachomoki wanachootakiwa kuchutama mambo yaishe wakikomaza shingo mtu anaumia hivihivi na wakitegemea rufaa ndiyo hakuna kitu kabisa
 
Habari Wakuu,

Leo 09/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.

Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki:Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 9, 2022

Baki nami.

Updates:


Jaji ameingia Mahakamani Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
  • Wakili Pius Hilla
  • Abdallah Chavula
  • Jenitreza Kitali
  • Nassoro Katuga
  • Esther Martin
  • Ignasi Mwinuka
  • Mawakili Wa Serikali Waandamizi
  • Wakili Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na
  • Wakili Michael Mwangasa
  • Gaston Garubindi
  • Evaresta Kisanga
  • Maria Mushi
  • John Masoud kwa Niaba ya Nashon Nkungu
  • Clinton Kipengele Kwa niaba ya John Mallya
  • Fredrick Kihwelo
  • Dickson Matata
Jaji: anaandika, Kisha anaita Majina ya Mshitakiwa wote Wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili Kuendelea Kusikilizwa na tupo tayari Kuendelea

Peter Kibatala: Nasi pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea

Shahidi anapanda kisha anasimama Kizimbani Jaji anaandika Kidogo

Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo

Shahidi: Sawa Mheshimiwa, Ila kuanzia Jana Jioni hali yangu haikuwa Nzuri lakini nitaendelea Kutoa Ushahidi

Kibatala: Good Morning Inspector

Shahidi: Morning

Kibatala: Nafikiri Unakumbuka Jana tulikuwa kwenye Swala la Mbowe Kuanzisha Ugaidi

Shahidi: Sahihi

Kibatala: Tulijadili Mpaka Pale ambapo Washitakiwa Walikutana pale Morogoro na Luteni Denis Urio

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Ni sahihi Kwamba Upelelezi wako Uligundua hivyo

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Na aliye Waita pale alikuwa ni Luteni Denis Urio

Kibatala: Na Utakubaliana na Mimi Kuwa Mpaka Mshitakiwa Wa Kwanza, Wapili na watatu anakutana na Denis Urio Mbowe alikuwa hawajui na hajawahi Kukutana nao

Shahidi: sahihi

Kibatala: Ni sahihi Kwamba kabla ya Kukutana Walikuwa wanafanya Shughuli zao halali

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Ni sahihi Kwamba Luteni Denis Urio aliwaita Morogoro Kwa sababu Yeye Makazi yake yalikuwa Morogoro

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Kwa namna yoyote Ile Freeman Mbowe Hakuwahi kuwa Morogoro kabla na baada ya hizo Tarehe walizokutana Morogoro

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Uliwahi Kugundua Kwa wewe Kuwa Pro Active au Kuhalifiwa na Luten Denis Urio Kwamba kabla ya Mohammed Ling'wenya Kuondoka Mtwara Kuja Morogoro, ilibidi awasiliane na Mzee Ling'wenya Kupata Ruhusa

Shahidi: Sikuwahi Kufahamu

Kibatala: Pia hufahamu Luteni Denis Urio alitoa Ushahidi Mahakamani akithibitisha

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Kwa hiyo hata nikikwambia Kwamba Mzee Ling'wenya ilibidi aitishe Kikao cha Ukoo/Familia Kujadili suala la Mtoto wao Kwenda Kwa Luteni Denis Urio

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Pia ufahamu Kwamba Wakati Wanamtoa Walimtoa Kwa Uangalizi Kwamba Wanamkabidhi Kwa Luten Denis Urio na Kwa Freeman Mbowe, Kwa sababu ni watu wanao aminika

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale

Shahidi: Fafanua tena

Kibatala: Ulikuwa unafahamu Kwamba Luteni Denis Urio, alikutana na Makundi Mawali Kwa wakati tofauti

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Baada ya Kuwa wamekutana Luteni Denis Urio na Khalfani Bwire na Moses Lijenje na Baadae Kundi la Pili Adam Kasekwa Mbowe Hakuwahi Kutia Neno katika yale yaliyo kuwa yanajadiliwa pale

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: aliyewaambia Bwire na Moses Lijenje na aliyewaambia Adamoo na Ling'wenya alikuwa ni Luteni Denis Urio, Je ni sahihi

Shahidi: Ni sahihi

Kibatala: Unaposema Kwamba alipo wasiliana na Mbowe aliwasiliana Meseji, Telegram au Simu

Shahidi: Kwa Njia ya Mdomo na Pia kwa Njia ya Mawasiliano ya Jumbe za Telegram

Kibatala: Walipoongea Denis Urio na Freeman Mbowe wewe Ulikuwepo

Shahidi: Sikuwepo

Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Ulishawahi Kusikia Neno Maarufu la Kiupelelezi la "Your Word against Mine"

Shahidi: Sijui

Kibatala: Kwa kuwa Wewe, Kingai, DCI hamkuwepo Wakati Mbowe anaongea na Urio

Shahidi: Hatukwepo lakini tulifanya Upelelezi

Kibatala: Watu Wawili wamezungumza, Na DCI hakuwepo, Kingai hakuwepo, na wewe hukuwepo Je si lazima sasa Tupime Maneno ya Denis Urio na Freeman Mbowe

Shahidi: Siyo lazima, Unaweza Kufanyia Kazi Maneno ya Denis Urio

Kibatala: Wewe Kama Mpelelezi Wakati Denis Urio anakutajia Kuwa Kuna Cassa Motel, Je Uliwahi Kwenda hata Kuthibitisha

Shahidi: Sijawahi Kwenda

Kibatala: Mgahawa ambao Denis Urio alitaja Wamekutana na Mbowe Wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda

Shahidi: Sikwenda

Kibatala: Je Urio aliwahi Kukwambia Kwamba alipanda Tax Mgulani

Shahidi: sikwenda

Kibatala: Je aliwahi Kukwambia Kwamba alikuwa Mjini alipanda bodaboda

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je Uliwahi Kufika Kuona Kama Kuna Kituo cha Bodaboda

Shahidi: Sikwenda

Kibatala: Je Uliwahi Kwenda Cassa Motel Kuthibitisha Kama Gari ya Denis Urio lilifika pale

Shahidi: Sikwenda

Kibatala: Uliwahi Kwenda Mgulani Kuthibitisha Kwamba Denis Urio aliwahi Kufika na Kuishi Pale

Shahidi: Sikwenda

Kibatala: Nyie Kama Polisi mkipata Taarifa Mnairekodi au Kufanyia kazi

Shahidi: Tunafanya kazi

Kibatala: Je wewe Kama Mpelelezi Uliwahi Kwenda 14 July 2020 Kule Ngerengere 92 KJ Ka kweli alikuwa kazini

Shahidi: Sikwenda

Kibatala: Je Unafahamu Kwamba Baada tu ya Kurejea Kutoka Darfur alikamatwa Kikosini baada ya Kutajwa na Adam Kasekwa

Shahidi: Sifahamu nilifanya Uchunguzi

Kibatala: Kwakuwa umechunguza Kule 92 KJ uliongea na nani

Shahidi: Nisha sema Sikwenda

Kibatala: Kwa hiyo wewe hata 92KJ hufahamu

Shahidi: Sifahamu

Kibatala: Unafahamu Kwamba Makampuni ya Simu yanatunza Kumbukumbu za Mawasiliano

Shahidi: Nafahamu

Kibatala: Je Yanatunza Kwa Muda gani

Shahidi: Sikumbuki

Kibatala: Je Wewe Kama Mpelelezi Uliomba Taarifa za Call Recordings katika Makampuni ya Simu Kati ya Freeman Mbowe na Denis Urio

Shahidi: Ndiyo Niliomba

Kibatala: Kwa Barua ya Tarehe Ngapi

Shahidi: Kwa Barua ya 13 August 2020

Kibatala: kwenda Kampuni gani

Shahidi: Kwenda Kwenye Kitengo Cha Uchunguzi Wa Makosa ya Mtandao

Kibatala: Kwa Inspector Ndowo?

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Kwa hiyo wewe Uliomba Taarifa Kwa Inspector Ndowo, Je yeye ndiye Mwenye Kuhifadhi

Shahidi: Yeye Ndiye aandike Barua kwenda Tigo na Airtel

Kibatala: kwa hiyo wewe Pamoja na Mambo yote Uli Mwomba Na Rekodi za Mawasiliano ya simu

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Je wewe Uliona Katika Barua yake kutoka Kwenu Terms of reference suala la Call Recordings lipo

Shahidi: Halipo

Kibatala: kwa hiyo Mliomba au Hamkuomba

Shahidi: Hatukuomba

Kibatala: Uwe sasa inasililiza kwa Makini.. Haya Unafahamu Kuhusu Sheria ya EPOCA
Wakili Msomi Peter (Kepha- Mwamba), Utembee daima chini ya uvuli wa Mkono wa Mungu. Neema na Baraka Zake Mungu Mwenyezi zikushukie na kukaa nawe na timu nzima ya Makamanda (Mawakili wa upande wa utetezi) wako daima. Amin
 
Jamaa Kibatala kama Simba anamlia timing vibaya sana jana kampeleka kirafiki leo naona anafanya finishing ya kufa mtu.
unajuwa sheria ukiwa unaijuwa sana huwezi kushindana na mtu ambaye hajui sana sheria na ndiyo maana kuna mengine wakati wa upelelexi wake hakuyafanya shahidi kazi yake ndogo sana kusema alichokipelelezasiyo kuanza kuainisha vipengele vya sheria anaema alichokipeleleza na alichogundua kwenye upelelzi wake kibatala analazimisha vit visivyowezekana ni sawa na mtoto mdogo umwambie atoe ushahidi wa tukio akaongea alichokishuhudia halafu uanze kumuuliza masawali ya PGO hataweza kuyasema lakini ukweli kausemautamshindaje hapo?mbowe hachomoki
 
Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo

Shahidi: Sawa Mheshimiwa, Ila kuanzia Jana Jioni hali yangu haikuwa Nzuri lakini nitaendelea Kutoa Ushahidi
sasa leo si ndo utakufa kabisa, Maana Wakili Msomi Kibatala leo ana maswali 999 bado mawakili wengine !
Mwonezi anataka huruma ya jaji, utavuna ulichokipanda bwana Inspector, Kazi ni kwako.......
 
Wakili Msomi Peter (Kepha- Mwamba), Utembee daima chini ya uvuli wa Mkono wa Mungu. Neema na Baraka Zake Mungu Mwenyezi zikushukie na kukaa nawe na timu nzima ya Makamanda (Mawakili wa upande wa utetezi) wako daima. Amin
shabiki ni kitu kibaya sana asiye juwa sheria unaweza ukafikili kibatala kuna la maana analolifanya hapo huyo ni mjanja wa maneno tu lakini hakuna anachokifanya kumuokoa mbowe anachokifanya ni kupoteza muda kwa maswali yasiyoisha kumchanganya shahidi hivi muda wote watu wawe walikuwa wanapanga kuchonga kesi ya kumfunga mbowe? siyo kweli makosa kafanya kweli na mwenzenu uko tayari kutoka lakini mmekomaza shingo kuwa hana makosa mwenzenu anateseka maana anajuwa alichokifanya
 
YAANI huwa hata hamtumii akili hivi kweli mashahidi woote hao wanatoa ushahidi kama kesi ingekuwa ya kutengeneza ingeishia njiani tena mapema sana na hivi vitu inaonekana kabisa ni vya muda mrefu ukianza kuhusisha katiba mpya na ugaidi wa mbowe na ushahidiunaotolewani tofauti maana ya kwamba wakati anakamatwa mbowe na mkaanza kusema kakamatwa kwaa jili ya katiba mpya huo ushahidi tayari ulishakusanywa muda mrefu na wakati huo kina komandoo wapo ndani muda mrefu na mbowe aliwatelekeza hakuna mtu alikuwa anawafuatilia HIVI LEO UJE USEME KESI YA MCHONGO ? yaani mbowe hawezi kushindana na serikali kwa ushahidi uiokusanywa na serikali ikishindwa hii kesi watakuwa wameshindwa kizembe mbowe hachomoki wanachootakiwa kuchutama mambo yaishe wakikomaza shingo mtu anaumia hivihivi na wakitegemea rufaa ndiyo hakuna kitu kabisa
Hivi Kuna ushahidi gani uliouona wewe zaidi ya hearsay? Ushahidi hauwi kitu kimoja ni lazima kuwe na corroboration ya ushahidi ili kesi iwe prima facie.Sijaona ushahidi unaothibisha jinai hapa.Maneno tu yasiyothibitishwa ndo ugaidi! Hakuna kitu hapo. Hata kikao cha pamoja watuhumiwa wote hakionekani.
 
Back
Top Bottom