Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022

Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022

Ukisikio vioja mahakamani ndio hii sasa, Inspector Swila hali tete, waache wakampange upya Ila mpaka sasa ukweli tumeshaujua.
 
Nilijua utaumwa ila sikukwambia baba tangu ulivyoamka nilikuona tu uso ilijikunja kama unakunya maarage mazima
 
Mwenye macho aambiwi Tazama Kuna msemo usemao

The search for truth takes you where the evidence leads you, even if, at first, you don't want to go there..

Haya ya Kibatala kamkalisha shahidi sijui shahidi Urio wa Mchongo asee

Hapa ilibidi Njia za ziada na sahihi kutumika katika kuhakikisha Mbowe hafungwi,

Story za akina Hilda na Yule Martin Masese Mtandaoni msiridhike nazo.

Kama unajiamini saanaa pinga nayodokeza.

Tunamweka Matatizoni Mbowe Badala ya Kumtetea tunaleta Mbwembwe kwenye kesi ya Msingi.

Mbowe Omba msamaha yaishe hata kama hatuna uhakika na kosa lako.

Sisemagi Mengi ntafufua huu Uzi in two months to come
 
Mwenye macho aambiwi Tazama Kuna msemo usemao

The search for truth takes you where the evidence leads you, even if, at first, you don't want to go there....
Leo umeandika andiko la kipuuzi kupitiliza. Aombe msamaha kwa kosa gani gani hasa?

Kutafuta walinzi wa kumlinda dhidi ya maadui zake ndiyo kumfanye aombe msamaha? Acheni kujitoa ufahamu bhana.

Watanzania wengi tunafuatilia hii kesi kwa ukaribu sana, ili tuone mwisho wa uovu ni nini! Kama siyo aibu.
 
Du shida sana, Ni rahisi kupotea njia ukihojiwa na ikiwa sio ukweli. Yetu macho.
 
Hii kesi imekuwa ngumu sana kwa mashahidi wa mchongo na mawakili wao. Mawaili wa serikali wamegeuka kama watetezi na mashahidi kama washtakiwa
hofu imewajaa , hata jaji anaona
nitashangaa akisema kuna kesi ya kujibu
na hapo ndo kesi itakuwa ngumu zaidi
 
Wakili msomi Peter Kibatala ni mmoja wa Mawakili mahiri kutokea katika nchi hii. Ikipendeza namshauri Mhe. Rais amteue Wakili msomi Peter Kibatala ili amsaidie Serekalini yake. Huyu anafaa kuwa DPP.
Siku Kibatala akajidanganya kwenda huko, ndio ameharibikiwa. Serikali hii inaharibu Sana vipaji na weledi wa watu. Huko ni lazima ukabariki uongo na kutetea dhuluma.

Ona wasomi wazuri Kama kina Kakurwa walivyo kuwa reduced to nothing.
 
Janja yao sasa hivi ni kuwatoa mashahidi kizimbani pindi wanapoona mambo yanawalemea ili wakajipange upya. Yote kwa yote uongo haujawahi kuishinda kweli. Wanavyozidi kupanga uongo ndivyo wanavyozidi kujididimiza kwenye shimo la kushindwa. Na kauli hii wanatakiwa kuijua kuwa uongo huonekana kweli kama tu huo uongo hautahojiwa.
 
Kama wanaenda kumfundisha majibu baada ya kuona ameanza kujikoroga. Ingekuwa ni kwenye boxing, hapo unamuona meneja anatupa taulo ulingoni! and the game is over, ila hapa - kipenga cha mwisho bado.
 
Back
Top Bottom