Yaliyojiri Uwanja wa Aman: Simba SC Vs Yanga,Kombe la Mapinduzi 10/1/2017

Dk 55, kosa hapa Dante anachichanganya Simba wanaingia hatariiiiiii Dante anaokoa

Dk 54, kona ya Kichuya, hatari tena, Dida anaokoa hapa

Dk 53, Kichuya anaingia vizuri hapa, hatariiii lakini Dante anamuwahi na kutoa nje, kona

Dk 53, Juma Abdul anacheza faulo hapa lakini mwamuzi anamsamehe, akimuonya kwa maneno. Kumbuka kadi ya njano

Dk 52 kona nyingine inachongwa na Kotei lakini Yanga wako makini wanaokoa

Dk 51, Simba wanafanya shambulizi kali hapa, krosi ya Kichuya Yondani anaokoa na kuwa kona, inachongwa na Kichuya, Dida anaokoa tena na kuwa kona tena

Dk 49, Simba wanagongeana vizuri na Mo Ibrahim anaachia mkwaju na Dida anadaka vizuri

Dk 47 krosi nzuri ya Mwinyi lakini Mwanjale anauwahi, kona. Inachongwa na Niyonzima , wanaokoa

Dk 46, Yanga wanacheza vizuri, lakini Tambwe anashindwa kupiga krosi kutokana na kasi ya mpira
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…