Yaliyojiri VPL: Simba SC vs Yanga SC - 20 October 2013

Status
Not open for further replies.
Mpwa umezinduka sasa...teh teh!!!

Mpwa hakuna siku uliyonipa presha kama leo.

Na bahati nzuri hakuna siku uliyonipa presha kama leo.

Leo ilikuwa mturudishie zile sita zetu. Hamtaweza tena.
 
Hata wewe unashangilia droo na kuenguliwa kileleni!? Basi haya majanga no wonder timu ya Watanzania kuongozwa na Msomali.

Potelea mbali mkuu. Leo ilikuwa tunywe si chini ya tano. Mungu alikuwa upande wetu.
 
Simba ni damu nyekundu ukijikata ukaona unnjano huo ni uchafu wa usaha wa yanga. Yanga uozo 3-0 then kidume Simba kazirudisha Yule mshabiki wenu kulialia atahama yanga soon.
 
Simba ni damu nyekundu ukijikata ukaona unnjano huo ni uchafu wa usaha wa yanga. Yanga uozo 3-0 then kidume Simba kazirudisha Yule mshabiki wenu kulialia atahama yanga soon.
alisema hii mechi wakipoteza anajinyonga
 

Mkuu....mimi ni Yanga lakini imefika mahali nimenyoosha mikono juu na kusema msimu huu Simba ni bora kuliko Yanga na ubingwa utakwenda Msimbazi, thanks to the genius of King Kibadeni.

Timu yoyote yenye uwezo wa ku-cancel a 0-3 deficit hiyo ni championship material. Simba msimu huu the championship is yours to lose!

Kwa Yanga, msimu huu timu hakuna but it is a bunch of expensive players with full of ego ambao hawaichezei timu yetu kwa kujituma - labda Ngasa tu.
 
Masuke Masuke Masuke mtani wangu.......

Unashangilia sare?........Hongereni sana kwa kuishinda Yanga magoli matatu mtani......

Simba hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

Mkuu hii sare ingekuwa ya funga nikufunge ningeona sawa tu lakini nakwambia mashabiki wote wa timu zote mbili baada ya Kiiza kufunga goli la tatu tulijua Simba ndo basi tena lakini kurudisha magoli yote matatu lazima nifurahi aise.
 
Huwezi kuiba timu ubingwa kwa mechi yenye tension kama ya Utani wa Jadi...

 
cha kushangaza mabao yote 6 yameingia upande mmoja wa uwanja
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…