Yaliyomkuta Abdul Jumbe yatamkuta Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Mh Othman ?

Yaliyomkuta Abdul Jumbe yatamkuta Mwanasheria mkuu wa Zanzibar Mh Othman ?

MWANASHERIA MKUU WA ZANZIBAR kitendo cha kupiga kura ya hapana ni taarifa kuonesha msimamo wa serikali ya upande wa pili, japo tulio wavivu wa kufikiri tutasema ni msimamo wake binafsi, na asubuhi niliandika humu jf kuletwa kwake chini ya ulinzi mkali, yaweza kuwa yu kizuizini bila kujijua!
 
Ilikuwa "April 1972" Mh: Alhaji Abdul Jumbe Mwinyi alipotwaa madaraka ya Zanzibar na kuwa Rais wa awamu ya pili wa serikali ya SMZ mara baada ya Mh: Abeid Aman Karume kuuwawa, Septembar 5, 1975 Mwalimu Nyerere akiwa kama Mwenyekiti wa Tanu na Rais wa Tanganyika aliwasilisha wazo kwenye kamati kuu ya "TANU" juu ya kuunganisha chama cha "TANU" na "ASP" suala lilijadiliwa na hatimae "OCTOBER 1976" "ASP" na "TANU" zilifikia muafakha juu ya kuungana na kuzalisha chama cha "CCM" ambacho uzinduzi wake ulikiwa Tarehe 5/2/1977, Mwendendo wa Abdul na Nyerere kwa wakati huu ulikuwa mzuri japo Abdul Jumbe alijisahau sana juu ya Taifa lake la Zanzibar lakini yote haya yalisababishwa na tamaa ya madaraka! Kwan alitamani awe rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Abdul jumbe safar yake ilianza kuwa mashakhani pale tu mara baada ya ujio wa "Edward Sokoine" ndipo alipo amua kuanza kudili na Taifa lake la Zanzibar kwa kuangalia maslahi ya Zanzibar na watu wake na kuona kuwa swala la Muungano limekaa vibaya na kuanda taarifa mbalimbali ili awasilishe mahakamani, Bila shakha wana jamvi mutakuwa munakumbuka nn kilimkuta Rais huyu wa Zanzibar Shekhe Abdul Jumbe Mwinyi kwani alipigwa kibuti na CCM mnamo mwaka 1984 kwa kisingizio cha kuvunja katiba hivo kupoteza nafasi zake zote alizokawa nazo yaani Rais wa Zanzibar, Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia na makamo mwenyekiti wa "CCM" japo nchi yake ilikuwa na katiba……!

Mwanasheria mkuu wa zanzibar (Mh: Othman Masoud Othman) ikumbukwe alijiulu katika kamati ya uandishi wa katiba pale BMK, Mwanasheria huyu huyu hakuonekana siku nyingi katika mara baada ya kujiuzulu pale kwenye kamati ya uandishi japo kwa upande wa "CCM" hawakuona kama ni tatizo kuto kuwepo kwake, wachambuzi wa masuala ya siasa hawakupenda juu ya kuendelea mchakato wa katiba huku kukiwa na makundi makubwa yanayo pingana juu ya namna ya kuandika katiba hiyo, Makamu Mwenyekiti wa wa "JUKATA" akihojiwa katika kipindi cha HOT MIX kinachoenda heweni chanel 5 alidokeza juu ya kile kilichomtoa mwanasheria huyu wa SMZ katika kamati ya undishi kuwa ni "kulingana na mjadala unavyoendelea BMK haoni maslahi ya Zanzibar ili katika Rasimu ya Tume ya mabadiliko ya katiba maslahi ya Zanzibar yalikuwepo kwa 100%" , ikiyaeleza haya makamo huyo wa mwenyekiti alisema kuwa yeye alipata nakala ya barua ya kujiengua ktk kamati hiyo ya uandishi, cha kushangaza ni leo mwanasheria huyu wa SMZ alipokuja BMK na kupiga kura ya HAPANA katika ibara na sura zote ambazo hakuzihafikhi…!!! Na kura ya NDIO kwa ibara ambazo hakuwa na tatizo nazo…!

Ya moyoni mwanangu;- Mwanasheria huyu hata undiwa zengwe kama alivyofanyiwa mzee Abdul Jumbe Mwinyi…??

Je kweli Mwanasheria huyu halifanya haya bila kumshirikisha Rasi wa SMZ…??

Je kuundwa kwa kamati ya mashauliano pale BMK jana alishajua wajumbe waliopiga kura hapana watarubuniwa na kubadiri misimamo yao na yeye akaamua kujitosa ili waone kama wako pamoja na yeye na kuwapa nguvu ya kusimamia yale wanayo yaamini…???

Je mwanasheria kashaona kuwa sasa si wakati wa kwaheri ukoloni, kwaheri uhuru…???

katika haya kuna moja au mawili lazima mwanasheria huyu aliyaona…………!!

Inauma historia ya muungano huu pale utaposoma kitabu cha kwaheri ukoloni, kwaheri uhuru……!
hakika mkuu serikali inaendeshwa kibabe sana
 
...kwa jinsi hiyo katiba hilivyo jaa upuuzi mwingi,ata kama shetani angekuwa mjumbe wa hillo genge la wahuni(BMK)angepiga kura ya hapana...
 
Katiba ya ccm sio ya watanzania ni yachama cha ccm.karba MPYA niile iliyo pendekezwa na wanannchi na kuletwa na walioba.
 
serikali ya ccm imetoa tamko usiku huu ikisema mwanasheria mkuu wa nchi ya Zanzibar alipatiwa ulinzi kutokana na msimamo/ mawazo yake ya kisemokrasia ambayo alipiga kura ya HAPANA akipiga katiba ya kihuni hasa kipengele chochote kilichotaja neno "Muungano" inayoteketeza kodi za walala hoi huku wakijua wanachokijadili wananchi hawajawatuma na yapo waliyotumwa kwenda kuyajadili pia serikali imeongeza kuwa itaendelea kumpatia ulinzi huo hata huko anakoenda baada ya kutoka viwanja vya bunge. ikumbukwe hata mzee Aboud Jumbe anapatiwa ulinzi mpaka leo kisicho na kikomo (ambapo kwa kifupi ni kifungo mpaka kufa kwake.. Inasemekana pia maccm yaitaka kumwua mzee Jumbe, lakini watapata taarifa kuwa wakithubutu kufanya hivyo zanzibar lazima kitanuka, maana wazanzibar wanajitambua. Baada ya kugundua hivyo, maccm yaliamua kumlima kifungo kisicho na kikomo tokea aliponyang'anywa madaraka yake Chimwaga, lakini hawakuishia hapo, walichokifanya inasemekana walimchoma sindano ya kupoteza kumbukumbu, na kumwathiri kisaikolojia kwa maslahi yao.

Hofu hapa inakuja kwamba kwa maccm yalivyo na kihoro, wanaweza wasimpeleke huyu Shujaa AG wa Zenji Mwabepande, wakihofia kitanuka Zanzibar, lakini wanaweza kumfanyizia kama walivyomfanya mzee wetu Aboud Jumbe ambaye yupo kifungoni mji mwema kigamboni tokea 1984 mpaka sasa...

Ndugu zangu watanganyika na Wazanzibari tupazeni sauti kumwokoa shujaa huyu...
AG wa Zenji wa The Heroe of the day!!

Wazanzibari wana kila sababu ya kuwastukia ccm, kwanini viongozi wa zenji wananyang'anywa mamlaka yao Dodoma? Tena wanapothubutu kutetea haki za wazanzibari? Wazenji stukeni, akili kumkichwa!!

Watanzania wote kwa ujumla, kinachoendelea Dodoma sasa inatupatia picha dhahiri kuwa Dr. Sengondo Mvungi hakuuawa na majambazi, na wala hakufa kwa bahati mbaya, bali aliuawa na system kwa ajili ya kubaka sauti ya wanyonge wa nchi hii. Nasema hivyo kutokana na Matukio ya kibabe ya BMK chini ya Sitta na tukio la kuuawa kwa shujaa Mvungi ku-tally.

Tutaona mengi zaidi....
 
Wakati umefika sasa wa kuchukua nchi yetu kutoka mikononi mwa mabeberu weusi wa ndani ya nchi yetu wenyewe.Nawaza kwa sauti ccn wakiijenga nchi hii kwa ngucu kubwa miaka zaidi ya thelathini leo hii wanaibomoa kwa nguvu ya damu.Damu ya think tanks wa Taifa hili.Tena kwa gharama kubwa ya uhai.Sasa naelewa kuuawa kwa Dr.Mvungi ilikuwa ni maandalizi ya kile tunachokiona leo.Kuounguza nguvu ya hoja dhidi ya uovu wao.Nalia na Mkuu wa nchi.Aliyewasaliti wapiga kura wqliotandika kanga zao chini ili apite,kina mama wajane na yatima waliopigwa jua wakimshangikia kwa nyimb😵le wao wanaoiweka nchi katika hatari kwa kupingana na demokrasia.Ole wa yule mwizi aliyeibia serikali mamilioni na kuyaita vijisenti leo hii ndio wachezeshaji wa mistari ndani ya katiba tena kwa majivuno na dharau zilezile za vijisenti.Ole wake yule aliyemlinda mke mtoa rushwa nyakati za uchaguzi.Aliyelia kwa Watanzania baada ya kunyang'anywa uspika.Kuprove kwamba bado anawafaa waliomdhalilisha leo anawaumiza walio lia nae wakati ule.GIVE ME BLOOD I GV U FREEDOM.
 
Asante Kamanda wangu ukiona mtoto anakukimbia wewe baba na si kukukimbilia jiangalie sana kuna shida mahali tena shida kubwa sana ccm watanzania wa leo si wale wakipindikile magenge yanu yote tumeyajua
 
Enzi zile siyo leo , wakithubutu kumdhuru bila shaka hali itachafuka na huenda isitakate tena !
 
Kushindana namipango ya Mungu nisawasawa nakusubiri meli Airport utashindwa tu ccm wakati wenu umefika wakufunga virago
 
Eti kapewa ulinzi kama ilivyo kawaida kwa BMK kufanya hivyo kwa mjumbe yeyote...well

Ok. Taarifa za habari (though shallowly) zimeonesha na kusema aliondoka na gari ya Serikali ya Mapinduzi, well...why not on his own car!?!?

Ok...well mbona BMK haikuwakikishia ulinzi wale waliotoa malalamiko yao jana kuwa wametishiwa maisha Kwa sababu ya kupiga kura za HAPANA.

Well...kwa hiyo CCM kupitia tamko lao wamethibitisha kuwa hata wale waliopiga kura za HAPANA walitishiwa na wale wale waliomtishia na kumghashi AG wa Zanzibar kiasi cha kumpatia ulinzi...

Well...CCM na mawakala wao wamesaidia kuongeza dots...asanteni.

Endeleeni kujifunga kwenye gunia hilo lenu. Mmegeuka kuwa MBUNI wa hadithi...

Mnatukumbusha Hadithi za Machimbo ya Mfalme Suleiman...tunasubiri huo mwezi...
 
Mwaka huu mtatunga hadi vidole vitapinda!
Mmetunga asubuhi kupitia Haki sawa kuwa mwanasheria katekwa na usalama wa taifa mkaumbuka!
Mmetunga kupitia Mohamedi Mtoi Sitta kaandika vimemo kumbe mmevitengeneza na mkashindwa kuvifananisha nenda kaangalie mwenzio alivyo umbuka!


Wewe umekuja na stori hizi na sito shangaa mkimteka halafu mkasingizi CCM!

Hivi maandano ya nchi nzima yamekwisha?
Kinacho wafanya muwewe seke ninni wakati mnauhakika kuwa rasimu itakataliwa?
 
Last edited by a moderator:
Wakuu,"Dunia imani imekwisha; na adui atoki mbali nasi"
NI WAKATI WA KUMWAMINI MOLA SI RAFIKI, KIONGOZI,MKE
{MIKA 7:2-6}
 
Wakati umefika sasa wa kuchukua nchi yetu kutoka mikononi mwa mabeberu weusi wa ndani ya nchi yetu wenyewe.Nawaza kwa sauti ccn wakiijenga nchi hii kwa ngucu kubwa miaka zaidi ya thelathini leo hii wanaibomoa kwa nguvu ya damu.Damu ya think tanks wa Taifa hili.Tena kwa gharama kubwa ya uhai.Sasa naelewa kuuawa kwa Dr.Mvungi ilikuwa ni maandalizi ya kile tunachokiona leo.Kuounguza nguvu ya hoja dhidi ya uovu wao.Nalia na Mkuu wa nchi.Aliyewasaliti wapiga kura wqliotandika kanga zao chini ili apite,kina mama wajane na yatima waliopigwa jua wakimshangikia kwa nyimb😵le wao wanaoiweka nchi katika hatari kwa kupingana na demokrasia.Ole wa yule mwizi aliyeibia serikali mamilioni na kuyaita vijisenti leo hii ndio wachezeshaji wa mistari ndani ya katiba tena kwa majivuno na dharau zilezile za vijisenti.Ole wake yule aliyemlinda mke mtoa rushwa nyakati za uchaguzi.Aliyelia kwa Watanzania baada ya kunyang'anywa uspika.Kuprove kwamba bado anawafaa waliomdhalilisha leo anawaumiza walio lia nae wakati ule.GIVE ME BLOOD I GV U FREEDOM.

Kamanda doreen

Maneno makubwa haya...well articulated Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom