D
Deleted member 485868
Guest
Habari zenu wana Jf
Nianze na mkasa ulionikuta jana..mida flani hivi nilienda kariakoo na Dada yangu..katika mizunguko yetu yeye alikua mbele mimi nyuma
Sasa si mwajua kariakoo ilivyo na watu wengi..nikiwa katika mshangao wa kushangashangaa nguo ghafla nikapigana kikumbo na mdada amevaa baibui ameziba macho kama avatar ya madame s
Yani nikaganda ghafla uku nikimuangalia tu..akafika mbele akageuka..lahaullah!! Macho ya yule dada sikuyaelewa hata kidogo alafu yalikua hayatulii kile kiini cheusi kinafanana na kiini cha paka
Nikasema hapana sikuamini nilichokiona nikageuka kuangalia mbele huku nikijiuliza kama yule ni mtu
Nikageuka tena nyuma alikua amefika mbali lakini bado aliponiangalia macho yalikua vilevile...ghafla Dada akaniita jina langu nikaitikia "aliniuliza vipi mbona umesimama tu hapo" sikumjibu kitu
Nikageuka kwa mara ya mwisho sikumuona tena yule dada
Yani nilinyon'gonyea hadi tunatoka kariakoo bado najiuliza..hivi nilikutana na jini ama kuna binadamu wenye macho ya vile!!!
Hayo ndio yaliyonikuta siku ya jana mwenzenu
Nianze na mkasa ulionikuta jana..mida flani hivi nilienda kariakoo na Dada yangu..katika mizunguko yetu yeye alikua mbele mimi nyuma
Sasa si mwajua kariakoo ilivyo na watu wengi..nikiwa katika mshangao wa kushangashangaa nguo ghafla nikapigana kikumbo na mdada amevaa baibui ameziba macho kama avatar ya madame s
Yani nikaganda ghafla uku nikimuangalia tu..akafika mbele akageuka..lahaullah!! Macho ya yule dada sikuyaelewa hata kidogo alafu yalikua hayatulii kile kiini cheusi kinafanana na kiini cha paka
Nikasema hapana sikuamini nilichokiona nikageuka kuangalia mbele huku nikijiuliza kama yule ni mtu
Nikageuka tena nyuma alikua amefika mbali lakini bado aliponiangalia macho yalikua vilevile...ghafla Dada akaniita jina langu nikaitikia "aliniuliza vipi mbona umesimama tu hapo" sikumjibu kitu
Nikageuka kwa mara ya mwisho sikumuona tena yule dada
Yani nilinyon'gonyea hadi tunatoka kariakoo bado najiuliza..hivi nilikutana na jini ama kuna binadamu wenye macho ya vile!!!
Hayo ndio yaliyonikuta siku ya jana mwenzenu