Yaliyotokea mpakani na Kenya, Zambia na Rwanda yanaonyesha haja ya umakini kwa Magufuli kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani wenye uwezo wa kidiplomasia

Yaliyotokea mpakani na Kenya, Zambia na Rwanda yanaonyesha haja ya umakini kwa Magufuli kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani wenye uwezo wa kidiplomasia

Naona Wakenya mnaendelea kutoka mashimoni mlipokuwa mmejificha.. Bado dawa yenu inachemka..
Nadhani wewe mtu akiongea kitu ambacho hukubaliani nacho basi atakuwa ni Chadema au Mkenya, sivyo? Jifunze kuongea kwa hoja badala ya tuhuma, huo ndio uungwana katika jamii.
 
John atakuwa aliwapigia simu martin na Anna akawaambia wachimbe mkwara.

hujamsikia balozi ameambiwa na aidani kuwa ampigie baada ya wiki kwa sasa yuko bize?
 
Nakumbuka katika kuteua wakuu wa mikoa muda fulani uliopita, Raisi Magufuli alisema kwamba alikuwa akiteua wakuu wa mikoa ya mipakani wengi wakiwa wanajeshi ili kusaidia katika suala la ulinzi mipakani. Lakini sasa, migongano na nchi jirani za Kenya, Zambia, Rwanda na hata Uganda zimetufundisha na kutupa onyo juu ya umuhimu wa kuhakikisha kwamba wakuu wa mikoa ya mipakani wanapaswa kuwa watu wenye uwezo mkubwa wa kidiplomasia.

Ukichukulia Tanga na Kilimanjaro kwa mfano, tumeshuhudia wakuu wa mikoa wakichochea badala ya kuzima moto wa jazba uliojitokeza kati yetu na Kenya, hadi kufikia hatua ya kuwakejeli viongozi wakuu wa nchi jirani! Sasa hii ni hatari sana, na tusipoangalia inaweza kuleta machafuko kufikia wananchi wa mipakani kuanza kupigana na watu wa nchi jirani na hata kuuana. Na mazingira kama hayo yanaweza kufikia hatua ya polisi au jeshi kuingilia kati, na hata risasi kupigwa dhidi ya nchi jirani na kuzua mpambano wa askari wenye silaha.

Sio vibaya kuweka wanajeshi kama wakuu wa mikoa ya mpakani, kwa kuwa wapo wanajeshi wanaojulikana kuwa mahili katika masuala ya diplomasia. Hata hivyo, kama ni suala la ulinzi mipakani ni vema kuwa na kambi za jeshi katika kila mkoa wa mpakani, na wakuu wa kambi hizi wakawa sehemu ya kamati za ulinzi za mkoa ambazo zinasimamiwa na wakuu wa mikoa.

Hata hivyo, kipaombele kiwe kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani ambao ni raia na watu wenye uwezo mkubwa katika masuala ya diplomasia. Na ikibidi, wakuu wa mikoa ya mipakani wawe wanapitia mafunzo maalumu ya diplomasia kabla ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi.

Ningependa kushauri kwamba mabadiliko haya yafanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.
Wewe tuliza kitesi huko ebhoo
 
Mkuu, umeongea jambo ambalo watu wengi sana wameniambia, kwamba reaction zote zilizofanywa na wakuu wa mikoa katika huu mtifuano lazima zilikuwa maagizo toka juu. Sitaki kabisa kuamini hilo, na labda basi mimi niko "naive" kufikiri kwamba hatuwezi kuwa na kiongozi asiye na busara kiasi hicho. Kama kweli huo ndio uongozi tulio nao, basi twapaswa kuogopa sana!

Mkuu hiyo reaction ya hao RC's ni maagizo ya jiwe direct.
 
Hio ndio dawa yao. Ilibidi wakuu wote wa mikoa mipikani wafanye kama Tanga. Ingependeza sana.
Tuoneshane makali kidogo kidogo
Unajua uungwana ni sifa, sio udhaifu. Ukikumbuka hilo maisha yako nyumbani, kazini hata na jirani zako yatakuwa mazuri sana
 
Nadhani Tanga, Kilimanjaro huyu mama sidhani kama alishakuwa mwanajeshi. Lakini hiyo ilikuwa kauli ya ujumla, hakuna tuliposema Mkuu wa mkoa Tanga na Kilimanjaro ni wanajeshi. Ila Magufuli alisema anataka kuweka wanajeshi mikoa ya mipakani kama Kigoma na Kagera ili wasaidie masuala ya ulinzi mipakani
RC Shigela sio mwanajeshi,nadhani point yako ni kwamba RC's wa mikoa ya mipakani lazima wawe na uelewa na diplomasia,hata hvyo RC wa kigoma kwa mfano alishakuwa mwambata wa kijeshi katika ubalozi wa Tanzania Marekani
 
Nakumbuka katika kuteua wakuu wa mikoa muda fulani uliopita, Raisi Magufuli alisema kwamba alikuwa akiteua wakuu wa mikoa ya mipakani wengi wakiwa wanajeshi ili kusaidia katika suala la ulinzi mipakani. Lakini sasa, migongano na nchi jirani za Kenya, Zambia, Rwanda na hata Uganda zimetufundisha na kutupa onyo juu ya umuhimu wa kuhakikisha kwamba wakuu wa mikoa ya mipakani wanapaswa kuwa watu wenye uwezo mkubwa wa kidiplomasia.

Ukichukulia Tanga na Kilimanjaro kwa mfano, tumeshuhudia wakuu wa mikoa wakichochea badala ya kuzima moto wa jazba uliojitokeza kati yetu na Kenya, hadi kufikia hatua ya kuwakejeli viongozi wakuu wa nchi jirani! Sasa hii ni hatari sana, na tusipoangalia inaweza kuleta machafuko kufikia wananchi wa mipakani kuanza kupigana na watu wa nchi jirani na hata kuuana. Na mazingira kama hayo yanaweza kufikia hatua ya polisi au jeshi kuingilia kati, na hata risasi kupigwa dhidi ya nchi jirani na kuzua mpambano wa askari wenye silaha.

Sio vibaya kuweka wanajeshi kama wakuu wa mikoa ya mpakani, kwa kuwa wapo wanajeshi wanaojulikana kuwa mahili katika masuala ya diplomasia. Hata hivyo, kama ni suala la ulinzi mipakani ni vema kuwa na kambi za jeshi katika kila mkoa wa mpakani, na wakuu wa kambi hizi wakawa sehemu ya kamati za ulinzi za mkoa ambazo zinasimamiwa na wakuu wa mikoa.

Hata hivyo, kipaombele kiwe kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani ambao ni raia na watu wenye uwezo mkubwa katika masuala ya diplomasia. Na ikibidi, wakuu wa mikoa ya mipakani wawe wanapitia mafunzo maalumu ya diplomasia kabla ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi.

Ningependa kushauri kwamba mabadiliko haya yafanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.
Hebu Wape Ushaur hawa waliokosa dipolo.masia wafanye nn cha kidipolomasia ili wadeal na kukosa "diplomasia" kwa Rais wa nchi jiran.

Naomba uwape USHAURI ambao n Substantive


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu Wape Ushaur hawa waliokosa dipolo.masia wafanye nn cha kidipolomasia ili wadeal na kukosa "diplomasia" kwa Rais wa nchi jiran.

Naomba uwape USHAURI ambao n Substantive
That is very simple. Unapo deal na mtu mwenye kukosa diplomasia onyesha diplomasia!
 
Mkuu, unajua inawezekana Rwanda waliamua kuwa na diplomasia kuliko sisi ndio mana tatizo pale likaisha, umefikiria hilo?
Inawezekana kabisa,upo sahihi...Lakini pia inawezekana majirani zetu wa kaskazini-mashariki wana diplomasia ya chini mno kuliko sisi...Rais wetu si alitangaza hatafunga mipaka kutokana na majirani zetu kutegemea bidhaa kutoka kwetu hasa chakula na wengine za bandarini? Hapo tu diplomasia alishaionyesha....Sasa walimwamsha aliyelala walitegemea nini? Hawa walijiamini sana na kuona hakuna atakayewatikisa zone hii...Let's see who is who.
 
Mimi naona Shigela amekuwa mpole ilitakiwa zaidi.Jumuiya ya Africa mashariki ilikufa sababu ya unyang'au wa hawa watu.
Uweke diplomasia na watu walioshindwa kuunganisha makabila yao.
Mkuu, hivi Tanzania tunaweza kuwasema wakenya kuhusu ukabila? Kwani kabila ni nini - kikundi cha watu wenye desturi na mila na lugha sawa. Na ukabila unakuja pale ambapo kikundi kimoja cha namna hiyo kinakuwa na bifu na kikundi kingine, sivyo?

Basi kwa jinsi hiyo hata chama cha siasa kinakuwa ni namna ya kabila.Tunaweza kuwa na kabila la CCM, na kabila la Chadema, ACT nk

Sasa niambie, wepi wana hali mbaya zaidi - Wakenya katika ukabila wao wa vikundi vya lugha au Watanzania katika ukabila wetu wa vikundi vya kivyama?

Tanzania hata siku moja hatuwezi kuwasema Wakenya katika ukabila wao wa vikundi vya kilugha, kwa kuwa ukabila wetu wa vikundi vya kivyama unaweza kuwa mbaya kuliko wa kwao!

Nilimshangaa sana Prof Kabudi bila aibu anawaambia Wakenya waache ukabila. Tanzania tuna hali mbaya ya ukabila wa kivyama kuliko Kenya!
 
Back
Top Bottom