Yameanza kwa TRA yatafata kwengine, TRA kusimamia wenyewe ajira badala ya utumishi tunarudi kule kule kwenye ajira za ukoo na kujuana

Yameanza kwa TRA yatafata kwengine, TRA kusimamia wenyewe ajira badala ya utumishi tunarudi kule kule kwenye ajira za ukoo na kujuana

Hoja ya kipuuzi sana, Kwanza sahili nyingi huwa ni siku za kazi jumatatu hadi ijumaa, Pili hata ikifanyika jumamosi kwa wasabato huwa kuna ibada ya mchana.

ANYWAY!!

NImegusia mambo mazito yanayohusu mustakabali wa raia asiye na connection kupata ajira..na si siku gani usaili ufanyike.

Unaweza kufanya Huo usaili siku tofauti na ya sabato lakini bado ukakumbana na ukiritimba wa mfumo.
Kama hujui kitu uliza usitake kujifanya mwerevu kumbe ni mweupe ibada ya mchana uliisikia wapi sabato inaanza ijumaa jioni mpk jmosi jioni hakuna kufanya kazi yoyote wewe hiyo ibada ya mchana umeitoa wapi usifananishe imani ya wasabato na wengine
 
Mimi nilichojifunza maisha ya Tanzania ni kwamba, kuna maamuzi yanafanywa na watu kwa lengo la manufaa yao, yaani na wenyewe wanufaike. Taasis zipo nyingi siyo TRA. Kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake!
 
Mke: Mume wangu, mdogo wangu kile kipindi utumishi wanasimamia ajira hakupata kabisa.

Mme: Ni kweli utumishi walikuwa pasua kichwa, walituharibia sana, mambo ya connection yalipigwa panga.

Mke: Sasa Mama karuhusu Mashirika mjisimamie msaidie basi mdogo wangu.

Mme: Ondoa shaka, mdogo wako aombe tu, mengine ntamalizia

Nikiri kwamba kulikuwa na malalamiko ya utumishi kuchelewa kuita watu kazini ila ni vema hayo malalamiko yangefanyiwa kazi kuliko Rais kuruhusu taasisi ziajiri zenyewe,

Unadhani mabosi wataruhusu watoto wao ama ndugu zao wabaki mtaani kisha wewe usie na connection hata uwe na cheti kizuri upenye ? Ni ngumu sana hio!! Na ndio maana kulikuwa na utumishi ili kukabiliana na hili maana hata hao mabosi pamoja na elimu zao ni binadamu tena waafrika wenye utamaduni wa kuweka mbele watoto, ndugu, marafiki, watu wa kabila lao, dini yao, n.k.

Utumuishi pamoja na changamoto zake wengi tulijionea mambo ya connection yalipungua sana, watu hata waliotoka familia za chini ilikuwa kawaida sana wanapenya.

Ghafla mwezi wa pili Mama akatoa speech kwamba taasisi nazo waanze kujisimamia ajira, Balaa ndipo lilipoanzia hapa sasa linaloenda kuleta ubaguzi kwenye ajira.

Nimeona pia mitihani haifanywi sehemu moja ni mikoa tofauti tofauti, zamani wote mlikuwa mnaenda Dodoma ila kwa utaratibu huu mpya ni rahisi kuvuja mtihani.

Source"

Kuruhusu mashirika yajisimamie kwenye ajira badala ya utumishi

TRA Tangazo la kuitwa wenye Usaili
Ungewashauri tume ya ajira iache urasimu haya yasingetokea.
Taasisi inaomba kuajiri wanaruhusiwa baada ya mwaka sasa itakidhi vipi mahitaji ktk hicho kipindi cha mwaka wamekaa bila wafanyakazi
 
Mama hapo alikurupuka, kuna vigogo ndani ya TRA na nje ya tra waliotengeneza tatizo ili ionekane utumishi kuna shida. Mimi binafsi nimefanya kazi kwenye taasisi za serikali zinazoajiri zenyewe na zile zinazoajiri kupitia utumishi, nimeshuhudia undugunization wa hatari kwenye taasisi zinazoajiri wenyewe, kwa watoto wa mama ntilie nawataarifu tu kazi za TRA mtaishia kuziona kwenye matangazo tu, wale intake ya mwisho iliyobahatika kupenya kupitia utumishi ndio ilikuwa intake ya wasakatonge waliofunga mlango.

Mama samia nakuomba hili ulitizame kwa upana wake. Hapo TRA kuanzia mchakato wa kununua mfumo wa Ajira (takribani milion 700 imetumika) umegubikwa na ufisadi wa hali ya juu, fairness kwenye mchakato wa ajira kwa watanzania wasiokuwa na connection inakwenda kutoweka.

Suala la ajira kwenye taasisi/mashirika ya umma lisimamiwe na utumishi, inawezekana kuna mapungufu madogo madogo yapo utumishi nashauri ni vyema yangetatuliwa hayo luliko kuondoa kabisa mandate ya wao kufanya mchakato wa ajira kwa mashirika/taasisi za umma. Ni matumaini yangu utayasikiliza na kuyafanyia kazi haya. Bado haujachelewa.
Kwani utumishi inasimamiwa na mashine?
Kama ni binadamu kwani heads wa utumishi na mashirika hawajuani.?
Kusema utumishi wanakuwa unbiased syo kweli
 
Mke: Mume wangu, mdogo wangu kile kipindi utumishi wanasimamia ajira hakupata kabisa.

Mme: Ni kweli utumishi walikuwa pasua kichwa, walituharibia sana, mambo ya connection yalipigwa panga.

Mke: Sasa Mama karuhusu Mashirika mjisimamie msaidie basi mdogo wangu.

Mme: Ondoa shaka, mdogo wako aombe tu, mengine ntamalizia

Nikiri kwamba kulikuwa na malalamiko ya utumishi kuchelewa kuita watu kazini ila ni vema hayo malalamiko yangefanyiwa kazi kuliko Rais kuruhusu taasisi ziajiri zenyewe,

Unadhani mabosi wataruhusu watoto wao ama ndugu zao wabaki mtaani kisha wewe usie na connection hata uwe na cheti kizuri upenye ? Ni ngumu sana hio!! Na ndio maana kulikuwa na utumishi ili kukabiliana na hili maana hata hao mabosi pamoja na elimu zao ni binadamu tena waafrika wenye utamaduni wa kuweka mbele watoto, ndugu, marafiki, watu wa kabila lao, dini yao, n.k.

Utumuishi pamoja na changamoto zake wengi tulijionea mambo ya connection yalipungua sana, watu hata waliotoka familia za chini ilikuwa kawaida sana wanapenya.

Ghafla mwezi wa pili Mama akatoa speech kwamba taasisi nazo waanze kujisimamia ajira, Balaa ndipo lilipoanzia hapa sasa linaloenda kuleta ubaguzi kwenye ajira.

Nimeona pia mitihani haifanywi sehemu moja ni mikoa tofauti tofauti, zamani wote mlikuwa mnaenda Dodoma ila kwa utaratibu huu mpya ni rahisi kuvuja mtihani.

Source"

Kuruhusu mashirika yajisimamie kwenye ajira badala ya utumishi

TRA Tangazo la kuitwa wenye Usaili
Hii ni awamu haramu ya uongozi na utawala. Maskini hamna chenu, zaidi ya njaa, kukosa na kaburi.

CCM ni chama dhalimu
 
Hoja ya MTOTO wa MASKINI sijawahi ielewa kabisa.

Mtoto wa TAJIRI hana HAKI ya AJIRA isipokuwa Mtoto wa MASKINI?

Yawezekana huyo MTOTO wa Maskini akawa ndio tatizo zaidi maaana tyr ni MASKINI, akipata kazi atawaza KUIBA tu ili ajikomboe na UMASKINI.. ee unaon Mentality ilivyo?

Turudi ktk MADA,

Watanzania Sisi ni WANAFKI sana, ukiona mtu analalamikia jambo basi ujue HANA FAIDA nalo.. Akifaidika nalo hutomskia akibwabwaja tena.

Ndio maana Wanasiasa wanawapa rushwa ya kofia na Vitenge vya Chama. Mnajisahau mnawapigia KURA tena.
 
Hao utumishi walituhujumu sana wasabato kila usaili wanapanga jumamosi licha ya malalamiko walitia pamba masikioni bora ilivyorudi hivi na shida kubwa ni kutaka kuwafanyisha watu wote sehemu moja tu hivyo kuwa ngumu kupata venue kuwaaccomodate wote kwa hiyo inabidi kuweka siku isiyo na kazi na hivyo kuiweka jmosi huu uamuzi upo sawa kbs utaondoa hiyo shida
Acha ujinga
 
Kama hujui kitu uliza usitake kujifanya mwerevu kumbe ni mweupe ibada ya mchana uliisikia wapi sabato inaanza ijumaa jioni mpk jmosi jioni hakuna kufanya kazi yoyote wewe hiyo ibada ya mchana umeitoa wapi usifananishe imani ya wasabato na wengine

Aisee, watu huwa wanafanya mtihani hadi ijumaa na ni siku ya Waislam kuswali unataka nao waje kulalamika hapa ?.. Yan mtu kaleta hoja ya msingi kabisa we unataka kuleta maswala ya dini hapa mkuu ??
 
haya mashirika ni yale yanayojiendesha kwa rasilimali zake yenyewe, ni kwamba lazima ifike sehemu yawe na mentality ya private sector, yaweze kuajiri kulingana na vigezo vyake yenyewe bila kufuata vigezo vya Serikali kuu
 
Utumishi walikua wanaajiri watu, wakifika kwenye mashirika mashirika yanawarudisha sababu hawakidhi viwango. Sasa sielewi inamaana process nzima ya kuajiri haikua inamhusisha aliyeomba kuletewa watu au.
 
Hao utumishi walituhujumu sana wasabato kila usaili wanapanga jumamosi licha ya malalamiko walitia pamba masikioni bora ilivyorudi hivi na shida kubwa ni kutaka kuwafanyisha watu wote sehemu moja tu hivyo kuwa ngumu kupata venue kuwaaccomodate wote kwa hiyo inabidi kuweka siku isiyo na kazi na hivyo kuiweka jmosi huu uamuzi upo sawa kbs utaondoa hiyo shida
Mbona kuna safari walipanga usaili jumapili, hapo ni sawa si ndio? Nyie na hilo dhehebu lenu mna mambo mengi sana amueni moja
 
Kwa tuliotoboa utumishi kwa Nguvu za Mungu pekee bila kumjua yotote huko serikalini ndio tunaujua umuhimu wa hiyo tume, ni sio mmoja ni maelfu, hivyo kurudisha kwenye taasisi husika usaili wa ajira ni kipengele kutokana na kubebana kwa kujuana.

Hiyo ya sehemu husika ibaki internship na field tu
Kwa waliotoboa kupitia utumishi wanajua umuhimu wa Utumishi kwenye suala la ajira
 
Back
Top Bottom