Well said man! nadedicate kwako ule wimbo unaosema...mamaaa you are the queen of my heart.....
mchunguze pengine kuna mtu anampiga mashine, anakutafutia sababu muachane mgawane mali kwanza kabila gani huyo kuna makabila bwana wao ni mali mbele mapenzi ni nyongeza tu........ ikishindikana kabisa bora muachane hata kama ni kugawana mali sawa utapata nyingine, bora kuishi masikini uwe na amani kuliko tajiri usiyepata usingizi na karaha kibao.
dah pole wangu
ebu mtume mshenga akazungumze nae kwa kireeeeeeeeeeeeefu na kumshauri nini cha kufanya katika kuendeleza ndoa yenu
sasa km awapend ata wazaz wako sasa atampenda nan jaman?
ata mtoto wako?
eLA ZA matumizi unamtumia ?
dah muwege makin mkikurupuka kuoa ndo mnabambana na ma DELILA km ivi
mwambie aelewe jins unavyokwazika na natabia zake...akikujbu ujinga bas ujue anacho kinachomtia jeuri...pole sana
Usikurupuke Bro kumuacha mkeo.
Fanya uchunguzi inawezekana ni hao ndugu zako ndio wana maneno. Ndugu hasa kama tegemezi au hawana cha kufanya kijijini, lazima watajaribu kuingilia ndoa yako ukiwachekea wanahania mjini kabisa na kujaza nyumba milele.
Isitoshe imeandikwa kila mmoja atamuacha baba na mama yake na kuambatana na mkewe, hao wawili watakuwa mwili mmoja. Kama nyie mnaelewana ndugu ndio wawaachanishe?? Labda hilo la mtoto wako kutokuishi na nyie ndio la msingi.
Ndoa changa haipendezi ndugu kuja kuishi na nyie manake mnakosa faragha.
Nyambura karibu sana kaka. Pole saana kwa tatizo lako, kutokana na opinion yangu inayotokana na the fact kua umetaja madhaifu ya mke wako mengi ambayo kweli si mazuri na bahati mbaya zaidi ni ya msingi sana for a marriage to survive. Ukilazimisha kua na huyo mke wako ujue kwamba familia yako automatically itajitenga from your whole family which is very bad. Siri ya mwanaume kua na amani katika ndoa yake ni kuoa mwanamke mwenye busara na ufikiri na hata akikosa hivyo walau awe sensitive. Una bahati its not too late mana hana mtoto, umejua tabia yake ni mbovu, ni jeuri (why would you want such a woman; stress za kazini utamplekea nani?) . Siwezi kukuambia muache lakini kaka tafadhali tafakari. Alafu huyo mtoto ukirudi mlete town, mpe access ya vitu ambavyo hawezi pata kijijini kwani ulimwengu umebadilika mno Ignorance haina nafasi.
Mpendwa Asha D,
Nakushukuru sana kwa ushauri wako mzuri, naamni wazi kuwa ushauri wako na wadau wengine pia wote utanisaidia. Kiukweli inaniuma sana mtu unayempenda na kumfanyia kila litu stil haonji hata chembe kama unampenda na zaidi ni kukuumiza na kukuletea dharau tele. Any way, nakushukuru mammy!
And pleeease I believe you are young, hutakua affected kivile mkigawana hivyo vitu, to me i know its worth it
tatizo kama hili la jamaa mi ilinipata baada tu ya kuoa: lkn mi nilifanya kiakili sana mpaka akaamua kukimbia mwenyewe. tofauti na huyu mi tayari nilzaa naye mtoto mmoja. Nilichofanya niliamua kumfanyia visa mara sirudi nyumbani, mara nafika nyumbani na mwanamke namtambulisha kama rafiki then natoka naye halafu sirudi siku hiyo, akilalamika nakaa kimya simjibu, simgombezi, sikumtukana ila vituko hivi tu vilitosha. Nilifanya hivi kwa miezi miwili tu akachapa lapa mwenyewe, wala mali hatukugawana. Baada ya kujivunza kupitia kwa huyu wa kwanza sasa ni mke anayestahili kweli kuitwa mke na ninaenjoy kweli maisha ya ndoa
Lizzy unautani na ID yangu?Yani hayo yote ya kutompenda mtoto wako au ndugu zako ndo umeyajua leo au ulikua unayajua tangu mwanzo ukajifanya kichwa ngumu na kumuoa hivyo hivyo????Ukishajibu ushauri utatoka kuendana na tatizo lako!