Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano, Trh 16 Aprili 2014 - Majadiliano ya bunge zima sura ya 1 & 6

Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano, Trh 16 Aprili 2014 - Majadiliano ya bunge zima sura ya 1 & 6

Pamoja na kuwa hoja ya serikali tatu ina mashiko,Kwa kipindi hiki kupita kwa hoja hii Ni kama ngamia kupita kwenye tundu la sindano..
. practically impossible......kanuni ya kura ilishapitishwa.....wengi wape......


.




.
 
UKAWA n wanafik wakubwa wale,wamechukua POSHO leo saa Tano na nusu na wamechukua pesa mpaka tr 31/4..kama walikuwa na lengo la kutoka y wasingetoka jana na kwannn wasiache zile pesa warud kwetu tuwaamin kama wapo kwa ajil ya waTz???ukawa n wahuni wote niseme hvo na wanatarajia sympath yetu wananchi wanashindwa elewa kuwa chaguz ndogo zote zilizopita CCM imewaburuza mbaya wapinzani.maskin upinzan hauna dira


Sent from my iPhone using JamiiForums.

Akili za udongo hata ukiongezewa mawazo mengi kama yapatikanayo JF utabakia vumbi tu...utakapofunguka macho 'udondoshe magamba' utagundua ulivyo na akili iliyo dhoofu!

Wanaokula posho wa wizi na kuweka wajumbe 201 hadi waganga wa kienyeji Kinje- (ajenti wa shetwani), hao ndio unawaona wanakula halali na kuuharibu uhalali wa Rasimu ya Katiba? Your poor mind shall cost you your entire intelligence and knowledge!
 
Kwa aliyeangalia bungu maalumu la katiba atujuze kama mheshimiwa zitto aliungana na kina lipumba kutoka nje ya bunge la katiba?
 
Nathubutu kujiuliza hili swali kwasababu nawaona wachangiaji wote waliobaki humu kwenye bunge la katiba wakisimama kuchangia hawazungumzii kitu cha maana au kujenga hoja za maana zinazohusu kufungu namba 6, badala yake wanaongea mipasho na kuwaponda UKAWA.
Kila mchangiaji haweki hoja madhubuti iliyo na mashiko kutetea serilaki mbili anazozitaka na kupambanua udhaifu wa serikali 3 wanazozitaka UKAWA.
The big deal kwao imekuwa kuongelea tundu lisu amemtukana nyerere, mara Haji Duni anaitwa babu wakati hana mjukuu, mara Mbatia hajui takwimu.
Sasa hizi posho wanazochukua wanazitendea haki gani??
Mimi naona hili bunge halitasaidia lolote zaidi ya upotevu wa pesa tu.
Swali; je ni kweli ukiwa m-CCM unajiwekea mipaka ya kufikiri na kupambanua hoja ambazo wananchi wanatarajia??

jibu ni ndiooooooooooooooooooo!
 
Waroho wa madaraka ni hao ccm wanaomfanyia dua mbaya Jaji Warioba afe kwa vile inapunguza madaraka ya wachumia tumbo wa ccm kwa hiyo wanaona nafasi zao zitakuwa mashakani.
Ndio maana wanang'ang'ania mbili ili waendele kitawala huku wakiendelea kuongeza wizara hadi mawaziri wengine hawana wizara maalum.
 
Wamechelewa sana!!!!!
Better late than never though

Ccm wameshinda kwa hoja za matusi .nilikuwa najiuliza sana ni jinsi gani Ukawa wanavyoweza kuvumilia matusi,kebehi..matambo,dhihaka .toka asubuhi mpaka jioni ,kwa kweli nimewadharua sana aina ya viongozi ndani ya ccm.
 
Nathubutu kujiuliza hili swali kwasababu nawaona wachangiaji wote waliobaki humu kwenye bunge la katiba wakisimama kuchangia hawazungumzii kitu cha maana au kujenga hoja za maana zinazohusu kufungu namba 6, badala yake wanaongea mipasho na kuwaponda UKAWA.
Kila mchangiaji haweki hoja madhubuti iliyo na mashiko kutetea serilaki mbili anazozitaka na kupambanua udhaifu wa serikali 3 wanazozitaka UKAWA.
The big deal kwao imekuwa kuongelea tundu lisu amemtukana nyerere, mara Haji Duni anaitwa babu wakati hana mjukuu, mara Mbatia hajui takwimu.
Sasa hizi posho wanazochukua wanazitendea haki gani??
Mimi naona hili bunge halitasaidia lolote zaidi ya upotevu wa pesa tu.
Swali; je ni kweli ukiwa m-CCM unajiwekea mipaka ya kufikiri na kupambanua hoja ambazo wananchi wanatarajia??

Hilo swali lako haliihitaji RESEARCH, si umewaona hata Dr. Mwakyembe na Prof. Shivji wanavyolamba matapishi yao??
 
Alichokisema Lipumba Leo bungeni
Mchango wa Mjadala wa Rasimu;

Mhe. Mwenyekiti gazeti la Mwananchi la tarehe 14 Aprili 2014 limeandika kuwa “Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ameanza kampeni kanisani kuwataka wananchi kupinga serikali tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, vinginevyo nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.”
Mhe. Lukuvi aliyasema haya katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika ibada ya kumsimika Mchungaji Joseph Bundala kuwa askofu. Hoja kama hiyo pia ilizungumzwa na Rais Kikwete wakati akilihutubia bunge Maalum tarehe 21 Machi 2014.
Ni kweli katika Rasimu ya Katiba taratibu imara za Mapato ya Serikali ya Shirikisho hazijawekwa vizuri. Serikali hiyo haina Mamlaka ya Mapato. Baada ya Rasimu ya kwanza kutolewa tatizo hilo nililichambua kwa kina katika mada niliyowasilisha katika Baraza la Katiba la TCD. Makala hii imetumiwa sana na Wajumbe wa Bunge hili. Hata hivyo wajumbe hawa hawanukuu ufumbuzi uliopendekezwa katika mada hii.
Baraza la Katiba la TCD chini ya Uenyekiti wa Augostin Lyatonga Mrema ulipendekeza muundo wa serikali tatu na utaratibu wa uchangiaji wa mapato toka serikali washirika kwa kadri mapato yanavyokusanywa na serikali washirika.
Zaidi ya asilimia 90 ya gharama za Shirikisho siyo mpya. Gharama za Rais wa Muungano za hivi sasa zitahamia kwa Rais wa Shirikisho.
Ikiwa tutakuwa na uwazi na uwajibikaji gharama hizo zitakuwa ndogo kuliko za sasa. Gharama za JWTZ, Polisi, Uhamiaji, Mambo ya nje zitahamia Serikali ya Shirikisho. Zote hizi siyo gharama mpya
Kwa sababu ya uzoefu wa “Akaunti ya Fedha ya Pamoja” na Tume ya pamoja ya Fedha, Rasimu ya Katiba haina pendekezo la kuwepo kwa chombo kinachoshirikisha serikali tatu kujadili na kukubaliana mgao wa mapato ya serikali za washirika kugharamia serikali ya Muungano.
Tume imependekeza ushuru wa bidhaa kuwa chanzo cha mapato ya kodi ya serikali ya shirikisho.Ni vyema mapato ya kugharamia serikali ya Muungano yakachangiwa na mapato ya serikali mbili.
Katiba itamke wazi serikali za washirika zitachangia sehemu ya mapato yao yote kwenye serikali ya Muungano. Kuzuia migongano ni vyema tukafikia muafaka wa asilimia ngapi ya mapato ya serikali yaende kwenye shughuli za Muungano.
Kwa kutumia uchambuzi wa gharama za Muungano uliofanywa na Tume ya Pamoja ya Fedha, gharama za Muungano ni asilimia 20 ya mapato ya Muungano. Katiba inaweza kutamka kuwa kiasi kisichopungua asilimia 20 ya mapato yote ya serikali za Washirika yatawasilishwa katika mfuko wa serikali ya Muungano kwa kadri mapato hayo yanavyokusanywa.
Izingatiwe kuwa kwa utaratibu huu bado mshirika mwenye uchumi mkubwa atakayechangia sehemu kubwa ya gharama za Muungano.
Katiba itamke kuwa Bunge la Shirikisho litatunga sheria ya kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa sehemu yake ya mapato yanayokusanywa na serikali za Washirika yanawasilishwa kwenye mfuko wa Serikali ya Shirikisho.
Mamlaka ya kukusanya mapato inaweza kusimamiwa kwa pamoja kati ya serikali ya shirikisho na serikali za washirika ili kuhakikisha kuwa mapato yanayokusanywa na kuyawasilisha kwa serikali ya Washirika na serikali ya Muungano kwa uwiano uliokubaliwa.
Miaka ya 1960 na 1970 Mamlaka ya kukusanya mapato ya Afrika Mashariki ilikusanya kodi za mapato, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa Kenya, Tanganyika na Uganda na kuziwasilisha kwenye serikali husika.
Sera za kodi zilitungwa na nchi husika lakini kodi za nchi hasa ushuru wa forodha zilifanana.
Kama CCM ingekuwa na nia njema utaratibu wa kukusanya kodi na kugawa kwenye serikali ya shirikisho na serikali za washirika siyo rocket science ni jambo ambalo linaweza kuwekwa vizuri ndani ya katiba. Katiba ya muungano kama katiba mama ijenge misingi mizuri ya usimamizi wa fedha za umma na ukusanyaji wa kodi.
Mhe. Mwenyekiti, Rasimu ya Katiba imeletwa na Tume ya Rais ili tuijadili na kuipitisha. Rasimu hii siyo ya CUF, siyo ya CHADEMA, siyo NCCR Mageuzi, siyo ya Wapemba. Ni Rasimu ya Tume ya Rais Kikwete.
Katika hotuba yake katika kanisa la Methodist Mhe. Lukuvi pia alisema “Serikali tatu zikipita ni wazi kuwa hata makanisa yatafungwa kwani nchi haiwezi kuwa na amani tena.”
Lukuvi alisema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Baadaye alipotakiwa kufafanua kauli yake, Lukuvi alisema alichokizungumza kanisani hapo ni mawazo yake binafsi ambayo yanafanana na Watanzania wengi, akiwamo Rais Jakaya Kikwete.
Mhe. Mwenyekiti je lengo la serikali mbili ni kuwadhibiti Wazanzibari wasianzishe dola ya Kiislam kama alivyoeleza Mhe. Lukuvi? Baada ya hotuba ya Mhe. Lukuvi “Askofu Bundala alisema kanisani hapo kwamba ili kudumisha Muungano ni vyema Katiba ya Zanzibar ifutwe ili iwepo moja ya nchi moja ambayo inadumisha Muungano.”
Mchakato wa kupata katiba mpya unapaswa kuwa wa maridhiano, Vipi Waziri anayemuwakilisha Waziri Mkuu anaenda kanisani na kusema Wazanzibari wanaotaka kuwa na nchi yao hawawezi kujitegemea, bali wanataka Serikali ili wapate nafasi ya kujitangaza kuwa ni nchi ya Kiislamu.
Kama hamuitaki Rasimu ya Katiba ya Tume ya Rais kwa nini mmetuleta hapa kwa gharama kubwa. Tunaambiwa Bunge limekarabatiwa kwa shilingi bilioni 8.2. Je ni utaratibu wa 10 percent uliohamasisha kutumia fedha nyingi huku serikali ikiamini kuwa Rasimu ya Katiba haifai kabisa.
Mjadala umekuwa wa matusi na siyo wa kujenga hoja. Kauli za kibaguzi zimetolewa dhidi ya Wapemba, dhidi ya Waarabu, dhidi ya Wahindi. Wajumbe wa Bunge Maalum wanashangilia kauli za kibaguzi. Tunaanza kupanda mbegu ya intarahamwe wa Tanzania. Kauli za kibaguzi ni kinyume cha maadili na tunu za Watanzania.
Kwa utaratibu wa kanuni 33 (7), Baada ya taarifa ya kamati namba moja hadi namba kumi na mbili kuwasilishwa, taarifa hizo zitajadiliwa kwa kipindi kisichozidi siku tatu. Baada ya mjadala kamati ya uandishi inapaswa kuanda vifungu vya sura hizo mbili ili vipigiwe kura na wajumbe wa pande mbili za muungano. Hilo halitafanyika.
Kufuatana na Ratiba, Bunge Maalum litaendelea hadi tarehe 25 Aprili bila kupiga kura na kufanya maamuzi ya vifungu vya sura hizi mbili kinyume na kanuni. Bunge linaahirishwa hadi Agosti bila kufanya maamuzi ili kuwapa nafasi CCM watafute theluthi mbili ya pande zote za Muungano kwa njia yeyote ile.
Tunaopigania katiba ya wananchi hatuwezi kubariki uchakachuaji wa maoni ya wananchi. Wakati umefika tuwaache CCM muendelee na vioja vyenu kwani hamtaki kuandika katiba inayotokana na mawazo ya wananchi badala yake mnahamasisha chuki dhidi ya Wapemba, Wahindi na Waarabu na kupandikiza uhasama wa kidini.
cc Ritz , FaizaFoxy na CHAMVIGA
===>Mnaojikomba nao hamuwajui,yao ndio hayo jipangeni sasa.
Source😛age ya Facebook ya Julius Mtatiro :https://www.facebook.com/julius.mtatiro/posts/10200979622253116
 
Last edited by a moderator:
Inabidi uhurumiwe sana kwa kuwa kana kwamba leo ndiyo unaingia hapa duniani lakini mimi sikushangai sana kwa kuwa ni miongoni mwa watu ambao akili yao wameshikiwa na ukawa pamoja na vyama vyao vya siasa.

kama wewe ambavyo ccm umekufanya umedumaa kiakili huwezi kufikiri nje ya box maskin.!
 
Hakuna mwenye utashi wa kiasiasa kati ya wale,tupo hapa tutaona mwisho wao,leo lipumba yupo pamoja na prof safar ijulkane kuwa Safar aliikimbia cuf baada ya kuona hawez chukua mikoba ya lipumba,sasa leo lipumba,safar,mbowe,mbatia hahahahahahaaha hakuna anaetaka kuwa chin hapo watazid aibika tu wananch ndo sisi na sisi ndo tumeipigia kura CCm chaguz ndogo zote inashinda kwa kishindo...


Sent from my iPhone using JamiiForums.


.....ni mbulumundu tu atakeye kataa S 3
 
kabla ya kuandika tafakari kwanza, UKAWA tuliwatuma kwenda kujadili rasimu yenye maoni ya watanzania na si maoni ya ssm.:israel::israel:
Laana ya NYERERE na KARUME kwa matusi yenu kwao imewarudieni
 
Kama atakuwa hajatoka, basi atakuwa amejidhalilisha sana! Kuendelea kubaki na hao interahamwe itakuwa ni aibu kwake!
 
Akili za udongo hata ukiongezewa mawazo mengi kama yapatikanayo JF utabakia vumbi tu...utakapofunguka macho 'udondoshe magamba' utagundua ulivyo na akili iliyo dhoofu!

Wanaokula posho wa wizi na kuweka wajumbe 201 hadi waganga wa kienyeji Kinje- (ajenti wa shetwani), hao ndio unawaona wanakula halali na kuuharibu uhalali wa Rasimu ya Katiba? Your poor mind shall cost you your entire intelligence and knowledge!

....well said Mkuu
 
nibora walivyo toka yani wabunge ambao wanamawazo tofauti na ccm wanawazomea yani hawana hata amani ya kuchangia.... ila akiongea mbunge wa ccm anapigiwa makofi akitukana pia anapigiwa makofi. yani ni zomea zomea tuuu mpaka mwisho
 
Ni kweli kabisa. Hata yule mbunge wa bunge maalum kutoka Znz aliyaona hayo.
 
Umoja ni nguvu Daima Umoja huu hadi Tanganyika Huru,
Zanzibar Huru,
Kisha Shirikisho Huru la Tanzania,
Wametoka huku wengine wakashangilia lakini moyoni wanaumia.
Tumewapokea kwa
Sauti ya Uchungu,
Sauti ya Mabadiliko
Sauti ya Tanganyika,
Sauti ya Zanzibar,
Sauti ya Shirikisho huru Tanzania.
Sauti ya kuulinda Muungano daima,
Mtatucheka huku mkiumia lakini kumbukeni walianza wachache sasa wako wengi,walioneka Chadema wanapenda kutoka sasa wote wameelewa kutoka ni kuepusha machafuko mjengoni;
Maoni yatu wananchi lazima yaheshimiwe,
Mmeshindwa kuyaheshimu basi msitulaumu kwa uwamuzi wetu Mungu yuko na sisi,
Tumevuka bahari tumekuwa kitu kimoja sasa Zanzibar na Tanganyika,
UKAWA DAIMA;
 
Akili za udongo hata ukiongezewa mawazo mengi kama yapatikanayo JF utabakia vumbi tu...utakapofunguka macho 'udondoshe magamba' utagundua ulivyo na akili iliyo dhoofu!

Wanaokula posho wa wizi na kuweka wajumbe 201 hadi waganga wa kienyeji Kinje- (ajenti wa shetwani), hao ndio unawaona wanakula halali na kuuharibu uhalali wa Rasimu ya Katiba? Your poor mind shall cost you your entire intelligence and knowledge!

Kichaa n kichaa tu hata umvishe suti ataivua na kubaki mtupu,ndo kitu unachokionesha hapa,umeshindwa jibu hoja povu limekutoka,ukitaja mawakala wa shetani uspomtaja Tundu lissu naww utakuwa agent wa Shetani pia....kama posho wamechukua za mpaka tr 31 kwann wasingelitoka jana,?kwann iwe leo huo ubaguz umeanza leo????mungu kukunyima akili za darasan hakumaanisha hata maish ufail pia huo n udhembe wako bnafs hata ustafe mchaw,


Sent from my iPhone using JamiiForums.🔩🔨
 
Back
Top Bottom