Unabii wa Danieli hauna uhusiano na Brexit
CL[/QUOTE]
SERIKALI KUU YA ULIMWENGU YA UINGEREZA NA MAREKANI NA MIGUU YA CHUMA NA UDONGO
Kuna uhusiano gani kati ya kichwa cha saba cha mnyama-mwitu na ile sanamu kubwa sana? Uingereza, kutia ndani na Marekani, zilitokana na Milki ya Roma. Hata hivyo, namna gani miguu ya hiyo sanamu? Biblia inasema kwamba miguu hiyo ni mchanganyiko wa chuma na udongo. (Soma Danieli 2:41-43.) Maelezo hayo kuhusu miguu yanatimia kipindi kilekile ambacho kichwa cha saba, yaani, Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani inapoibuka na kupata umaarufu. Kama vile ambavyo kitu kilichotengenezwa kwa mchanganyiko wa chuma na udongo kilivyo dhaifu kuliko kitu kilichotengenezwa kwa chuma tu, vivyo hivyo pia Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani ni dhaifu kuliko serikali ambayo ilitokana nayo. Hilo lilitukia jinsi gani?
Nyakati nyingine, kichwa cha saba cha mnyama huyo kimeonyesha nguvu kama za chuma. Kwa mfano, kilithibitisha kwamba kina nguvu kiliposhinda Vita vya Kwanza vya Ulimwengu. Katika Vita vya Pili vya Ulimwengu, kichwa cha saba kilionyesha pia nguvu kama za chuma. Hata baada ya vita hivyo, mara kwa mara kichwa cha saba kilionyesha nguvu kama za chuma. Hata hivyo, tangu mwanzoni, chuma hicho kimechanganyika na udongo.
Kwa muda mrefu watumishi wa Yehova wamekuwa wakijitahidi kuelewa kile ambacho miguu ya sanamu hiyo inafananisha. Andiko la Danieli 2:41 linasema kwamba mchanganyiko wa chuma na udongo ni “ufalme,” mmoja, si falme nyingi. Kwa hiyo, udongo unafananisha vitu fulani katika utawala wa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani, ambavyo vinaifanya iwe dhaifu zaidi kuliko Milki ya Roma iliyokuwa na nguvu kama chuma ambacho hakijachanganywa na kitu kingine chochote. Udongo unafananisha “uzao wa wanadamu,” au watu wa kawaida. (Dan. 2:43) Katika Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani, watu wameinuka na kudai haki zao kupitia kampeni za kupigania haki za raia, vyama vya wafanyakazi, na harakati za kutafuta uhuru. Watu wa kawaida wanafanya iwe vigumu kwa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani kutenda kwa nguvu kama za chuma. Pia, maoni ya kisiasa yanayopingana na matokeo ya uchaguzi yanayokaribiana na ambayo hayaonyeshi wazi mshindi yamedhoofisha uwezo wa hata viongozi maarufu, hivi kwamba hawana mamlaka ya kutekeleza sera zao. Danieli alitabiri hivi: “Sehemu moja ya ufalme huo itakuwa yenye nguvu na nyingine itakuwa dhaifu.”—Dan. 2:42; 2 Tim. 3:1-3.
Katika karne ya 21, serikali ya Uingereza na ya Marekani zimeendelea kuwa na uhusiano wa pekee, na mara nyingi zinashirikiana katika kushughulikia masuala ya ulimwengu. Unabii mbalimbali kuhusu ile sanamu kubwa sana na yule mnyama-mwitu unathibitisha kwamba wakati ujao hapatakuwa na serikali nyingine kuu ya ulimwengu ambayo itachukua mahali pa Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani. Huenda serikali hiyo kuu ya mwisho ya ulimwengu ya Uingereza na Marekani ikawa dhaifu zaidi kuliko serikali inayofananishwa na ile miguu ya chuma, lakini serikali hiyo haitavunjika yenyewe.
Je, idadi ya vidole vya miguu vya sanamu hiyo vina maana ya pekee? Fikiria jambo hili: Katika maono mengine, Danieli anataja idadi hususa, kwa mfano, idadi ya pembe zilizo kwenye vichwa vya wanyama mbalimbali. Idadi hizo zina maana. Hata hivyo, anapoeleza kuhusu ile sanamu, Danieli hataji idadi ya vidole vya miguu. Kwa hiyo, inaonekana kwamba idadi hiyo si muhimu sana kama vile ambavyo idadi ya mikono, vidole, miguu, na nyayo za sanamu hiyo si muhimu. Danieli anataja kihususa kwamba vidole vya miguu vingekuwa mchanganyiko wa chuma na udongo. Kutokana na maelezo yake, tunaweza kukata kauli kwamba Serikali Kuu ya Ulimwengu ya Uingereza na Marekani ndiyo itakayokuwa ikitawala wakati ambapo “jiwe” linalofananisha Ufalme wa Mungu litakapoipiga miguu ya sanamu hiyo.—Dan. 2:45.