Pre GE2025 Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA 2025: Tundu Lissu ashinda nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa kwa Kura 513 sawa na 51.5%

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Ni Mbowe au Lissu

  • Mbowe

    Votes: 179 14.7%
  • Lissu

    Votes: 1,038 85.3%

  • Total voters
    1,217
  • Poll closed .
Bila shaka utabubujikwa machozi ya furaha na kulia kwa kwikwi huku ukigalagala chini
 
CV ya Lissu ni kubwa sana ktk harakati za upinzani Tanzania. Naweza kusema huwezi kuwataja wapinzani wa CCM bila kumtaja Lissu. Licha ya huvyo Lissu hakumfikia marehemu Seif jinsi ya kuisumbua CCM.
Seif licha ya kutokuwa kiongozi mkuu wa Cuf yaani Mwenyekiti lkn aliitikisha sana CCM hadi kufikia miafaka zaidi ya 3 na hatimae ikaundwa serekali ya kitaifa.
Maalim alianziasha harakati za jino kwa jino lakini pia harakati za maridhiano.
Maalim alifariki akiwa na heshima kubwa ktk siasa za upinzani.
LISSU.
Lissu licha ya kuwa mpinzani lkn mtego aliongia ushammaliza kisiasa. Mtego wa kutaka kuisambaratisha chadema kupitia lema na Heche limemtoa kabisa ktk siasa za chadema.
Tumuombeeni sana Lissu ktk siasa za upinzani. Lilobaki aende CCM akamalizie maisha yake
Lissu nje ya chadema hawezi kuendesha siasa. Siasa za lissu litigemea chadema.
Kwa hivyo za kumuombea lissu baada ya kushindwa ni muhimu
 
CCM na mahaba kwa Mbowe imekujaje?, mbona inachekesha!!
 
Ni muhimu sana Watanzania na wadau wa JF na wanaCHADEMA kwa ujumla kumuweka kwenye maombi huyu mwanafalsafa wa siasa za Tanzania.

Ninaposema kwa KIBALI cha Mungu, namaanisha kuwa, shetani atakapominywa na kutopewa nafasi ya kuvuruga basi KUSUDI la Mungu linatimia. Sisi wanadamu ni kusimama na Mungu kwenye mpango wake bila kukengeuka

Anaungwa mkono na makundi mengi ya wapenda haki na Watanzania kwa ujimla. Hata CCM inatetemeka wanaposikia jina lake na hofu kubwa ni pale atakaposhinda uenyekiti.

Tanzania inahitaji ukombozi wa pili ambapo hapa tumefikishwa na watawala waliojimilikisha nchi ambao hawataki Tanzania ipige hatua za maendeleo kwenye nyanja zote



Kila la kheri wajumbe,

Kila la kheri Tundu Antipas Lisu na Asanti Mbowe kwa kujidhihirisha uhalisia wako na usaliti dhidi ya harakati za ukombozi wa kweli wa nchi yetu



Mungu Ibariki Tanzania
Mungu ibariki CHADEMA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…