Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 59,045
- 94,974
Acheni unafikiWajumbe wameamua kuiua CHADEMA
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Acheni unafikiWajumbe wameamua kuiua CHADEMA
Huna akili ww, kwahy dunia mzima hawajalala? Em acha bangi hizoWatu hawajalala hadi asubuhi hii ikiwa ni pamoja na mabalozi wa nchi mbalimbali waliohudhuria uchaguzi Mlimani City. Haijapata kutokea.
CHADEMA imepoteza mvuto siku hizi. Yaani hata page 100 hazijafika!😂😂😂
Pesa sabuni ya rohoAcheni unafiki
Tayar gentleman 🐒
Unaweza kuta Boni yai anapewa hata za LISU, kwani nani anaona majina hapo 🙂View attachment 3209552
Boni Yai ana vibunda viwili vya kura, kibunda kimoja kipo mezani, kibunda kingine amekishika mkononi.
Mbowe kura hizi amezitoa wapi?🙂
Wakuu,
Leo mbali na kuwa ni Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA pia wanasherekea Miaka 32 ya CHADEMA kupata Usajili wa Kudumu, ambapo ulipatikana Januari 21, 1993.
Mbivu na mbichi kujulikana leo, tumeona mengi na kusikia mengi kila upande ukitetea kwake. Je, nani ataibuka kidedea? Nani atatolewa kimasomaso na wajumbe?
Katika uchaguzi huu wajumbe watachagua Mwenyekiti Taifa pamoja na Makamu Mwenyekiti kwa Bara na Zanzibar, ambako ushindani mkubwa upo kati ya Mbowe na Lissu kwa nafasi ya Uenyekiti, na Wenje na Heche kwa nafasi ya Umakamu Uenyekiti.
Je, ni Mbowe au Lissu? Ni Heche au Wenje?
Orodha ya Wagombea wote ni;
Mwenyekiti Taifa
Makamu Mwenyekiti Bara
- Freeman Mbowe
- Odero Odero
- Tundu Lissu
Makamu Mwenyekiti Zanzibar
- Ezekia Wenye
- John Heche
- Mathayo Gekul
- Hafidh Saleh
- Said Issa Mohammed
- Said Mzee Said
- Suleiman Makame Issa
Wagombea Wanatoa Salamu kwa Wageni Waalikwa na Wapiga Kura
Tundu Lissu
Lissu amshukuru Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe kwa kufanya nae kazi kwa kipindi cha miaka 20, licha ya kutofautiana kimitazamo lakini amekiri hawajawahi kugombana.
"Nimekaa pembeni ya Mwenyekiti wetu wa Chama mfululizo kwa miaka zaidi ya 20 na katika kipindi chote hicho hatajawahi kugombana, hatujawahi kupigana mimi na yeye binafsi. Ndio tumetofautiana kimsimamo lakini hatujawahi kugombani"
"Vyovyote itakavyokuwa leo, tutakuwa pamoja katika kukijenga chama chetu (Chadema)"
Freeman Mbowe
"Hiki chama tunawajibu wote wa kibinadamu na Wakimungu wakukilinda kwa gharama yoyote ile, na chama hiki hatutakiruhusu kwa gharama yoyote eti kwasababu pengine kura za mbowe hazikutosha au kura za Mhe. Lissu hazikutosha ama za Mhe. Odero yule mzee wetu wa kesho kuna mwanga kwamba kura hazijatosha".
"Uchaguzi huu usiwe vita unapashwa kuwa furaha ya ujenzi wa demokrasia"
"Wako watabiri wengi sana wamesema kuhusu uchaguzi wa CHADEMA, Mhe. Mbowe unaenda kukipasua chama, Mhe. Mbowe inakuaje, hawa ni wanademokrasia, wote kama mnavyowaona. Tofauti zetu kwenye mitazamo hii naamini tunakwenda kuizika mwisho wa kikao hiki tunanelea mbele stronger together"
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, ametoa taarifa kwa ufupi kuhusiana na hali halisi ya Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na Urais wa mwaka 2020.
Mnyika asoma maazimio ya kamati kuu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa (2024), ambapo yatapelekwa Mkutano Mkuu kwaajili ya kupendekezwa kupitishwa kama maadhimio ya mkutano mkuu wa chama.
Mnyika amehitimisha kwa kuwasilisha mapendekezo ya maazimio ya Mkutano Mkuu
Zoezi la uhakiki wa Wajumbe
Shughuli za uhakiki wa wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zinaendelea katika ukumbi wa Mlimani City.
Uhakiki huo unaongozwa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na kukamilika kwake kutaashiria kuanza kwa uchaguzi wa nafasi za uenyekiti na makamu wa chama hicho Taifa.
Wajumbe 996 wathibitishwa ni halali, zoezi la kura kuanza.
Updates za Matukio
- Mwamakula: Wajumbe wameambiwa kuipiga picha au kuweke alama karatasi ya kura kama ushahidi wa kuongezewa pesa baadaye
- Jumla ya wajumbe wanaoenda kupiga kura ni 996, zoezi la kupiga kura linaanza muda wowote kuanzia sasa
- Frank Mwakajoka kachaguliwa kuwa mwenyekiti wa uchaguzi
- Mgombea Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar: Vijana walipewa nafasi ya kukiongoza chama hawakufanya kitu
Weka halisi achana na katuniTayar gentleman 🐒
Ngoja Lissu apitishwe ili tukasheherekee vzrKaka twende ambiance aisee hizo nyapu cheap sana siziwezagi
Ngoja Mbowe atangazwe mshindi utaelewa.Kwanini chama kife? Hao Ndio Wajumbe au Wewe ni mjumbe?
CHADEMA ni imara sanaPesa sabuni ya roho
CHADEMA imepoteza mvuto siku hizi. Yaani hata page 100 hazijafika!😂😂😂
CHADEMA ni KUBWA Sana Sana
We mwenyewe umekesha, watu wapo YouTube channel wakimaliza huko wanarudi jamii forum
Sawa mkuu.CHADEMA ni KUBWA Sana Sana
Mbona malalamiko mapema hivi?Wajumbe wameamua kuiua CHADEMA