LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
Ungeweza kuishi mateso kama hayo kwenye Nchi yako mwenyewe? Sisi hatukupitia mateso kama hayo ila unaona kulikua na Vita vya Majimaji, kina Mkwawa, kimweri na wengine wakapigana sembuse wao?
Mkuu wengi humu fuata upepo tu wala hawajui kiini cha mgogoro huu. Mfano kila lawama ni Hamas ila ukiwauliza mbona West Bank hakuna Hamas na bado palestines wanauwawa kila siku hawana jibu.
 
Usiangalie kilichoanza tarehe 7, angalia miaka 75 iliopita, hayo ya tarehe 7 ni matokeo ya mateso ya zaidi ya miaka 70 imagine wewe ni mpalestina
Historia ina mambo mengi yenye kuleta maudhi, mafunzo na majuto!

Ni sababu zipi za msingi ziliwafanya Waarabu wa Kipalestina (Wapalestina) kuukataa mpango wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1947 (UN partition plan)?
 
Historia ina mambo mengi yenye kuleta maudhi, mafunzo na majuto!

Ni sababu zipi za msingi ziliwafanya Waarabu wa Kipalestina (Wapalestina) kuukataa mpango wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1947 (UN partition plan)?
Hivi mkuu leo wairan waende Un then Tanzania igawanywe pasu pasu, nusu wapewe wao nusu waliobakia kutakalika hapa? Doesn't make Sense huo uamuzi, Walivyokuja Wayahudi wa Ulaya Wapalestina waliwapokea, Kasome History ya baba yake Bela na Gigi Hadidi utaelewa What happened.

Unamuona mtu katoka Ulaya kachoka ana utapiamlo unamkaribisha kwako unamsaidia unampa chakula, then mtu huyo huyo anakuja kukutoa kwako anafunga Nyumba na wewe mwenye Nyumba unakua Homeless.

Issue Mkuu si Uyahudi na Palestina, Issue ni Zionism na wanaoleta Fujo hilo eneo ni Hao Settlers, kila siku wanajiongezea maeneo, hata hio Nchi inge pigwa pasu still wanajiongezea Eneo.
 
Mkuu wengi humu fuata upepo tu wala hawajui kiini cha mgogoro huu. Mfano kila lawama ni Hamas ila ukiwauliza mbona West Bank hakuna Hamas na bado palestines wanauwawa kila siku hawana jibu.
Hoja kwamba West Bank hakuna Hamas sio sahihi!

Hamas ipo pia West Bank. Ina wafuasi wanaoiunga mkono. Tofauti ya Hamas ya West Bank na ile ya Gaza ni kwenye ngazi ya utawala. Hamas inatawala Gaza pekee ambako ndiko ngome yake iliko, lakini ina ushawishi na wafuasi ndani ya West Bank vilevile.

Labda kuwepo na hoja na ushahidi kwamba hayo mauaji yanayofanyika West Bank ni ya makusudi (kitu ambacho hakipaswi kuungwa mkono, kulingana na sheria ya kimataifa) na sio matokeo ya vurugu (violence) ambapo pande zote zinaweza kudhurika.
 
Lakini, kwa mujibu wa historia na sheria ya kimataifa, hakujawahi kuwepo nchi huru inayoitwa Palestina kwenye ardhi ambayo inahusisha Israel ya sasa. Kwa miaka mingi hata kabla ya Israel kupata uhuru mwaka 1948, hilo eneo limekuwa milki ya madola mengi ya kizamani.

Hiyo ni tofauti kabisa na Tanzania ambayo ni nchi huru na "mwenye nyumba" ni Mtanzania.

Eneo linaloitwa "Palestine" kabla ya ugomvi wa mwaka 1947 lilikuwa likikaliwa na watu wa jamii mbalimbali. Ndio maana kuna watu wanaitwa "Waarabu wa Kipalestina", pia kuna "Wayahudi wa Kipalestina". Jamii zote hizo zinadai kuwa hilo eneo ni makazi yao ya kihistoria.

Kwahiyo mtu yeyote atakayejitokeza kujimilikisha eneo lote, lazima ugomvi uwepo. Ndio maana ya kuletwa kwa pendekezo la UN partition ambalo Waarabu wa Kipalestina walilikataa.

Nafikiri tunapaswa kuutazama huu mgogoro katika perspectives zote!
 
Kwamba mkuu hujui kama West Bank watu wanauliwa kimakusudi tu?


Hio ni report ya UN kati ya Nov 2022 na March 2023 Wapalestina 614 ambao ni Civilian wameuliwa na Jeshi la Israel


Kuna watoto 34 na majina yao wa west Bank wameuliwa

Ukitaka hadi na Video Zipo, kuna video Askari wa Israel wana Sniper wanacheka kabisa wanalenga watoto wa Palestina wanawaua. Na wenyewe Israel ndio wanazi upload hizo video.
 
Niko hapa nacheki live huko central Gaza ni hatari tupu kunavyolipuliwa mfululizo usiku huu kumegeuka mchana. Sijui ni makombora gani haya wanayotumia israel yani unaona kitu kama jua halafu mwanga wake unatanuka. T14 Armata
 
Hawa ni washenzi hawana hata chembe ya utu ila utakuta kuna mswahili huku kashiba gongo zake anakwambia taifa teule, huku wazungu wengi wakiandamana kulaani udhalimu , watu weusi tuna roho mbaya sana
 
Kwa Historia ya Tanzania hakuna Nchi inayoitwa Tanzania kabla ya mwaka 1964, Je Iran wakija na Excuse hii ili wapewe Tanzania utawaelewa?

Palestina ipo maelfu ya miaka, Sababu ilikuwa ni Koloni la Nchi X, Y, Z haiondoi uhalali kwamba hapo waliishi watu. Hii ni Hela ya Palestina mwaka 1927.


Hii ni Ramani ya National Geography kabla ya 1948 na Physical copies zipo


Kuna Barua kibao Kuanzia Napoleon miaka ya 1700, Mpaka Ottoman miaka ya 1800 iki refer hilo eneo kama Palestina, ni propaganda za Zionist karibuni kwamba hilo eneo halikua Palestina na hakukua na Nchi ya Palestina.

Hio Barua ya Napoleon kwa Jews akitaka kuwapa Palestina.
 
Kichapo kipo pale pale
 
Kwa mujibu wa sheria ya kimataifa, mauaji dhidi ya watu wasio na hatia ni haramu. Pia nimesema, mauaji ya namna hiyo, kulingana na sheria ya kimataifa, hayapaswi kuungwa mkono.

Isitoshe, hakuna sheria ya kimataifa inayotoa uhalali wa kufanya mauaji ya raia wasio na hatia kama njia ya kulipa kisasi dhidi ya mtu fulani kwa kile ambacho umefanyiwa ama ulifanyiwa hapo kabla na mtu huyo.
 
Iran haiwezi kupata chochote Tanzania kwa sababu, kwa mujibu wa sheria ya kimataifa, Tanzania ni sovereign state. Hata kabla ya uhuru wa Tanganyika, Iran haikuwahi kuwa na mandate ya eneo lolote lile lililokuwa likikaliwa na wazawa wenye asili ya Tanganyika.

Hiyo ni tofauti na "Palestine" ambayo haikuwahi kuwa nchi huru kabla ya 1947, vilevile hata sasa hivi hakuna nchi huru inayoitwa "Palestina" inayohusisha eneo la Israel ya sasa.

Sarafu uliyoileta hapa ni sarafu ya Mamlaka ya Palestina (Palestine Mandate); mamlaka ambayo iliwekwa na Mwingereza chini ya masharti ya League of Nations. Hiyo sarafu iliwekwa na Mwingereza mwenyewe mwaka 1927 na haina uhusiano wowote na 'utaifa' wa kile kinachofahamika kama "Palestine".

Bahati nzuri ni kwamba, hiyo sarafu uliyoileta inathibitisha hoja yangu kwamba eneo ambalo linafahamika kama "Palestine" kwenye hiyo ramani ni eneo lililokuwa likikaliwa na watu wenye jamii mchanganyiko na sio milki au mali ya jamii moja pekee.

Sarafu ambayo Mwingereza aliwapatia "Wapalestina" wa kipindi kile ina alama ya utambulisho na maandishi yenye lugha tatu mchanganyiko ambazo ni Kiarabu, Kiingereza na Kiebrania. Maana yake ni kuwa, hukukuwa na taifa moja la Kiarabu lililokuwa likiitwa "Palestina".

Hii "Palestina" inayofikiriwa na kuzungumzwa sasa hivi kama "nchi huru ya Waarabu wa Kipalestina" ni tofauti kabisa na "Palestine" iliyokuwepo kabla ya 1947.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…