FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Nilishauri kwamba tuutazame huu mgogoro katika perspectives zote! Nina maswali kadhaa kwaajili yako:Unachoshindwa kuelewa na kuzingatia ni kwamba netanyahu na Zionists wenzie hawana uhusiano wowote na Hilo eneo la Palestine,si kwao,ndiyo maana nikakupa mfano wa lugha na Imani ya kiyahudi,Mimi muislam,siwezi sema saudia kwetu kisa mtume alizaliwa huko,waisriwa 'asili' waliokuwepo wakiishi bega kwa bega na wapalestine wao wakiwa minority,na hao real Jews/Israelis wanawapinga akina netanyahu,Zionism ni political movement iliyochanganywa na dini,netanyahu hapo Palestine Hana uhusiano napo,mfano wa Tanganyika na wakongo usiukwepe,Kuna wanyamwezi walienda Kongo zamani na mpaka Leo wapo huko na lugha yao inashabihiana na kinyamwezi,siku wakirudi tabora na kudai nchi yao itakua sawa!?
1) Ni kwa sababu zipi Wayahudi wanaofahamika kama "Zionists" hawana uhusiano na hilo eneo?
2) Je, Wayahudi waliotoka Ulaya na kwingineko na kuhamia "Palestine" chimbuko ama asili yao ni wapi hasa?
3) Ni nani alikuwa na uhalali (legality) wa milki ya eneo lililoitwa "Palestine" wakati wa Zionism?
Mfano wako kuhusu Wakongo nimeshauzungumzia. Sijaukwepa! Tanzania ni sovereign state. Hakuna uhalali wowote wa hao Wakongo kudai "nchi yao" ndani ya Tanzania bila ya Tanzania yenyewe kupoteza uhuru wake kwanza.
Vilevile, Tabora haijawahi kuwa nchi huru yenye mipaka inayotambulika. Kulingana na sheria ya kimataifa, mfano wako hauna uhalisia. Huwezi kudai kurudishiwa kitu ambacho haukuwa nacho hapo awali!